Kitilya wa TRA kupelekwa TANESCO ?

Mkataba wowote ule ulioingiwa kwa njia za udanganyifu na kisha wahusika kushindwa kutimiza masharti ya mkataba ule ya kufua umeme ni mkataba batili. Kama Serikali ingekuwa makini katika kuipanga kesi yake basi TANESCO ingeshinda katika kesi ile lakini wahusika wakuu toka Serikalini walikuwa wameshahesabu mgao wao toka kwa fisadi Rostam Azizi hivyo hawakuhakikisha umakini katika utetezi wa kesi yao dhidi Fisadi Rostam na mwenzie Al Alawi.

Kama Serikali iliweza kupinga hukumu ya kesi yake dhidi ya Valambhia na kukataa kulipa mabilini ya pesa kwa kampuni hiyo. Basi pia Serikali hii DHAIFU ikiwa makini inaweza kabisa kufanya hivyo. Kumbuka pesa hizo zilitakiwa kulipwa tangu December 2010 lakini kutokana na kupinga kwa Watanzania pamoja na hii Serikali DHAIFU kuridhia kulipa pesa hizo hazijalipwa na kama tukiweza kusimamia zislipwe hadi 2015 na CHADEMA kuchukua nchi basi Mafisadi ndani ya Serikali waliokuwa wanaumezea mate mgao wao haramu toka kwa mafisadi Rostam na Al Alawi hawataona hata senti tano toka hazina.


Wewe wacha pumba, wewe unaijuwa mikataba kuliko majaji wa mikataba ya kibiashara? Hakuna cha chadema wala nini, Nyerere mwenyewe muulize alifanywa nini na Tiny wa LONRHO. Mpaka kafa hana hamu nae alipojidai kutaifisha biashara zilizo na mikataba, alikiona cha mtema kuni.
 
Wewe wacha pumba, wewe unaijuwa mikataba kuliko majaji wa mikataba ya kibiashara? Hakuna cha chadema wala nini, Nyerere mwenyewe muulize alifanywa nini na Tiny wa LONRHO. Mpaka kafa hana hamu nae alipojidai kutaifisha biashara zilizo na mikataba, alikiona cha mtema kuni.

Hakuna pumba hapo magamba, weye magamba unaona Pumba ili kutetea magamba wenzio kama Serikali ilisharidhia kulipa hiyo pesa tangu 2010 sasa inakuwaje tena wakabadili maamuzi yake ya kulipa pesa na kuanza kujikanyagakanyaga? Kama zingekuwa ni pumba basi Serikali hii DHAIFU ingetamka kwamba tunakubaliana na hukumu ya mahakama ya kibiashara hivyo tutalipa pesa hizo. Walioingia mkataba na Richmond ni Serikali na siyo TANESCO lakini Serikali hii DHAIFU baada ya kupindisha taratibu za kuingia mkataba sasa inaisakizia TANESCO ndio wabebe jukumu la kulipa. Soma hiyo Article hapo juu uone utata kuhusu kizungumkuti cha mkataba huu batili.

 
TANESCO kuwalipa Dowans giza nene
Mwandishi Wetu

Toleo la 168
12 Jan 2011
RAIA MWEMA



  • Uharaka wa Ngeleja, Werema watia shaka


    WAKATI Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werama wakiwa tayari kutumia kodi za wananchi kuilipa kampuni ya Dowans, kasi ya kutaka kampuni hiyo kulipwa inatia shaka, Raia Mwema, imebaini.

    Shaka hiyo ikiachwa, utata umeendelea kuibuka kuhusu nani hasa atakayelipwa fedha hizo kutokana na mvutano uliopo kuhusiana na wamiliki halisi wa Dowans na mtangulizi wake, Richmond Development LLC.

    Ngeleja na Werema wamekuwa na haraka ya kutaka malipo yafanyike huku kukiwa na baadhi ya kesi zilizowahi kutolewa hukumu na Mahakama ya Tanzania ili zifidiwe lakini zikagonga mwamba kwa zaidi ya miaka 10 sasa.

    Moja ya kesi hizo ni ile iliyokuwa ikimhusu mfanyabiashara Devram Valambhia, aliyetakiwa kulipwa na Serikali shilingi bilioni 60 katika kesi ambayo iliunguruma kwa muda mrefu huku Serikali ikishindwa kila mara.
    Msingi wa kesi hiyo ni mfanyabiashara Valambhia kuidai Serikali dola 55 milioni kutokana na kuiuzia Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, magari kutoka Chekoslovakia.

    Serikali ilikuwa ikihangaika na kesi hiyo kwa kukata rufaa na kushindwa kila mara huku ikitumia mawakili wa kukodi wanaoelezwa kuwa nao waligharimu shilingi bilioni nane.

    Kutokana na Serikali kuhangaika kutokutaka kumlipa mfanyabiashara huyo ililazimika kukata rufaa nyingi na kutumia fedha za kukodi mawakili kiasi cha Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kutilia shaka mwenendo huo.

    Wasiwasi wa CAG ulijikita katika malipo makubwa waliyokuwa wakilipwa mawakili waliokuwa wakisimamia kesi hiyo kwa niaba ya Serikali.

    Katika harakati za kuzuia malipo hayo Serikali iliwahi kuielekeza Benki Kuu kutokutoa fedha kwa ajili ya kumlipa Valambhia na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) alikiri kwa baadhi ya vyombo vya habari kuhusu kuelekezwa, hasa baada ya kuwapo ushauri kuwa malipo hayo yafanyike nje ya Mahakama.

    Wasiwasi huo unajitokeza katika wakati ambao Serikali imetaja wamiliki wa kampuni ya Dowans Tanzania itakayolipwa mabilioni hayo kama hukumu ya Mahakama ya Kibiashara ya Usuluhishi inavyoelekeza. Mahakama hiyo imetaka Dowans Tanzanaia Ltd ilipwe Sh bilioni 94.

    Hata hivyo, rekodi za baadhi ya wamiliki hao ambao wote ni raia wa kigeni hazipatikani moja kwa moja kwenye mtandao wa kompyuta. Wakati Hon Sung Woo anayetajwa kuwa mmiliki wa Dowans kutoka Singapore na Guy Arthur Picard wa Canada, taarifa zao haziko wazi kwenye mtandao.

    Tayari mawaziri William Ngeleja wa Nishati na Madini, na Samuel Sitta wa Uhusiano wa Afrika Mashariki ambaye pia alikuwa Spika wa Bunge lililopita, wametofautiana kuhusu kufanya malipo hayo.

    Waziri Sitta anaamini kuwa kabla ya waziri kutangaza rasmi kutaka kuilipa kampuni hiyo, uamuzi huo ulipaswa kujadiliwa na Baraza la Mawaziri kwanza lakini pia anaamini kuna mianya ya kisheria kupinga kufanywa kwa malipo hayo.

    Kuhusu hukumu hiyo ya Novemba 15 mwaka jana, Ngeleja aliweka bayana kuridhika na uamuzi huo kuwa mkataba wa TANESCO na Dowans ulivunjwa kabla ya wakati na hivyo kustahili kulipwa.

    Kwa hatua hiyo, Dowans italipwa dola milioni 65.8 za Marekani sawa na shilingi bilioni 94 na si shilingi bilioni 185 ambazo zimekuwa zikiripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari nchini.

    Hata hivyo, alisema fedha hizo zitalipwa mara Dowans itakaposajili hukumu hiyo katika Mahakama Kuu ya Tanzania.
    Katika hati yake ya mashitaka, Dowans iliomba kulipwa dola milioni 149 na TANESCO kwa kuvunja mkataba wa kuzalisha megawati 100 za umeme, lakini Mahakama ya usuluhishi ilihukumu ilipwe milioni 65.8.
    Wakati hayo yakiendelea, Dowans na Richmond wameshitakiana nchini Marekani baada ya kutofautiana kuhusiana na biashara waliyorithishana na TANESCO.
 
Kwanza atueleze kama DEEP GREEN, MEREMETA, RICHMOND, and EPA victims hasa Jitu Patel, Manji, Rostam wanalipa kodi kiasi gani. Na kwa utaalam wake wa kodi ameshindwaje kuishauri serikali kuhusu kodi za mirahaba za madini and the like. Hafai kabisa kupelekwa TANESCO maana TRA ameshindwa, tena sana!!! Hivi si alitakiwa kustaafu kwa kuwa tayari ametimiza 60 au naye ni miongoni mwa wale watumishi wenye vyeti fake vya kuzaliwa kama ilivyo kwa mtuhumiwa fake wa Dr. kipenzi Ulimboka?
 
Suala kubwa sio kutoweza kwa wazawa, bali kutowezeshwa na kupewa uwanja wa kuweza kufanya yale tuoanayo kuwa magumu. Walio huko Rwanda miongoni mwao ni WaTz. ndio wanafanya mambo tunayotamani yatokee, serikali imeruhusu wafanye na waweze kufanikiwa, kwetu tunawabana na kufurahia kushindwa kwao kwa maumivu ya Watanzania wote.
 
Hakuna pumba hapo magamba, weye magamba unaona Pumba ili kutetea magamba wenzio kama Serikali ilisharidhia kulipa hiyo pesa tangu 2010 sasa inakuwaje tena wakabadili maamuzi yake ya kulipa pesa na kuanza kujikanyagakanyaga? Kama zingekuwa ni pumba basi Serikali hii DHAIFU ingetamka kwamba tunakubaliana na hukumu ya mahakama ya kibiashara hivyo tutalipa pesa hizo. Walioingia mkataba na Richmond ni Serikali na siyo TANESCO lakini Serikali hii DHAIFU baada ya kupindisha taratibu za kuingia mkataba sasa inaisakizia TANESCO ndio wabebe jukumu la kulipa. Soma hiyo Article hapo juu uone utata kuhusu kizungumkuti cha mkataba huu batili.


Mkataba wa Dowans umeusoma, au tukuwekee hapa, ule ulikuwa ni wa Serikali? wacha kuzuwa ulikuwa ni TANESCO.

Hiyo mitambo iko wapi sasa? wacha kuupoteza umma.

Halafu eti Serikali wameisukumia TANESCO wakati hao Dowans ndio walishtaki, waende wakashtaki mtu wasie na mkataba nae si kesi ingetupiliwa mbali?

Soma huu hapa:
ICC Case No. 15947/VR: Dowans (Claimant) and TANESCO (Respondent)
 
TANESCO kuwalipa Dowans giza nene
Mwandishi Wetu

Toleo la 168
12 Jan 2011
RAIA MWEMA



  • Uharaka wa Ngeleja, Werema watia shaka


    WAKATI Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werama wakiwa tayari kutumia kodi za wananchi kuilipa kampuni ya Dowans, kasi ya kutaka kampuni hiyo kulipwa inatia shaka, Raia Mwema, imebaini.

    Shaka hiyo ikiachwa, utata umeendelea kuibuka kuhusu nani hasa atakayelipwa fedha hizo kutokana na mvutano uliopo kuhusiana na wamiliki halisi wa Dowans na mtangulizi wake, Richmond Development LLC.

    Ngeleja na Werema wamekuwa na haraka ya kutaka malipo yafanyike huku kukiwa na baadhi ya kesi zilizowahi kutolewa hukumu na Mahakama ya Tanzania ili zifidiwe lakini zikagonga mwamba kwa zaidi ya miaka 10 sasa.

    Moja ya kesi hizo ni ile iliyokuwa ikimhusu mfanyabiashara Devram Valambhia, aliyetakiwa kulipwa na Serikali shilingi bilioni 60 katika kesi ambayo iliunguruma kwa muda mrefu huku Serikali ikishindwa kila mara.
    Msingi wa kesi hiyo ni mfanyabiashara Valambhia kuidai Serikali dola 55 milioni kutokana na kuiuzia Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, magari kutoka Chekoslovakia.

    Serikali ilikuwa ikihangaika na kesi hiyo kwa kukata rufaa na kushindwa kila mara huku ikitumia mawakili wa kukodi wanaoelezwa kuwa nao waligharimu shilingi bilioni nane.

    Kutokana na Serikali kuhangaika kutokutaka kumlipa mfanyabiashara huyo ililazimika kukata rufaa nyingi na kutumia fedha za kukodi mawakili kiasi cha Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kutilia shaka mwenendo huo.

    Wasiwasi wa CAG ulijikita katika malipo makubwa waliyokuwa wakilipwa mawakili waliokuwa wakisimamia kesi hiyo kwa niaba ya Serikali.

    Katika harakati za kuzuia malipo hayo Serikali iliwahi kuielekeza Benki Kuu kutokutoa fedha kwa ajili ya kumlipa Valambhia na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) alikiri kwa baadhi ya vyombo vya habari kuhusu kuelekezwa, hasa baada ya kuwapo ushauri kuwa malipo hayo yafanyike nje ya Mahakama.

    Wasiwasi huo unajitokeza katika wakati ambao Serikali imetaja wamiliki wa kampuni ya Dowans Tanzania itakayolipwa mabilioni hayo kama hukumu ya Mahakama ya Kibiashara ya Usuluhishi inavyoelekeza. Mahakama hiyo imetaka Dowans Tanzanaia Ltd ilipwe Sh bilioni 94.

    Hata hivyo, rekodi za baadhi ya wamiliki hao ambao wote ni raia wa kigeni hazipatikani moja kwa moja kwenye mtandao wa kompyuta. Wakati Hon Sung Woo anayetajwa kuwa mmiliki wa Dowans kutoka Singapore na Guy Arthur Picard wa Canada, taarifa zao haziko wazi kwenye mtandao.

    Tayari mawaziri William Ngeleja wa Nishati na Madini, na Samuel Sitta wa Uhusiano wa Afrika Mashariki ambaye pia alikuwa Spika wa Bunge lililopita, wametofautiana kuhusu kufanya malipo hayo.

    Waziri Sitta anaamini kuwa kabla ya waziri kutangaza rasmi kutaka kuilipa kampuni hiyo, uamuzi huo ulipaswa kujadiliwa na Baraza la Mawaziri kwanza lakini pia anaamini kuna mianya ya kisheria kupinga kufanywa kwa malipo hayo.

    Kuhusu hukumu hiyo ya Novemba 15 mwaka jana, Ngeleja aliweka bayana kuridhika na uamuzi huo kuwa mkataba wa TANESCO na Dowans ulivunjwa kabla ya wakati na hivyo kustahili kulipwa.

    Kwa hatua hiyo, Dowans italipwa dola milioni 65.8 za Marekani sawa na shilingi bilioni 94 na si shilingi bilioni 185 ambazo zimekuwa zikiripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari nchini.

    Hata hivyo, alisema fedha hizo zitalipwa mara Dowans itakaposajili hukumu hiyo katika Mahakama Kuu ya Tanzania.
    Katika hati yake ya mashitaka, Dowans iliomba kulipwa dola milioni 149 na TANESCO kwa kuvunja mkataba wa kuzalisha megawati 100 za umeme, lakini Mahakama ya usuluhishi ilihukumu ilipwe milioni 65.8.
    Wakati hayo yakiendelea, Dowans na Richmond wameshitakiana nchini Marekani baada ya kutofautiana kuhusiana na biashara waliyorithishana na TANESCO.

Watu wanaongelea kesi mahakamani wewe unaleta habari za magazeti. hivi nyinyi watu huwa mnasoma shule zipi? au ndio mazao ya NECTA?
 
Mkataba wa Dowans umeusoma, au tukuwekee hapa, ule ulikuwa ni wa Serikali? wacha kuzuwa ulikuwa ni TANESCO.

Hiyo mitambo iko wapi sasa? wacha kuupoteza umma.

Halafu eti Serikali wameisukumia TANESCO wakati hao Dowans ndio walishtaki, waende wakashtaki mtu wasie na mkataba nae si kesi ingetupiliwa mbali?

Soma huu hapa:
ICC Case No. 15947/VR: Dowans (Claimant) and TANESCO (Respondent)

Acha uzushi weye fisadi Zomba alias Faiza Foxy weka ushahidi hapa jamvini pale nilipozuwa kama nilikuwa TANESCO.

Mwananchi yeyote yule ambaye anatetea mafisadi na kukandamiza maslahi ya nchi yake hata pale ambapo kuna ushahidi wa kutosha (mkataba wa Richmond/Dowans ulikuwa ni batili utapiga kelele mpaka povu zikutoke, lakini ukweli ndio huo)unaonyesha kwamba nchi yake inadhulumiwa ni wa kuogopwa kama UKOMA....Source BAK.
 
Hakuna cha kuchemsha, mashirika yote ya umma yaliyoshindwa kuendeshwa kifaida na Serikali watu binafsi wameyachukuwa bila ruzuku ya Serikali na wanafanya vizuri tu. Mfano mzuri wa shirika kubwa ni NBC. Ilikuwa ni hasara tupu, sasa tunaona wanalipa kodi nyingi tu. TBL?

Mkuu hayo mashirika unayotolea mfano yanajipangia kila kitu based on market forces, tanesco siyo hivyo, bei zao wanapangiwa na ewura, kiukweli bei ya umeme tunayolipa ni below operating costs, ukitaka uamini ninachokwambia linganisha bei zetu za umeme na za nchi nyingine hata zile ambazo tunalingana nazo kiuchumi. Kifupi suala la tanesco usichukulie kirahisi rahisi hivyo!
 
Mkuu hayo mashirika unayotolea mfano yanajipangia kila kitu based on market forces, tanesco siyo hivyo, bei zao wanapangiwa na ewura, kiukweli bei ya umeme tunayolipa ni below operating costs, ukitaka uamini ninachokwambia linganisha bei zetu za umeme na za nchi nyingine hata zile ambazo tunalingana nazo kiuchumi. Kifupi suala la tanesco usichukulie kirahisi rahisi hivyo!

Below operating cost si kwa kuwa walishindwa kuwekeza on time. Unafikiri umeme wa kukodisha majenereta utaufuwa kama wa maji au wa nuclear? Steigler Gorge ilipendekezwa toka wakati wa Nyerere na gharama zilikuwa ni kama 10% tu ya gharama za leo. Wapi?

Sasa hii Tanesco nayo ipo njiani, sheria za ushindani wa ufuaji umeme Kikwete kisha zi saini, zinafanyiwa maboresho tu na tutaanza kuona likibaki kama ilivyo TTCL wapo kama hawapo.
 
Acha uzushi weye fisadi Zomba alias Faiza Foxy weka ushahidi hapa jamvini pale nilipozuwa kama nilikuwa TANESCO.

Mwananchi yeyote yule ambaye anatetea mafisadi na kukandamiza maslahi ya nchi yake hata pale ambapo kuna ushahidi wa kutosha (mkataba wa Richmond/Dowans ulikuwa ni batili utapiga kelele mpaka povu zikutoke, lakini ukweli ndio huo)unaonyesha kwamba nchi yake inadhulumiwa ni wa kuogopwa kama UKOMA....Source BAK.

Hiki hapa nini?
quote_icon.png
By BAK
Hakuna pumba hapo magamba, weye magamba unaona Pumba ili kutetea magamba wenzio kama Serikali ilisharidhia kulipa hiyo pesa tangu 2010 sasa inakuwaje tena wakabadili maamuzi yake ya kulipa pesa na kuanza kujikanyagakanyaga? Kama zingekuwa ni pumba basi Serikali hii DHAIFU ingetamka kwamba tunakubaliana na hukumu ya mahakama ya kibiashara hivyo tutalipa pesa hizo. Walioingia mkataba na Richmond ni Serikali na siyo TANESCO lakini Serikali hii DHAIFU baada ya kupindisha taratibu za kuingia mkataba sasa inaisakizia TANESCO ndio wabebe jukumu la kulipa. Soma hiyo Article hapo juu uone utata kuhusu kizungumkuti cha mkataba huu batili.

Soma hiyo halafu useme kama sio kupindisha maneno ni nini? Serikali ipi au TANESCO ipi ilikuwa na mkataba na Richmond ulioamuliwa mahakama ya kibiashara? nimekuwekea juu hapo mpaka kesi namba na nani mdai na nani mdaiwa bado tu unakataa? Ni DOWANS walioshtaki si Richmond wacha kuendelea kubisha ujinga. Nakuwekea tena hapa chini:

Soma huu hapa:
ICC Case No. 15947/VR: Dowans (Claimant) and TANESCO (Respondent)
 
Below operating cost si kwa kuwa walishindwa kuwekeza on time. Unafikiri umeme wa kukodisha majenereta utaufuwa kama wa maji au wa nuclear? Steigler Gorge ilipendekezwa toka wakati wa Nyerere na gharama zilikuwa ni kama 10% tu ya gharama za leo. Wapi?

Sasa hii Tanesco nayo ipo njiani, sheria za ushindani wa ufuaji umeme Kikwete kisha zi saini, zinafanyiwa maboresho tu na tutaanza kuona likibaki kama ilivyo TTCL wapo kama hawapo.

Yes, hapo kwa red umenena mkuu
 
Hiki hapa nini?


Soma hiyo halafu useme kama sio kupindisha maneno ni nini? Serikali ipi au TANESCO ipi ilikuwa na mkataba na Richmond ulioamuliwa mahakama ya kibiashara? nimekuwekea juu hapo mpaka kesi namba na nani mdai na nani mdaiwa bado tu unakataa? Ni DOWANS walioshtaki si Richmond wacha kuendelea kubisha ujinga. Nakuwekea tena hapa chini:

Soma huu hapa:
ICC Case No. 15947/VR: Dowans (Claimant) and TANESCO (Respondent)

Badilika na kuanza kutetea maslahi ya nchi badala ya yale ya mafisadi. Inaelekea hujui hata details za mkataba kati ya Serikali na Dowans. Walioingia mkataba na Richmond ni Serikali na siyo Dowans baada ya wizi wao kufichuka wakauruka mkataba na kudai TANESCO ndio wanaotakiwa kuilipa Dowans. Acha kuonyesha ujuha wako.

 
Na Saed Kubenea - Imechapwa 05 January 2011

dowans_123.jpg



VIGOGO ndani ya serikali wanatuhumiwa kupanga njama za kutaka kuilipa inyemela mabilioni ya shilingi kampuni ya Dowans, kabla taratibu muhimu kuhitimishwa.

MwanaHALISI lina taarifa kuwa Dowans Tanzania Ltd., imewasilisha ankara zake Hazina, tayari kwa malipo kabla maamuzi kusajiliwa mahakama kuu.
Wakati taarifa hizo zikivuja, umetokea utata wa kampuni ipi hasa ya Dowans ilipwe, kwani kuna makampuni mawili yaliyojitokeza.

Kwa mujibu wa nyaraka zilizopo, kampuni ya Dowans Holdings SA (Costa Rica) ndiyo ilikuwa na mkataba na Tanesco kupitia kurithi mkataba wa kampuni ya kufua umeme ya Richmond.

Bali uamuzi wa Mahakama ya Kimataifa ya usuluhishi wa migogoro ya Biashara (ICC) wa 15 Novemba 2010, unaagiza Tanesco kulipa Sh.185 bilioni kwa makampuni yote mawili.
Makampuni hayo ni Dowans Holdings SA (Costa Rica) na Dowans Tanzania Limited.

Utata huo unaongezeka kwa vile wakati wote wa mgogoro wa Richmond na Dowans, hakukuwa na Dowans Tanzania Limited ambayo sasa imetinga katika maamuzi ya ICC.

Nayo kampuni ya Dowans Holdings SA (Costa Rica), hata hivyo iliwahi kutajwa na msajili wa makampuni nchini Costa Rica kuwa haijawahi kusajiliwa nchini humo.
Kuibuka kwa taarifa hizi kumekuja wiki mbili baada ya gazeti hili kuripoti kuwa Dowans ni mradi wa vigogo watatu wakubwa ndani ya serikali na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Taarifa kutoka ndani ya serikali zinasema, mpango wa kulipa makampuni hayo unasukwa kwa ustadi mkubwa na watumishi wawili –mmoja kutoka wizara ya nishati na madini na mwingine ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali (AG).

Alipoulizwa Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkullo kuhusu njama za kutaka kulipa Dowans kinyemela alisema, "Hapa ninapozungumza na wewe niko Kilosa. Sina taarifa za karibuni za ofisini." Mkullo alikana pia kujua iwapo Dowans wamewasilisha ankara kwa ajili ya malipo.

Kwa mujibu wa sheria za usuluhishi nchini na zile za kimataifa, uamuzi wa ICC sharti usajiliwe katika mahakama kuu ya Tanzania.
Aidha, kwa mujibu wa makubaliano yaliyopo katika mkataba kati ya Dowans Holdings SA (Costa Rica) na Tanesco, yote yaliyokubaliwa ndani ya mkataba yatafuata sheria za Tanzania.
Hata hivyo, taarifa zinasema, msukumo wa kutaka malipo hayo kufanywa kinyemela, umefuatia kutajwa katika mwenendo wa kesi, mbunge wa Igunga, Rostam Aziz.

"Hapa kuna kitu kinafichwa. Rostam hataki kesi hii isajiliwe hapa, maana jina lake limetajwa ndani ya kesi hii zaidi ya mara tatu. Hivyo anajua kuwa iwapo itasajiliwa ataumbuka," ameeleza ofisa mmoja wa serikali.

Naye mjumbe mmoja wa Bodi ya Tanesco aliyezungumza kwa sharti la kutotajwa gazetini amethibitisha kuwa ankara za madai ya Dowans tayari zimewasilishwa serikalini kwa hatua zaidi.

"Bodi ya Tanesco iliarifiwa jambo hili katika kikao chake kilichofanyika 21 Desemba 2010, na kila mmoja alishtuka," ameeleza mtoa taarifa.
Alisema, "…wanaleta ankara za madai hata kabla mahakama kuu haijasajili kesi yao? Hapana! Tukasema, sisi bodi hatuwezi kuidhinisha malipo haya…"
Kutajwa kwa Rostam katika shauri la Dowans kulifuatia kubanwa na majaji wa mahakama hiyo, mfanyakazi wake mmoja kutoka kampuni ya Caspian.

Mfanyakazi huyo aliyekuwa anahudhuria bila kukosa vikao vyote vya mahakama vilivyokuwa vikifanyika katika hoteli ya Kilimanjaro Kempinski, alieleza mahakama, "…niko hapa kufuatilia maslahi ya bosi wangu."
Mtoa taarifa anasema, "Yule bwana aliulizwa na wale majaji, mbona kila siku anaingia mahakamani na hatoki mpaka muda wa kesi unamalizika."

Anasema, "Ndipo yule kijana akajibu, ‘nimetumwa na bosi wangukumwakilisha.'" Mahakama ikataka kujua huyo bosi ni nani? Ndipo akamtaja Rostam," anaeleza mtoa taarifa wa gazeti hili.

Anasema mara baada ya kutaja jina la Rostam, majaji waliokuwa wanasikiliza shauri lile, haraka wakauliza, ‘Kwani Rostam ni nani katika Dowans?' Yule bwana akajibu, ‘Ni mwanahisa…'"

Kuna taarifa za kuaminika kuwa mmoja wa watu wawili waliosaini makubaliano ya kuhamisha mkataba kutoka Richmond kwenda Dowans, ni Henry Surtees, Mwingereza anayedaiwa kuwa mtumishi wa kampuni ya Rostam ya Caspian.

Wiki iliyopita, gazeti la kila siku la Mwananchi lilimnukuu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema akisema, Dowans ilisajiliwa nchini Costa Rica na Rostam ndiye aliyepewa nguvu ya kisheria kusimamia malipo hayo.

Werema hakuzungumzia kwa undani hatua ya wanaojiita wamiliki wa Dowans kumpa Rostam nguvu hizo za kisheria.
Tarehe 7 Februari 2008, Rostam alikana kumiliki aina yoyote ya hisa kwenye kampuni mbili – Dowans na Richmond.

Mmoja wa wanaotajwa kuwa wamiliki wa Dowans katika nyaraka za sasa zilizopo ofisi ya usajili wa makampuni (BRELA), Brigedia Jenerali Sulaiman Mohamed Yahya Al Adawi amekana mara kadhaa kuifahamu kampuni hiyo.


Naye raia wa Canada, Andrew James Tice anayeonekana katika nyaraka za sasa za BRELA, aliwahi kuwa meneja uzalishaji katika kampuni ya Songas na baadaye kushika nafasi hiyo katika kampuni ya Richmond.

Kwa mujibu wa nyaraka mbalimbali ambazo gazeti linazo, Tanesco na Dowans wamekubaliana kuwa maamuzi yoyote ya suala hilo, ni lazima yafuate sheria za Tanzania.

Ibara ya 14 ya mkataba wao inasema pamoja na suala hilo kufikishwa ICC, pale ambapo kutatokea mgogoro, bado sheria za ndani ya Tanzania zitatumika wakati wa kufikia utatuzi.

Ibara ya 17 ya sheria ya usuluhishi inasema, mara baada ya maamuzi husika kutolewa, yatasajiliwa na mahakama kuu na baada ya hapo itachukuliwa kuwa ni amri halali ya mahakama ya nchi.

Nchini Costa Rica, ambako Dowans inadaiwa kusajiliwa, hakuna rekodi zozote inazoonyesha kuwapo kwa kampuni hiyo. "Dowans si kampuni halali ndani ya Costa Rica," inasema barua kutoka ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali nchini Costa Rica.

Barua hiyo ilisainiwa na Marianela Jimenez, Jumamosi ya 3 Agosti 2008 na kutumwa ofisi ya katibu wa Bunge la Jamhuri, saa 11:09 jioni ya siku hiyo.
Mmoja wa wanasheria nchini ameliambia gazeti hili kuwa serikali haistahili kulipa hata shilingi kwa Dowans kwa kuwa kampuni hiyo ilinunua mkataba kutoka kwa kampuni feki – Richmond.


Amesema, "Hata hatua ya Dowans Holding kuingiza kampuni ya Dowans Tanzania Limited katika madai yao, wakati wakijua fika kwamba kampuni hiyo siyo iliyosaini hati ya kuhamisha mkataba, ni kinyume cha taratibu na sheria za makampuni."
Kampuni ya Dowans ilirithi mkataba kutoka kampuni nyingine yenye utata ya Richmond ambayo ilipewa kazi ya kufua umeme kuanzia Januari 2007 hadi Juni 2008.
 
CAG's ruling on who should pay Dowans
Sunday, 22 May 2011 22:50

dowanssite.jpg

By Bernard James,
The Citizen Reporter

Dar es Salaam. The Controller and Auditor General has added his voice to the chorus opposing payment by Tanesco of Sh94 billion compensation to Dowans for breach of contract.Instead, Mr Ludovick Utouh says the government should take full responsibility for the payout if the High Court dismisses the petition contesting the award.

The International Chamber of Commerce (ICC) awarded the compensation to Dowans SA and Dowans Tanzania Limited after concluding that Tanesco was in breach of the contract it entered into with Richmond Development Company in 2008, which was later transferred to Dowans SA.

However, it is not clear who is supposed to shoulder the burden, with Tanesco saying the government had the final say on the contract. Mr Utouh says in a letter to the Finance and Economic Affairs ministry that he had studied developments leading to the agreement, and concluded that the government should take responsibility for the compensation after interfering in Tanesco's contract mandate and obligations.

The CAG has also suggested that the government reviews Tanesco's debt portfolio and ease the burden on the public utility arising from contracts in which the State is involved."This will enable Tanesco to be evaluated on fair grounds and be held accountable for its own decisions," says the CAG.

The letter, dated March 12, 2011, is addressed to the Finance and Economic Affairs permanent secretary and Paymaster General and dwells on Tanesco's audited financial statements for the year ended December 31, 2009.
The ministry had written to the CAG on February 9 suggesting that cash-strapped Tanesco bears responsibility for the compensation.

Richmond had transferred its rights and obligations to Dowans SA before the contract was terminated.
But in his response, the CAG says the government cannot in any way escape full liability after overruling the procurement functions of Tanesco's board of directors and management with regard to the Richmond deal.

"I have been able to evaluate the sequence of events pertaining to the procurement process of the 100MW rental emergency generating plant in Dar es Salaam, which was awarded to Richmond Development Company USA, and the transfer of its rights and obligations to Dowans SA.

"I have noted with concern the ministry of Energy and Minerals' override on the procurement functions of the board of directors and management of Tanesco and on non-compliance with the Public Procurement Act, 2004 and its related regulations of 2005," says Mr Utouh's letter, whose copy was seen by The Citizen.

The CAG's verdict is likely to end a four-month dispute between the government and Tanesco on who should pay the compensation.Finance minister Mustafa Mkulo said in January that the Treasury did not have funds to pay the compensation, adding that it was the burden of the Energy and Minerals ministry.

Contacted on Wednesday, Mr Utouh declined to comment further on the issue, saying it was still pending in court. "The issue is still pending in court and at this point in time neither you nor I can comfortably say the what the outcome will be. Let's be patient as we wait for the court's decision," Mr Utouh told The Citizen by telephone.

Energy and Minerals minister William Ngeleja also declined to comment on the matter.But Mr Utouh says in his letter that it was evident the Energy and Minerals ministry handled the procurement process of the emergency power supply contract, and the transfer of Richmond rights and obligations to Dowans.

"It is evident that if the government, through the ministry of Energy and Minerals, had not directly been involved, the Richmond and Dowans saga would not have occurred," says the CAG. He further observes that Tanesco's current financial position is not sound, with the situation worsening every year.
 
Hiki hapa nini?


Soma hiyo halafu useme kama sio kupindisha maneno ni nini? Serikali ipi au TANESCO ipi ilikuwa na mkataba na Richmond ulioamuliwa mahakama ya kibiashara? nimekuwekea juu hapo mpaka kesi namba na nani mdai na nani mdaiwa bado tu unakataa? Ni DOWANS walioshtaki si Richmond wacha kuendelea kubisha ujinga. Nakuwekea tena hapa chini:

Soma huu hapa:
ICC Case No. 15947/VR: Dowans (Claimant) and TANESCO (Respondent)

Fisadi wewe unataka kuamini kwamba Richmond ni kampuni tofauti na Dowans lakini ukweli ni kwamba Richmond ndiyo pia Dowans. Kutokana na kuwa na Serikali DHAIFU inayoongozwa na mafisadi, Mafisadi Rostam na Al Alawi hawakupata shida kuizuga Serikali eti mkataba wa Richmond umechukuliwa na kampuni mpya iitwayo Dowans. Richmond na Dowans ni Baba mmoja mama mmoja.

https://www.jamiiforums.com/habari-...-cag%92s-ruling-on-who-should-pay-dowans.html

However, it is not clear who is supposed to shoulder the burden, with Tanesco saying the government had the final say on the contract. Mr Utouh says in a letter to the Finance and Economic Affairs ministry that he had studied developments leading to the agreement, and concluded that the government should take responsibility for the compensation after interfering in Tanesco’s contract mandate and obligations.

The CAG has also suggested that the government reviews Tanesco’s debt portfolio and ease the burden on the public utility arising from contracts in which the State is involved.“This will enable Tanesco to be evaluated on fair grounds and be held accountable for its own decisions,” says the CAG.
 
Back
Top Bottom