Kitendo chake kilituhuzunisha wengi

Sonara

JF-Expert Member
Oct 2, 2008
726
68
Ashikiliwa polisi kudaiwa kumbaka mamake 2006-10-31 09:47:47Na Mariam samiji
Dodoma Polisi mkoani hapa inamshikilia kijana, Nguja?Mpali (23) mkazi wa kijiji cha Mbabala, kilichopo nje kidogo ya manispaa ya Dodoma kwa tuhuma ya kumbaka mama yake mzazi mwenye umri wa miaka (45). Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma Bw. Omari Mganga alisema kuwa kijana huyo alimbaka mama yake ambaye alikuwa na wiki mbili tangu ajifungue na kusababishia maumivu makali. Bw. Mganga alisema kuwa tukio hilo lilitokea Oktoba 28, mwaka huu majira ya saa 11 jioni?wakiwa nyumbani kwao Mbabala. Alisema kijana huyo alirudi nyumbani akitokea kwenye mizunguko yake ambapo alimuomba mama yake ampe ugaliambapo alimjibu ugali hakuna na ndipo alipombaka. Kamanda Mganga alisema kuwa wakati mama huyo akifanyiwa kitendo hicho, alipiga kelele ambapo majirani walifika na kumkta mama hajiwezi hivyo kumkimbiza hospitali ya mkoa wa Dodoma ambako alilazwa. Kijana huyo alikamatwa na anatarajiwa kufikishwa mahakamani. Kwa mujibu wa mama mzazi huyo, kijana wake ana tabia ya ulevi na uvutaji wa bangi ambazo ndizo zimemsababishia kufanya kitendo hicho.
 
ndo matokeo ya kutowapeleka watoto shule, na kusuburi kuwa kila mtoto anabahati yake duniani. hata hivyo pole kwa huyo mama, na amsamehe mwanae kwani alikuwa katika msukumo wa bangi. maDR, kama watakuwa na akili hawatamtia hatiani kijana huyu.

wazani wafundisheni mema watoto zenu, na mungu atuepushie uvunjifu huu wa tabia.
 
Back
Top Bottom