Kitimtim Bungeni: Wenje atolewa nje ya Bunge

kweli ni aibu kwa bunge Samirnasri kaeleza vzuri utadhani mtumishi wa hansard, ishu ni mwenyekiti wa leo kuwa shabiki wa chama na kushau wajibu wake na kutaka kumkomoa Lisu, nadhani umefika wakati kwa watanzania kukataa kuburuzwa.
 
kuna malumbano kuhusu hoja ya tundu lissu kutakiwa awasilishe ushahidi wa waziri kusema uongo. Aliyeanzisha vita ni moses machali aliyehoji inakuwaje lissu awasilishe ushahidi saa tano asubuhi hii wakati yeye ni mbunge na kikao cha bunge kinaendelea, kwa nini asipewe muda awasilishe baadaye. Mwenyekiti kakomaa lissu awasilishe ushahidi saa tano. Baadae kaibuka wenje kuomba kutoa hoja ya kuahirisha mjadala wa bajeti ili bunge lijadili jambo la dharura ambalo yeye amesema lina maslahi kwa taifa. Mwenyekiti amegoma na kusema mjadala wa bunge unaweza kuahirishwa tu pale nchi inapokuwa kwenye vita na kwa sasa nchi haiko kwenye vita. Pamoja na hayo wenje aliendelea kusimama na kutaka kutoa hoja yake lakini mwenyekiti akamtishia kumtumia askari kumtoa wenje nnje. Wenje hakusikia kaendelea kudai ni jambo la dharula ambalo lina maslahi kwa taifa. Baadae mwenyekiti kamuagiza surgent akamtoe wenje nje, sajent akiwa njiani kuelekea kumtoa wenje nje ya ukumbi wa bunge tanesco wakachukua umeme wao huku mitaa ya mabibo, hivyo sijui kilichoendelea baada ya hapo, naomba anayeendelea kutazama bunge atujuze nini kimeendelea.

aisee mkuu nakupa tano kwa kupanga stori vema, utadhani namimi naangalia, nimecheka mpaka machozi hapo kwenye red dah... senks senks
 
Hahahahaha, binadamu hatuko sawa kwa kweli, lakini hii inathibitisha zaidi hoja za kifalsafa kuwa ni vigumu sana kuwa na premises za ovyo ukaishia na conclusion makini. Binafsi, nafikiri tuzipime hoja za Lukuvi zilivyo bila kuhusisha na mke wake kwa sababu kwa mtazamo wangu havijaonyesha uhusiano wowote hasa kwenye mjadala wa leo.
Mwenyekiti wa Bunge amefuata ushauri wa Waziri Lukuvi kwa vile mke wa Lukuvi na watoto wako Bungeni hivyo mwenyekiti hakutaka kuona waziri anaaibika mbele ya mke wake, jambo la kujiuliza ingekuwaje kama Wenje naye mke wake na watoto wake wangekuwa Bungeni- pangechimbika.
 
Ushahidi wa maneno hauwezi ukawa na maana yoyote. Kwa mbunge makini kama Lissu anapoongelea ushahidi nafikiri ni lazima awe na nyaraka zinazothibitisha hili. Na kama hauongozwi na ushabiki utakubaliana nami kuwa Lisu alishaanza kusoma hizo documents kuthibitisha kauli zake. Kwa hiyo alikuwa hapigi blabla za mdomo.
hapo kwenye RED-alitakiwa aachwe asome wote hadi uishe-wananchi tusikie-lakini wao wanachofanya wanataka akaukabidhi-sasa akishaukabidhi hakuna atakaye usikia tena-maana mifano ipo-hata uongo wa pinda ulipo kabiziwa kwa spika-haukusomwa tena-so hoja ni kwamba aachwe ausome-tufahamu madudu ya hawa watu wa magamba
 
huyo mwenyekiti wa zenji mbona mlaini sana! hapo ingefuata mkono tu zipigwe apatikane mshindi, iko siku heshima ya bunge itarudi
 
Wabunge wa Chadema wamezidi uhuni, muda wa ziada wa nini wakati Tundu Lisu alisema yuko tayari kutoa sasa hivi. Wanaharibu sana quality ya mijadala.

we pimbi kweli, Mh. Tundu Lissu alikuwa tayari kutoa ushahidi pale pale, na wakati mwenyekiti akiwa amempatia muda wa kuanza kutoa ushahidi wa uongo wa Waziri, mwana-magamba mmoja akaomba taarifa, na kutaka maswali yaendelee na Lissu atoe ushahidi tym ingine, na mwenyekiti akakubaliana na taarifa ya Magamba mwenzie !sasa wewe unaongea nini, au unakurupuka tu
 
Nafuatilia hoja hii kwa makini nimegundua kuna mfuasi wa magamba ambaye anajifanya haelewi kwamba CCM na ma spika wao wakiona mbunge wa upinzani anataka kuachia hoja kali wanamzuia kusema kwa hoja za kipuuzi na kusema tuletee kwa maandishi..kwa nini hawakumuacha wenje aseme anachoongea..angekuwa mbunge wa CCM anataka kutoa taarifa angezuiwa?acheni kuhongwa na magamba kuja kueneza upuuzi humu CCM wameishiwa,wamebaki kutumia akili za matope kwenye hoja nzito na masuala muhimu ya Taifa
 
Huku Arusha ngeleja ametukatili, endeleeni kutujuza yanayojiri wakuu
 
wabunge wa CCM wapo bungeni kwa maslahi ya Chama chao tu na si wananchi full stop!!
 
Sasa wenyeviti wazinzi wanaongoza bunge unatarajia nini???
 
Huu nao ni uongo and there are no statistics to substantiate the claims. Pamoja na CDM kuongeza viti bungeni bado hawajaweza kuipiku CCM na hii inadhihirishwa na idadi ndogo ya wabunge wa CDM ukilinganisha na CCM. Wangekuwa na busara, CDM wangetakiwa kuja na mkakati wa kujipanga ili kuongeza ushawishi wao kwenye jamii hasa kwa kutoa uwakilishi makini kama walivyofanya kina Slaa kuliko ulevi wanaoanza kuonyesha sasa.

@Thintank CCM wana 78%, the remaining inatoka upinzani. Please soma my comment again - nimesema upinzani (total) siongelei chama kimoja cha upinzani hapa maana hata tafsiri ya neno upinziani imekuwa modified na bunge la Makinda to include anything outside ccm-box.
 
Mwenyekiti alikubaliana naye kwa sababu hoja hiyo ilizingatia kanuni na ratiba ya shughuli za bunge. Kila kitu kinapangiwa muda wake na hicho hakikuwa kipindi cha ushahidi kilikuwa kipindi cha maswali na majibu. Isije wewe ndo umefungwa na ushabiki huoni vitu katika upana wake.
we pimbi kweli, Mh. Tundu Lissu alikuwa tayari kutoa ushahidi pale pale, na wakati mwenyekiti akiwa amempatia muda wa kuanza kutoa ushahidi wa uongo wa Waziri, mwana-magamba mmoja akaomba taarifa, na kutaka maswali yaendelee na Lissu atoe ushahidi tym ingine, na mwenyekiti akakubaliana na taarifa ya Magamba mwenzie !sasa wewe unaongea nini, au unakurupuka tu
 
Sasa unaambiwa mwenyekiti mbunge wa
"""dole""""
akili zake mnatarajiwa ziweje waungwana??wana vidole juu mnajua dole iko wapi
 
Mwenyekiti alikubaliana naye kwa sababu hoja hiyo ilizingatia kanuni na ratiba ya shughuli za bunge. Kila kitu kinapangiwa muda wake na hicho hakikuwa kipindi cha ushahidi kilikuwa kipindi cha maswali na majibu. Isije wewe ndo umefungwa na ushabiki huoni vitu katika upana wake.

Tangu lini wabunge wa ccm na spika/wenyeviti wao wakajua umuhimu wa muda? Tumeona kila siku wakishukuru wake zao, majirani, na kututangazia nani anamtumia nani sms. Ni kama ccm wao wana 36 in a day na sio 24! Hivi inakuwaje uchaguliwe mwezi wa october 2010, lakini unatoa shukrani (kwa dakika 3) kwa waliokuchagua, mwezi July 2011!?
 
Huu nao ni uongo and there are no statistics to substantiate the claims. Pamoja na CDM kuongeza viti bungeni bado hawajaweza kuipiku CCM na hii inadhihirishwa na idadi ndogo ya wabunge wa CDM ukilinganisha na CCM. Wangekuwa na busara, CDM wangetakiwa kuja na mkakati wa kujipanga ili kuongeza ushawishi wao kwenye jamii hasa kwa kutoa uwakilishi makini kama walivyofanya kina Slaa kuliko ulevi wanaoanza kuonyesha sasa.
Hebu fafanua huo ulevi ndugu!Maana hujaeleweka kabisa!
 
Back
Top Bottom