Kitilya wa TRA kupelekwa TANESCO ?

Duh! Makampuni mangapi yanayoendeshwa na Wazungu ambayo yamekuwa na scandals mbali mbali katika uendeshaji? Wazungu si matatizo ya nchi yetu hata siku moja. Kule Rwanda hakuna Wazungu pamoja na wahutu na Watusi kuuana kwa idadi kubwa mwaka 1994 sasa hivi nchi yao inafanya vizuri sana katika sekta nyingi tu pamoja na kuwa hawana Wazungu. Kagame alikataa kabisa kuajiri Wazungu katika nafasi nyeti ndani ya Serikali yake.

Siye kila aliye ndani ya TANESCO na ana nafasi ya juu utendaji wake ni mbovu wengi tu ni wachapa kazi wazuri sana ila wanaangushwa na Serikali DHAIFU ambayo imeamua kuitumia TANESCO kama mradi wao wa kutajirika

Kama Rwanda wameweza kuinyanyua nchi yao katika sekta mbali mbali kwa kuwatumia wazawa, basi na Tanzania inaweza kabisa kufanya hivyo.






kupata scandal kwa kampuni siyo sawa na kushindwa ongoza kampuni
hapa TZ makampuni yanayo perfom better yanaendeshwa na wageni
mostly wazungu...
1.TBL
2.VODACOM
3.TIGO
4.AIRTELL
5.STANBINC
6.CITYBANK
7.NMB
8. na mengineyo meengi

nitajie wewe kampuni inayo chechmea bongo huku inaendeshwa na Wazungu....

tukubali tu kuwa 'the culture of efficiency' hatuna bado.....
tukubali kushindwa na ku 'import hiyo culture'

Nasita kukubali hayo kwa sababu najiuliza ni mpaka lini? Kumbuka tuko miaka hamsini sasa!
Halafu tatizo kubwa liko kwetu wenyewe watanzania. Hatuwezi kufanya kazi pamoja, tuna cancer ya kuchongeana sana. Tena hata kwa wageni, tunaudhaifu mkubwa sana katika hilo na imani za kichawi zimetawala mno hadi Bungeni.

Lakini nataka tu nikuambie kuwa yule Meneja wa NHC -Mchechu anafanya vizuri. Anaweza kuliendesha shirika la TANESCO.
 
Kwanini iwe ni lazima kutaja kampuni iliyoshindwa kuendeshwa na Wazungu iwe Bongo tu? Mbona Rwanda nchi yao imeshikwa na wazawa na wanafanya vizuri katika sekta nyingi? Kama Wanyarwanda wameweza kuendesha taasisi zao kwa ufanisi wa hali ya juu kwa nini Watanzania tushindwe? Yako makampuni mbali mbali yaliyokuwa yanaendesha na Wazungu katika nchi mbali mbali duniani yaliyoshindwa na kupotea katika Ulimwengu wa kibiashara.

BAK, either hauzijui menejimenti za kiswahili au una ile kitu "mapenzi ya kweli" ambapo chongo hugeuka kengeza.

Mpaka mtu anaponda menejimenti ya kiswahili ujue ameshaziona na kuzilinganisha na za wenzetu wa mbele. Angalau mpe benefit of doubt.
 
Maundumula,
Duuh mkuu umesema kweli. Kumbe tunajifilisi wenyewe halafu tunashangaa nani anatuloga! Anyway, kuna wakati bora tuwarudishe wazungu maana tunaweza kuwa na aibu kidogo kuliko hivi tunavyoendesha hilo shirika. Uchumi wetu utakuwaje kama kila siku tunawasha vibatari? na hata kama tutaongeza generation, with no displine on payment it is like wasting resources! Nimekupata mkuu and it is a challenge to us all.

Yap boss,

Tanesco inuliwa na madeni na huu umeme expensive wa mafuta wakati gas ipo songo songo ya kumwaga. Sijui kwa nini hawajafikiria kufunga mitambo huko huko Songo songo.
 
Yap boss,

Tanesco inuliwa na madeni na huu umeme expensive wa mafuta wakati gas ipo songo songo ya kumwaga. Sijui kwa nini hawajafikiria kufunga mitambo huko huko Songo songo.

Do you know how much the pay for fuel? The price is way above the market price for a good reason. Ndio maana coal na gesi ya songosongo sio muhimu sana kwa power production kwa sasa
 
...Yale yale!!! Kwa mafanikio yepi aliyoyapata TRA hadi apelekwe TANESCO? Si ndiye huyu aliyeshindwa kubuni mikakati ya kuongeza mapato ya Serikali na pia aliyeisababisha nchi kupoteza shilingi bilioni 500 pale kampuni ya kihindi ilipoamua "kuwekeza" nchini!?
Siyo kubuni tu mikakati, ameshindwa kabisa kukusanya kodi hata kwa sheria na taratibu zilizopo na sijui mpaka sasa yupo TRA kwa maslahi ya nani?
 
Back
Top Bottom