Kitendo cha Mbatia kumfungulia Kesi Halima Mdee je anajua kuwa anafanya kazi ya CCM?

Joblube

JF-Expert Member
Mar 4, 2011
369
151
Hakuna kitendo kilichonishangaza kama cha Jemsi Mbatia kufungulia kesi H. Mdee hasa kwa kuwa wote wanajiita wapinzani na lengo lao ni kuitoa CCM madarakani. Kitendo kile kinanifanya kutambua uwezo mdogo wa baadhi ya wanaojiita wanasiasa, kwa sababu mimi natoka jimbo hilo na kama kweli Mbatia angelikua na uwezo wa kiuongozi angepaswa kuwa na ulewa kidogo tuu usihitaji shahada yeyote kuwa hata leo hii uchaguzi wa jimbo la kawe ukirudiwa hana uwezo wa kumshinda H. Mdee kwa sasa jinsi anavyokubalika nasisitiza kwa sasa. Hili nimeliona wakati wa kampenini na hata sasa kule site wanasema Mbatia hawezi kushinda anafanya kazi aliyotumwa na CCM.

Pili angepaswa kujua kuwa kitendo cha kumfungulia kesi mbunge mwenzake wa upinzani kinafanya aonekane yeye anafanya kazi kwa kivuli cha CCM hivyo kumpunguzia heshima kwa wanaounga mkono upinzani. Hawa ndio wanasiasa wa tanzainia wenye kudai wana sera mbadala wa hizi za CCM lakini jambo dogo kama hili hawawezi kusoma alama za nyakati.

Tujadili
 
Mimi nadhani huu ni uelewa mdogo wa kwako. Mbatia anayo haki ya kushitaki pale taratibu, kanuni na sheria za uchaguzi zinapokiukwa. Kitendo cha yeye kwenda mahakamani ni haki yake na tambua kuwa hizi ni tuhumu na mahakama haijamtia Mdee hatiani basi tusubiri tuone haki hii itakwenda kwa nani, kwa sababu hili ndio jukumu la msingi la mahakama. Tusiwe tunaenda mbali wakati mwingine kwa sababu kujadili mambo yaliyopo mahakamani ni kuingilia uhuru wa mahakama. Tuziache mahakama zifanye kazi zake lakini kumbuka kuwa pia Mbatia anayo haki ya kushtaki pale anapoona inamfaa kufanya hivyo, na hili hajatumwa na ccm kama unavyodai.
 
Kwani hamjui Mbatia anawakilisha mawazo ya ccm singilizeni hata maongeze yake kwenye makangamano .
 
Mimi nadhani huu ni uelewa mdogo wa kwako. Mbatia anayo haki ya kushitaki pale taratibu, kanuni na sheria za uchaguzi zinapokiukwa. Kitendo cha yeye kwenda mahakamani ni haki yake na tambua kuwa hizi ni tuhumu na mahakama haijamtia Mdee hatiani basi tusubiri tuone haki hii itakwenda kwa nani, kwa sababu hili ndio jukumu la msingi la mahakama. Tusiwe tunaenda mbali wakati mwingine kwa sababu kujadili mambo yaliyopo mahakamani ni kuingilia uhuru wa mahakama. Tuziache mahakama zifanye kazi zake lakini kumbuka kuwa pia Mbatia anayo haki ya kushtaki pale anapoona inamfaa kufanya hivyo, na hili hajatumwa na ccm kama unavyodai.

Nakuunga mkono. Wapinzani wanaipinga CCM na wapinzani wanapingana pia wao kwa wao. Haiwezekani kuwe na ukiukwaji wa taratibu (tuhuma) halafu mtu aliyetendewa anyamaze kimya ati kwa kuwa katendewa na mpinzani mwenzake, alaa!! Wapinzani wanapingana kwa kuwa hakuna makubaliano ya kuachiana majimbo na sera zao pia zinatofautiana ndio maana CHADEMA hawakumuachia Kafulila atambe peke yake kule kigoma japokuwa alikuwa akikubalika. Tuache sheria zichukue mkondo wake na wala sio kujificha katika kichaka cha Upinzani huku wapinzani wengine wakiwa hawatendewi haki.
 
Hamkutuhumu alipogombea leo mnamtuhumu kwa kwenda mahakamani! Aliwekeza hela nyingi bwana. Lazima arushe mateke angalau.
 
Kama Mbatia aligundua kuwa Halima Mdee alishinda kwa kukiuka sheria ni lazima amshitaki, na hiyo ndio demokrasia yenyewe. Angalia sana! Unaweza kudai kuwa unatetea Demokrasia kumbe ndio unaizika, kwa kudhani kwamba kwa kuwa wewe ni mpinzani basi watu wakuunge mkono hata unapovunja sheria.
 
Kama Mbatia aligundua kuwa Halima Mdee alishinda kwa kukiuka sheria ni lazima amshitaki, na hiyo ndio demokrasia yenyewe. Angalia sana! Unaweza kudai kuwa unatetea Demokrasia kumbe ndio unaizika, kwa kudhani kwamba kwa kuwa wewe ni mpinzani basi watu wakuunge mkono hata unapovunja sheria.

Mkuu uko sawa. Naanza kuhisi kwamba humu ndani ya forum tunakuwa watovu wa demokrasia. Ni vema tukajipambanua kwa kutetea demokrasia na wala si ushabiki wa vyama na watu. Vyama havitatufikisha kokote. Mimi kwangu vyama katika nchi hii kuanzia CCM, CHADEMA, CUF, UMD, Siju MAKINI, utitiri mwingine, n.k ni magenge tu ya wasaka tonge!!
 
lazima kujua kuwa ana haki kisheria kudai haki yake anayohisi kuwa ameporwa.

Wapeni nafasi na mahakama itaamua mbivu na mbichi
 
Wacha afungue kesi ashindwe tena, afungue tena ashindwe tena hadi 2015... Mbatia ana haki!!! Lakini si dhani kama kila haki ni kukimbilia mahakama
 
taratibu zinazolalamikiwa zisije zikawa ni zile za jinsi wapiga kura walivyolinda kura zao zisi"PORWE" sijui Msarendo na Kimbunga mtasemaje
 
Hakuna kitendo kilichonishangaza kama cha Jemsi Mbatia kufungulia kesi H. Mdee hasa kwa kuwa wote wanajiita wapinzani na lengo lao ni kuitoa CCM madarakani. Kitendo kile kinanifanya kutambua uwezo mdogo wa baadhi ya wanaojiita wanasiasa, kwa sababu mimi natoka jimbo hilo na kama kweli Mbatia angelikua na uwezo wa kiuongozi angepaswa kuwa na ulewa kidogo tuu usihitaji shahada yeyote kuwa hata leo hii uchaguzi wa jimbo la kawe ukirudiwa hana uwezo wa kumshinda H. Mdee kwa sasa jinsi anavyokubalika nasisitiza kwa sasa. Hili nimeliona wakati wa kampenini na hata sasa kule site wanasema Mbatia hawezi kushinda anafanya kazi aliyotumwa na CCM.

Pili angepaswa kujua kuwa kitendo cha kumfungulia kesi mbunge mwenzake wa upinzani kinafanya aonekane yeye anafanya kazi kwa kivuli cha CCM hivyo kumpunguzia heshima kwa wanaounga mkono upinzani. Hawa ndio wanasiasa wa tanzainia wenye kudai wana sera mbadala wa hizi za CCM lakini jambo dogo kama hili hawawezi kusoma alama za nyakati.

Tujadili

Mbatia si wa kwanza kufanya kazi aliyotumwa na CCM. Lamwai naye pia....
 
Tuache unafiki, kama Mbatia na ushahidi wa kutosha na anaamini kuwa Mdee hakushinda kihalali ni haki yake kwenda mahakamani, kuwa mpinzani na kuwa na lengo la kuiondoa CCm madarakini haimaanishi kuwa zifanyike rough kufikia malengo we need fair play and that applies to both CCM and oppositions! go Mbatia it is your right!
 
Back
Top Bottom