Amanikwenu
Senior Member
- Dec 1, 2009
- 187
- 0
Kazi yenu miliyoifanya kama UDASA siku ya Jumamosi ya tarehe 15/01/2011 ni nzuri na inastahili pongezi za kipekee.
Kama mlivyoahidi inatia moyo kuona kuwa mtakuwa na mijadala mingi ya aina hiyo na kwa nchi nzima kama ikiwezekana. Binafsi naamini kuwa mmeishaanza kutafakari kuhusu mpango wenu wa utekelezaji ili kuhakikisha kuwa kila Mtanzania anashiriki katika kuhakikisha kuwa nchi yetu inapata katiba mpya na iliyo bora.
Pamoja na kile mtakachopanga katika kufanikisha lengo lenu kuu, naomba nami nipendekeze yafuatayo:-
1. Baada ya kuwa na mpango kamili wa utekelezaji itisheni mkutano maalumu na vyombo vya habari ili kila chombo cha habari kitoe nafasi maalumu katika kufikisha moja kwa moja kile kitakachokuwa kikijadiliwa katika kila mdahalo katika siku husika--Ombi hili ni hasa kwa vituo vya Redio na Televisheni. Pia ziombeni Televisheni na Redio zetu zitenge muda maalumu wa angalau saa moja kila siku kwa ajili ya kuuelimisha umma wa Watanzania kuhusu katiba na njia ipi bora inafaa kutumika ili kupata katiba nzuri na iliyo bora. Kwa upande wa magazeti yaige mfano wa RaiaMwema ambalo limeanza kuichapisha katiba kuanzia toleo lake la tarehe 12/01/2011. Ni matumaini ya Watanzania wengi kuwa itawezekana kuwa na mdahalo angalau mmoja kila wiki ifikapo mwezi Machi mwaka huu.
2. Kwa kuwa shughuli nzima ya kuzunguka nchi nzima na kuendesha Midahalo mbalimbali kuhusu katiba itahitaji fedha tunaomba muanzishe utaratibu maalumu ili Watanzania tuweze kuuchangia mpango huu kupitia njia mbalimbali kama vile simu zetu za mkononi. Mkumbuke kuwa kwa mwezi mmoja tu matumizi yetu kupitia simu za mkononi ni zaidi ya shilingi bilioni 185 (www.tcra.go.tz).
3. Tengenezeni Timu Maalumu ya Wataalamu ambayo itazunguka nchi nzima kuendesha midahalo na kutumia ipasavyo vyombo vya habari katika kuelimisha Watanzania haja ya kuwa na Katiba mpya na ni mambo gani ya msingi yanapasa kuzingatiwa katika uandikaji wa katiba mpya.
Naomba kuwasilisha.
Kama mlivyoahidi inatia moyo kuona kuwa mtakuwa na mijadala mingi ya aina hiyo na kwa nchi nzima kama ikiwezekana. Binafsi naamini kuwa mmeishaanza kutafakari kuhusu mpango wenu wa utekelezaji ili kuhakikisha kuwa kila Mtanzania anashiriki katika kuhakikisha kuwa nchi yetu inapata katiba mpya na iliyo bora.
Pamoja na kile mtakachopanga katika kufanikisha lengo lenu kuu, naomba nami nipendekeze yafuatayo:-
1. Baada ya kuwa na mpango kamili wa utekelezaji itisheni mkutano maalumu na vyombo vya habari ili kila chombo cha habari kitoe nafasi maalumu katika kufikisha moja kwa moja kile kitakachokuwa kikijadiliwa katika kila mdahalo katika siku husika--Ombi hili ni hasa kwa vituo vya Redio na Televisheni. Pia ziombeni Televisheni na Redio zetu zitenge muda maalumu wa angalau saa moja kila siku kwa ajili ya kuuelimisha umma wa Watanzania kuhusu katiba na njia ipi bora inafaa kutumika ili kupata katiba nzuri na iliyo bora. Kwa upande wa magazeti yaige mfano wa RaiaMwema ambalo limeanza kuichapisha katiba kuanzia toleo lake la tarehe 12/01/2011. Ni matumaini ya Watanzania wengi kuwa itawezekana kuwa na mdahalo angalau mmoja kila wiki ifikapo mwezi Machi mwaka huu.
2. Kwa kuwa shughuli nzima ya kuzunguka nchi nzima na kuendesha Midahalo mbalimbali kuhusu katiba itahitaji fedha tunaomba muanzishe utaratibu maalumu ili Watanzania tuweze kuuchangia mpango huu kupitia njia mbalimbali kama vile simu zetu za mkononi. Mkumbuke kuwa kwa mwezi mmoja tu matumizi yetu kupitia simu za mkononi ni zaidi ya shilingi bilioni 185 (www.tcra.go.tz).
3. Tengenezeni Timu Maalumu ya Wataalamu ambayo itazunguka nchi nzima kuendesha midahalo na kutumia ipasavyo vyombo vya habari katika kuelimisha Watanzania haja ya kuwa na Katiba mpya na ni mambo gani ya msingi yanapasa kuzingatiwa katika uandikaji wa katiba mpya.
Naomba kuwasilisha.