Kitendawili msingi cha Tanzania

Expedito Mduda

JF-Expert Member
Sep 22, 2009
522
240
Tanzania ni tajiri katika rasilimali na bado watanzania wengi ni maskini. Kwa nini? Hiki
ni kitendawili kikubwa ambacho tunapaswa kukijibu.
Umaskini katika Tanzania sio ugonjwa ambao tiba yake haipatikani kwa urahisi. Kwa
kweli umaskini tulionao huku tukiwa tumejaliwa rasilimali nyingi na utajiri mwingi
unaotokana na mchakato wa mambo mengi yanayokuwepo kwa wakati mmoja.
Hali tuliyo nayo imeletwa na mchanganyiko wa mambo mengi. Tunapaswa kuchunguza
na kuchanganua mambo hayo na hasa tukijiangalia sisi wenyewe, mienendo yetu, na
kisha tuelewe ukweli wetu, mazuri na kasoro zetu. Kuondokana na umaskini, ni lazima
kufuata mchakato wa kubadilika. Mwenye wajibu katika kuongoza mchakato huo ni sisi
wenyewe. Ni lazima tuwe viongozi wa mchakato huo. Haifai kuwaachia watu wa nje,
wafadhili, ama fedha kutoka kwingine popote. Hatuwezi kufaulu kwa kujifunza na
kupokea njia zilizosaidia nchi nyingine. Kikwazo cha maendeleo yetu ni utegemezi na
kukosa uwajibikaji miongoni mwa mawakala katika jitihada za kuleta maendeleo.
Kukosa uwajibikaji ndio sababu kuu na jambo kuu linalosababisha umaskini wetu. Ni
lazima, kwa hiyo, tujiwajibishe wenyewe katika kujinasua na mtego huu. Lazima
tujisumbue na tuhangaikie kutafuta ufumbuzi wa matatizo yetu tukitumia ubunifu wetu
wenyewe na rasilimali zetu wenyewe.
Mafisadi na kutokuwa na uaminifu ni vikwazo vikubwa sana katika kujiletea maendeleo! Watanzania tusimame kidete kuhakikisha mambo hayaendelei kuwa hivi yalivyo na hatua ya kwanza kubwa ni kuhakikisha tunapata katiba mpya!!!!!!!!!
 
Tanzania ni tajiri katika rasilimali na bado watanzania wengi ni maskini. Kwa nini? Hiki
ni kitendawili kikubwa ambacho tunapaswa kukijibu.
Umaskini katika Tanzania sio ugonjwa ambao tiba yake haipatikani kwa urahisi. Kwa
kweli umaskini tulionao huku tukiwa tumejaliwa rasilimali nyingi na utajiri mwingi
unaotokana na mchakato wa mambo mengi yanayokuwepo kwa wakati mmoja.
Hali tuliyo nayo imeletwa na mchanganyiko wa mambo mengi. Tunapaswa kuchunguza
na kuchanganua mambo hayo na hasa tukijiangalia sisi wenyewe, mienendo yetu, na
kisha tuelewe ukweli wetu, mazuri na kasoro zetu. Kuondokana na umaskini, ni lazima
kufuata mchakato wa kubadilika. Mwenye wajibu katika kuongoza mchakato huo ni sisi
wenyewe. Ni lazima tuwe viongozi wa mchakato huo. Haifai kuwaachia watu wa nje,
wafadhili, ama fedha kutoka kwingine popote. Hatuwezi kufaulu kwa kujifunza na
kupokea njia zilizosaidia nchi nyingine. Kikwazo cha maendeleo yetu ni utegemezi na
kukosa uwajibikaji miongoni mwa mawakala katika jitihada za kuleta maendeleo.
Kukosa uwajibikaji ndio sababu kuu na jambo kuu linalosababisha umaskini wetu. Ni
lazima, kwa hiyo, tujiwajibishe wenyewe katika kujinasua na mtego huu. Lazima
tujisumbue na tuhangaikie kutafuta ufumbuzi wa matatizo yetu tukitumia ubunifu wetu
wenyewe na rasilimali zetu wenyewe.
Mafisadi na kutokuwa na uaminifu ni vikwazo vikubwa sana katika kujiletea maendeleo! Watanzania tusimame kidete kuhakikisha mambo hayaendelei kuwa hivi yalivyo na hatua ya kwanza kubwa ni kuhakikisha tunapata katiba mpya!!!!!!!!!
Maneno meeengi umeandika ambayo ni pumba!
Ungeandika hapo penye red tu ungeeleweka!
 
Back
Top Bottom