Kitimtim Kipawa - JK azuiliwa kupita

HEBU TUJULISHENI MLIOKO KIPAWA...mabomu ya machozi huko...ni aje wamemzuia mkuu wa nchi asipite?
Tangia watu wa Mbeya wampopoe mawe hakuna tena mambo ya Mh. Raisi kusimama bila ratiba, tena watu wenyewe wanaotaka awasikilize wana hasira!
 
Great,

Afadhali umetufahamisha walau kama hali imetulia. Ilikuwaje? Nani alikuwa anapiga mabomu hayo? Ili iweje? Kwanini wananchi watawanyishwe? Kwanini rais asiwasikilize kabla ya kuendelea na safari yake? Kipi muhimu kwake?

Rais?

Rais gani? Kwani nchi ina rais hii? Nchi ipo kwenye autopilot, na tuombee tu tusipate janga huyu msanii amalize miaka yake mitano, asiwe na uchu wa kuendelea. Zaidi ya hapo akitaka kuendelea tumtoe kwenye ballot box.

Nchi haina rais hii chonde chonde jamani msi expect anything from Kikwete.You will be only setting yourselves for a big disappointment.
 
Bahati mbaya sana, serikali inajivuruga yenyewe. Sio kweli kwamba Fidia inalipwa kwa kile kinachoitwa sheria mpya. Sheria Na. 47 ya 1967 bado ndio inatumika pote nchini. Kigezo kimoja kilichokuwa na utata ambacho kimebadilishwa na Sheria Na. 4 ya 1999 ni kile kinachohusu fidia kwa ardhi tupu.

Hao vijana wa Kikwete wameogopa kusema kwamba viwango wanavyotumia ni vile vya 1997(sio SHERIA YA 1967) ambavyo walivi-index pale wizarani. Serikali wamechelewesha malipo kwa zaidi ya miaka 10. Wakasita kurudi field kwenda kupima nyumba upya maana nyingi zimechakaa mno, nyingine hazimo tena na nyingine za wale wasioogopa wamezikarabati au kujenga upya kabisa. Walikuwa njia panda, maana wangeanza upya zoezi wananchi wengine wasingepata haki kwani physically hakuna kitu. Kwa ajili hio the only option ni kufanyia kazi data za enzi hizo lakini hawawezi kuwaeleza wananchi na wala kukaa nao waeleze shida zao.

If consulted wananchi wangeelewa tu na makubaliano yangefikiwa. Kuna uwezekano mdogo sana kwa kesi za wananchi kushinda mahakamani, maana sheria ile ndiyo inayotumika kutwaa na kufidia ardhi! Bado wananchi watateseka. CONSULTATION jamani, Honesty! Ukiwa mkweli, sijui TRANSPARENT wote hatutaingia mihasara ya kijinga jinga namna hii,,,,nimechukia sana
 
JESHI la Polisi jana lililazimika kutumia mabomu ya machozi, maji ya kuwasha na risasi za moto kutawanya mamia ya wakazi wa Kipawa waliotanda barabarani kwa nia ya kuuzuia msafara wa rais.
Wananchi hao walikuwa wakitaka kumfikishia Rais Jakaya Kikwete ujumbe wao wa kupinga kulipwa fidia ya kubomolewa nyumba zao kwa kutumia sheria ya mwaka 1967.
Sheria ya Ardhi ya 1999 inathaminisha ardhi na nyumba tofauti na sheria ya awali ambayo ilikuwa ikithaminisha nyumba pekee kwa kuwa ardhi ilikuwa mali ya serikali.
Sheria hiyo pia inamshirikisha mkazi kwenye mchakato wa tathmini, inatoa fedha za gharama za usafiri na kodi ya pango kwa kipindi cha miezi 36.
Serikali ya mkoa juzi ilitangaza kuanza kulipa fidia jana na ilipanga kuwa malipo hayo yafanyike ndani ya eneo la Gereza la Ukonga, hatua ambayo ilionekana kulenga kuepuka vurugu za wakazi hao.
Lakini badala ya kwenda Ukonga, wakazi wengi wa Kipawa, ambao wametakiwa wahame kupisha upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, waliamua kutanda kwenye Barabara ya Nyerere kwa lengo la kuzuia msafara huo wa rais ambaye alikuwa akitokea mkoani Mara.
Wakazi hao walitanda barabarani wakiwa wamevaa vitambaa vyeupe mikononi na mabango yaliyosomeka “sisi wakazi wa Kipawa hatudanganyiki na kulipwa fidia kwa sheria ya zamani" na "hakuna kusaini hundi kwa sheria ya zamani,” kauli ambazo wamekuwa wakizitumia kila wanapokutana kwenye harakati zao.
Kutokana na hali hiyo polisi ililazimika kutoa matangazo kwa kutumia kipaza sauti ikiwataka wakazi hao kutawanyika kwa madai kuwa mkusanyiko huo si halali na umekiuka sheria za nchi, lakini umati huo wa watu ulikaidi ukidai kinachoendelea kufanywa na serikali ni ubabe.
“Sisi tunapinga kulipwa fidia kwa sheria ya zamani; tumeshaiandikia serikali notisi ya siku tisini tukitaka ibatilishe utaratibu wake la sivyo tunakwenda mahakamani, inakuwaje leo serikali ianze kulipa fidia, kwa nini serikali inang’ang’ania sheria hiyo hata kukiuka notisi tulizokwishazifikisha mahakamani,” alihoji Rajabu Hussein mkazi wa Kipawa.
Wakazi hao walisema kinachofanywa na serikali ni usanii kwani wanaostahili kulipwa ni wao na si watu waliokwenda kupokea fedha hizo na kumtaka rais aingilie kati sakata hilo.
Wakazi hao walidai watu wanaopokea fidia wamepandikizwa na si wakazi wa Kipawa huku wakisisitiza kuwa wakazi wa Kipawa ndio waliopo kwenye eneo hilo wakipinga sheria hiyo kutumika.
Wakati hayo yakiendelea, Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Evance Balama aliwasili katika eneo hilo na kueleza kuwa watu wa Kipawa ni wabaya na kwamba hawaitakii mema serikali yao.
“Polisi hakikisheni watu hawa wanatawanyika,”alisema Balama na kuondoka kuelekea uwanja wa ndege kwa ajili ya kumpokea rais aliyewasili jana kutokea mkoani Mara.
Kauli ya Balama ilionekana kama kichochea kwani kuanzia hapo askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), wakitumia mabomu ya machozi, walianza kuushambulia umati wa watu uliokuwa umekusanyika katika eneo hilo.
Polisi hao walikwenda mbali zaidi baada ya kuingia kwenye makazi ya watu karibu na barabara hiyo na kuwapiga na baadaye kumkamata mwenyekiti wao, Mulisa na wasaidizi wake.
Katika tukio hilo, polisi walimjeruhi mtu mmoja na kusababisha watoto watano kupotea.
Hali ilikuwa tofauti kwenye maeneo ya Gereza la Ukonga ambako idadi ndogo ya watu ilijitokeza kuchukua hundi za malipo ya fidia zao.
Akizungumza mara baada ya kuchukua hundi hizo, Hamisi Mvugalo, aliyejitambulisha kuwa ni mkazi wa Kipawa, alisema ameamua kuchukua fedha hizo baada ya kuridhika na kiwango alichokabidhiwa.
Alisema ameteseka kwa muda wa miaka 13 sasa, lakini baada ya kujua analipwa kiasi gani ameona kinatosha na atafanikiwa kujenga nyumba zake zote mbili na pia kupeleka watoto wake sekondari mwakani.
“Fedha ninayoipata inatosha. Mimi nina watoto wawili wanahitaji fedha kwa ajili ya karo, pia hela hiyo nimeona ni nyingi na itatosha hata kujenga nyumba zangu mbili,” alisema Mvugalo.
Serikali iliwazuia wakazi wa Kipawa kuendeleza makazi yao kwa ahadi ya kuwalipa fidia baada ya kufanya tathmini ya mali zao, lakini tangu tathmini hiyo ifanywe mwaka 1997, wakazi hao wamekuwa wakisubiri fidia bila ya mafanikio huku nyumba zao zikibomoka kiasi cha baadhi yao kulazimika kuhamia kwenye majengo ya Shule ya Msingi ya Kipawa kujihifadhi.
Lakini baada ya serikali kutenga fedha za fidia, ilitangaza kuwa itawalipa kwa kutumia Sheria ya Ardhi ya 1967, badala ya sheria ya mwaka 1999.
Afisa ardhi mwandamizi mkoa wa Dar es Salaam, Edgar Japhet alisema wamepanga kulipa fidia kwa wakazi wote wa eneo hilo kwa muda wa siku 45.
Alisema wamekadiria kuwalipa watu 100 kwa siku na kusisitiza kuwa kama idadi itaongezeka, watazidisha nguvu ili kuhakikisha wote wanalipwa.
Malipo hayo yalikwenda sanjari na notisi ya siku 45 kwa kila aliyepokea hundi kutakiwa awe amebomoa nyumba yake.
Msafara wa Rais Kikwete ulipita eneo hilo saa 8:05 mchana na kukuta pande zote za eneo la Kipawa zikiwa zimezingirwa na FFU waliokuwa chini ya Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ilala, Faustine Shilogile.


Source: Gazeti la Mwananchi
 
10_09_xajpr7.jpg

A Kipawa resident negotiating with the Field Force Unit (FFU) members who went to disperse the area's residents who blocked the road today with the aim to tell President Jakaya Kikwete who was coming from Butiama their compensation problems. (Photo by Yusuf Badi).

DARIUS MUKIZA, 15th October 2009 @ 09:40
Daily News

POLICE today used tear gas and canisters to disperse about one thousand Kipawa residents who aimed at stopping the Presidential entourage to address their grievances to President Jakaya Kikwete of not being compensated basing on the 1967 compensation act.

The move started around 9.00 am after the residents had discovered that the President was to pass on the area from Butiama where had attended the 10th commemoration of the Father of the Nation Julius Nyerere.

The residents prepared placards that had various massages and lined besides the road with white handkerchief in hands voicing that ‘help us our President'. Some of the posters read as ‘Kipawa Hatudanganyiki Kwa Vijisenti vya Fidia ya Sheria ya Zamani'.

Few minutes after they had lined up, police forces arrived on the place well armed to disperse the gathering after the order had been given.

It took almost ten minutes after the police had arrived on the scene, the order came from the Ilala District Commissioner Evans Balama saying, "these people are endangering the peace of this country, commander do your work."

After the order from the DC, the game started police used tear gases and canisters to disperse them.

The exercise that lasted for not more than ten minutes was also revenged by residents who threw stones to police forces but inured no one, but at some point the situation got worse as some police officers took refuge in car that belongs to the publisher of Daily News and Habari Leo, which was there for news coverage.

In the exercise, Juma Waziri, one of the resident injured by canisters on his feet and legs. Neighbors rushed him to hospital for medical check ups.

Moreover, after the exercise, some of the residents, including the chairman of the Kipawa
Mr Magnus Malisa, were arrested and taken to Ukonga police station.

In a dramatic turn of events, while their fellows were blocking the road to see the president, Daily News reporters witnessed other Kipawa residents lining for their compensation chequesat Ukonga prison Social hall, meaning that they agreed to be paid according to Compensation Act of 1967, contrary to what those at the road want.

The Regional land officer, Mr Edgar Japhet said that the exercise would continue and last after those willing to collect their cheques have appeared. He however, said those who were against the exercise were house tenants not house owners.

Mr Japhet' claims were disowned by a member of residents committee who do not accept the compensation according to 1967 Act Elias Justice who said the claims were cooked for political motives.

On his part Mr Andwindile Malaki who was among residents who appeared to collect their money according to old act called on other residents not to go against the exercise. A total of 1,007 residents signed up not to collect compensation according to old act.

The land compensation of 1967act among other things does not allow residents to be compensated in consideration of inflation rates and it does not recognize disturbance allowances. These benefits are recognized by the new act of 2001.
 
3339298.jpg

Friday, October 16, 2009 10:23 AM
ASKARI wa Kikosi cha kutuliza Ghasia (FFU), jana walilazimika kuwatawanya kwa mabomu ya machozi wakazi wa eneo la Kipawa, jijini Dar es Salaam waliokusanyika kando ya barabara ya Nyerere wakisubiri kumpokea Rais Jakaya Kikwete ili waweze kumweleza ma Wakazi hao walichukua hatua hiyo baada adha wanayoipata juu ya ulipwaji fidia wa nyumba zao kwa lengo la kupisha ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere wa Jijini Dar es Salaam.


Tukio hilo la kutimuliwa kwa mabomu hayolilitokea jana majira ya saa 7 mchana na zoezi kuisha kwenye majira ya saa 9 na kupelekea barabara ya Nyerere kutopitika kwa muda.


Hali katika eneo hilo ilichafuka kwani ilitawaliwa na harufu ya moshi wa mabomu ya machozi na kusababisha wananchi, hasa watoto kukimbia hovyo kusaka maji ya kunawa uso kupoza makali ya moshi huo wa mabomu, yaliyokuwa yakivurumishwa na FFU.


Katika zoezi hilo kuna baadhi ya watu walijeruhiwa na mkazi mmoja aliyetajwa kwa jina moja la Waziri, ameripotiwa kuwa ana hali mbaya baada ya kupigwa risasi na polisi wakati wakijaribu kuwatawanya wakazi hao.


Wakazi hao waliona ni bora wamsubiri JK ambaye alikuwa anatojkea Butiama katika maadhimisho ya miaka kumi ya kifo cha Malimu Nyerere yaliyofanyika Butiama na kuona wamsubiria hapo mana wakati anapita kuelekea Ikulu lazima angewaona wananchi hao barabarani.


Wananchi hao walikusanyika huku wakiwa wameshika vitambaa vyeupe pamoja na mabango mbalimbali, likiwemo lililosomeka kuwa ‘Kipawa Hatudanganyiki kwa Vijisenti vya Zamani vya Mwaka 1967”.



Wakazi hao waliweza kuwaambia waandishi kuwa walifikia hatua ya kukusanyika kwa lengo la kumweleza Rais Kikwete jinsi wanavyonyanyaswa juu ya ulipaji wa fidia zao ambazo wamekuwa wakisotea kwa miaka 12 sasa.


Aliongeza kuwa baada ya kujikusanya mahali hapo, baadaye walitokea askari polisi na kuwataka waendelee kukaa kwa amani wakimsubiri rais, lakini walishangaa kuona magari ya FFU yakiwatangazia watawanyike na walipokaidi, wakaanza kupigwa mabomu ya machozi.


Askari walifika eneo hilo na magari kama sita hivi, likiwemo gari lenye maji ya kuwasha na ma-defender mengine ya kawaida, baadaye wakamkamata Mwenyekiti wao Magnus Mulisa na wengine ambao ni Mapunda, Ally na Gobali.

Ndipo vurugu zilipoanzia kwani watu hao wakapigwa na kuanza kumwagiwa maji ya kuwasha, na hali iligeuka ilikuwa na kuwa mbaya sana katika eneod hilo.


Mwenyekiti wa waathirika hao alieleza kwa kusikitishwa kwake na kipigo walichopata kwani hakukuwa na dalili zozote za uvunjifu wa amani hasa ikizingatiwa kuwa lengo lao lilikuwa kumwona Rais Kikwete ili awasaidie.


“Tukio la leo limetufanya tukose imani na Jeshi la Polisi kwani hakututarajia kwa nchi kama yetu inayofuata utawala wa sheria, kutufanyia hivi, nasi tunaisubiri Serikali ya CCM mwakani kwenye uchaguzi ili tuiadhibu,” alisema.


Kabla ya sakata hilo katika wiki iliyopita, wakazi hao zaidi ya 1,000 walifungua kesi Mahakama Kuu ya Tanzania Kitengo cha Ardhi ili kupewa ufafanuzi wa sheria ipi kati ya ile ya mwaka 2001 na ya 1967, inayostahili kutumika kuwalipa fidia ili kupisha upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.


Waliamua kufungua kesi hiyo ili kujua mahakama itachukua uamuzi gani kati ya sheria hizo mbili itakayotumika kuwalipa fidia mana serikali inataka kuwalipa fidia kwa sheria ya mwaka 1967 na kugoma kuchukua malipo na kutaka sheria hiyo ibadilishwe.

Kwa miaka 12 sasa, wakazi wa Kipawa wamekuwa wakisotea malipo ya fidia kutokana na mpango wa serikali kutaka kuwahamisha ili kupisha upanuzi wa Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Julius Nyerere.

http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsId=3339298&&Cat=1
 
3339298.jpg

Friday, October 16, 2009 10:23 AM
ASKARI wa Kikosi cha kutuliza Ghasia (FFU), jana walilazimika kuwatawanya kwa mabomu ya machozi wakazi wa eneo la Kipawa, jijini Dar es Salaam waliokusanyika kando ya barabara ya Nyerere wakisubiri kumpokea Rais Jakaya Kikwete ili waweze kumweleza ma Wakazi hao walichukua hatua hiyo baada adha wanayoipata juu ya ulipwaji fidia wa nyumba zao kwa lengo la kupisha ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere wa Jijini Dar es Salaam.


Tukio hilo la kutimuliwa kwa mabomu hayolilitokea jana majira ya saa 7 mchana na zoezi kuisha kwenye majira ya saa 9 na kupelekea barabara ya Nyerere kutopitika kwa muda.


Hali katika eneo hilo ilichafuka kwani ilitawaliwa na harufu ya moshi wa mabomu ya machozi na kusababisha wananchi, hasa watoto kukimbia hovyo kusaka maji ya kunawa uso kupoza makali ya moshi huo wa mabomu, yaliyokuwa yakivurumishwa na FFU.


Katika zoezi hilo kuna baadhi ya watu walijeruhiwa na mkazi mmoja aliyetajwa kwa jina moja la Waziri, ameripotiwa kuwa ana hali mbaya baada ya kupigwa risasi na polisi wakati wakijaribu kuwatawanya wakazi hao.


Wakazi hao waliona ni bora wamsubiri JK ambaye alikuwa anatojkea Butiama katika maadhimisho ya miaka kumi ya kifo cha Malimu Nyerere yaliyofanyika Butiama na kuona wamsubiria hapo mana wakati anapita kuelekea Ikulu lazima angewaona wananchi hao barabarani.


Wananchi hao walikusanyika huku wakiwa wameshika vitambaa vyeupe pamoja na mabango mbalimbali, likiwemo lililosomeka kuwa ‘Kipawa Hatudanganyiki kwa Vijisenti vya Zamani vya Mwaka 1967".



Wakazi hao waliweza kuwaambia waandishi kuwa walifikia hatua ya kukusanyika kwa lengo la kumweleza Rais Kikwete jinsi wanavyonyanyaswa juu ya ulipaji wa fidia zao ambazo wamekuwa wakisotea kwa miaka 12 sasa.


Aliongeza kuwa baada ya kujikusanya mahali hapo, baadaye walitokea askari polisi na kuwataka waendelee kukaa kwa amani wakimsubiri rais, lakini walishangaa kuona magari ya FFU yakiwatangazia watawanyike na walipokaidi, wakaanza kupigwa mabomu ya machozi.


Askari walifika eneo hilo na magari kama sita hivi, likiwemo gari lenye maji ya kuwasha na ma-defender mengine ya kawaida, baadaye wakamkamata Mwenyekiti wao Magnus Mulisa na wengine ambao ni Mapunda, Ally na Gobali.

Ndipo vurugu zilipoanzia kwani watu hao wakapigwa na kuanza kumwagiwa maji ya kuwasha, na hali iligeuka ilikuwa na kuwa mbaya sana katika eneod hilo.


Mwenyekiti wa waathirika hao alieleza kwa kusikitishwa kwake na kipigo walichopata kwani hakukuwa na dalili zozote za uvunjifu wa amani hasa ikizingatiwa kuwa lengo lao lilikuwa kumwona Rais Kikwete ili awasaidie.


"Tukio la leo limetufanya tukose imani na Jeshi la Polisi kwani hakututarajia kwa nchi kama yetu inayofuata utawala wa sheria, kutufanyia hivi, nasi tunaisubiri Serikali ya CCM mwakani kwenye uchaguzi ili tuiadhibu," alisema.


Kabla ya sakata hilo katika wiki iliyopita, wakazi hao zaidi ya 1,000 walifungua kesi Mahakama Kuu ya Tanzania Kitengo cha Ardhi ili kupewa ufafanuzi wa sheria ipi kati ya ile ya mwaka 2001 na ya 1967, inayostahili kutumika kuwalipa fidia ili kupisha upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.


Waliamua kufungua kesi hiyo ili kujua mahakama itachukua uamuzi gani kati ya sheria hizo mbili itakayotumika kuwalipa fidia mana serikali inataka kuwalipa fidia kwa sheria ya mwaka 1967 na kugoma kuchukua malipo na kutaka sheria hiyo ibadilishwe.

Kwa miaka 12 sasa, wakazi wa Kipawa wamekuwa wakisotea malipo ya fidia kutokana na mpango wa serikali kutaka kuwahamisha ili kupisha upanuzi wa Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Julius Nyerere.

http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsId=3339298&&Cat=1



Waliokusanyika kumsubiri Kikwete Kizimbani

WAKAZI tisa wa Kipawa jijini Dar es Salaam, jana walipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala, wakituhumiwa kwa kosa la kukusanyika kutaka kumwona Rais Jakaya Kikwete bila kibali. Washitakiwa hao ambao Mwenyekiti wao Magnus Mulisa (48) ambae ni mfanyabiashara, Abdallah Dadi (30) mfanyabiashara, Athuman Gobali (75) mkulima, Ally Abdallah (57) na Joseth Laiser (25).

Wengine ni Juma Musa, Samwel Temba (34), Mathew Mapunda (35) na Teddy Giligisi (32) ambae ni mwanamke pekee katika kesi hiyo.


Kesi hiyo ilisomwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashitaka Mkuu wa Mahakama hiyo, Inspekta Naima Mwanga, mbele ya Hakimu wa Wilaya Joyce Minde.


Mwanga alidai kuwa watuhumiwa hao wanakabiliwa na makosa matatu likiwemo shitaka la kwanza wanadaiwa kumpiga askari polisi katika eneo hilo.


Alidai kuwa siku hiyo washitakiwa kwa pamoja, walimpiga kwa mawe askari wa Kituo cha Polisi Buguruni, D.2237 CPL Kija na kumsababishia maumivu makali ya mwili.


Kosa la pili kwa wakazi hao ni kufanya fujo ambapo ilidaiwa mahakamani hapo kuwa siku ya tukio, wakiwa kwenye eneo hilo walifanya ghasia hizo kwa lengo la kuvunja amani kwa wakazi wengine.


Katika shitaka la tatu, watuhumiwa hao wanadaiwa kukusanyika bila kibali na kuhatarisha amani katika eneo la Kipawa na maeneo ya jirani.


Washitakiwa walikana mashitaka hayo na kurudishwa rumande kwa kunyimwa dhamana hadi Oktoba 30, kesi yao itakapotajwa tena, na kudaiwa kuwa upelelezi haujakamilika.
 
Back
Top Bottom