Tumaini Makene
JF-Expert Member
- Jan 6, 2012
- 2,642
- 6,071
Wazee wawili wastaafu wa nchi hii wako Channel Ten kwenye kipindi cha Je Tutafika. Nafikiri leo ndiyo siku yake (kama si marudio). Ni Dkt. Hansy Kitine na Dkt. Kiwanuka.
Mada ni uadilifu na uwajibikaji serikalini. Mzee Kitine kama kawaida yake...leo anasema anashangaa inakuwaje watu wachafu wameendelea kuteuliwa katika nafasi ya uwaziri baada ya MSUKO (hii yangu) mpya wa jana.
Anasema mathalani kuwa waziri mmoja amepewa fedha za nchi huko Comoro, Moroco na Libya, ametia mfukoni mwake. Amezifanya ni za kwake. Waziri huyo kwa sasa anajenga au kamaliza kujenga hoteli kubwa katika makao makuu ya moja ya mikoa ya Kusini mwa Tanzania.
Mzee Kitine anashangaa, anasema sasa huyo waziri anausaka urais, sasa kama sasa ni fisadi akiwa rais atakuwaje, ataacha kwa sababu kapata urais aliokuwa anautaka.
Kipindi ni kizuri. Wazee wanajenga hoja vyema juu ya uwajibikaji wa serikali na viongozi kwa wananchi. Kiwanuka anasema uongozi wakati wa Mwalimu ilikuwa ni utumishi. Unatumikia watu, si watu wakutumikie wewe.
Mada ni uadilifu na uwajibikaji serikalini. Mzee Kitine kama kawaida yake...leo anasema anashangaa inakuwaje watu wachafu wameendelea kuteuliwa katika nafasi ya uwaziri baada ya MSUKO (hii yangu) mpya wa jana.
Anasema mathalani kuwa waziri mmoja amepewa fedha za nchi huko Comoro, Moroco na Libya, ametia mfukoni mwake. Amezifanya ni za kwake. Waziri huyo kwa sasa anajenga au kamaliza kujenga hoteli kubwa katika makao makuu ya moja ya mikoa ya Kusini mwa Tanzania.
Mzee Kitine anashangaa, anasema sasa huyo waziri anausaka urais, sasa kama sasa ni fisadi akiwa rais atakuwaje, ataacha kwa sababu kapata urais aliokuwa anautaka.
Kipindi ni kizuri. Wazee wanajenga hoja vyema juu ya uwajibikaji wa serikali na viongozi kwa wananchi. Kiwanuka anasema uongozi wakati wa Mwalimu ilikuwa ni utumishi. Unatumikia watu, si watu wakutumikie wewe.