Kitakacho andikwa tanzania baada ya siku 9 kumalizika

Henry Kilewo

JF-Expert Member
Feb 9, 2010
899
1,084
kwanza litakuwa nijambo la faraja sana kuwaweka watanzania kwenye maisha mapya ya kujenga uchumi upya, kuandaa maisha mapya na kuweka misingi bora kwa kizazi kipya, kwa haraka haraka ukifikiria neno siku 9 unaweza kulidharau na kuliponda kutokana na fikra zako zinavyo fikri.

ila neno hili ukilidadavua unapata maana kubwa sana na yakukupa matumaini ya kufanya mabadiliko makubwa sana..... maana CDM hawakukurupuka walikaa chini na kupanga jinsi ya kuingia mtaa kwa mtaa kuhakikisha ya kuwa ndani ya siku 9 kila mtanzania atakuwa amefahamu umuhimu wake katika kulitetea taifa lake.

dhahiri kwamba maovu yaliyofanywa na serikali ya CCM kila mmoja alikuwa amechoshwa nayo, ila hapa kulikuwa kuna kama kamchezo kila mmoja anamsubiri mwenzake aanze ila apate kushiriki, muamko ule wa mwanza ni kiashiria tosha chakuonyesha ni jinsi gani watanzania tunasubiri mabadiliko haya kwa hamu kubwa sana,

najua wapo wanao amini juu ya ujio wa mabadiliko hayo na wapo wasiyo amini ujio wa mabadiliko hayo kwa kukosa moyo wa uthubutu, naomba ni mnukuu RAIS WANGU (SLAA) slaa huwa simumunyi maneno: kwa mtu mwenye fikra na hakima haya maneno ni machache sana ila nimaneno ya ukombozi kama kweli wewe unadhamira ya kweli kwanini umumunye maneno?

ila kunahaja ya kulazimisha mabadiliko katiks ukanda wa pwani, umekuwa ndiyo ukanda namba moja kushindwa kupokea upepo huu wa mabadiliko kwa wakati, ukanda huu ndiyo ukanda unaoongoza kwa makazi duni, kama vile watu wake kuendelea kuishi kwenye nyumba za tembe, kukosa huduma za afya, kati rais wa NEC kipindi alipokuwa waziri wa mambo ya ndani alikuwa mbunge wa eneo hili na sasa kabuka kuwa rais wa NEC ila hali bado inaendelea kuwa tete,

siku tisa kwangu ni siku ya furaha na majonzi kwakuwa najua wapo watakao ona ni kupoteza muda na watakao amini ni wakati muafaka sasa.... ni bora ukaishi miaka 30 ukafa sauti yako ikabaki milele hapa duniani, kuliko ukaishi miaka miamoja ukafa ukazikwa ukapotea kama mnyama..... maneno haya hunipa ujasiri wa kutobadilisha dhamira ya mabadiliko na kuwa tayari kupingwa risasa hadharani kwa kulitetea taifa langu,

siku tisa zitaweka historia mpya na uongozi upya wenye dira mpya katika taifa hili kwasasa...... kizazi kijacho kinahitaji mabadiliko sasa ilikiweza kulipeleka taifa mbali zaidi ya hapo lilipo, kwani naamini baada ya 6 zijazo TANZANIA ya kweli tutaiona, eeeh mungu mbariki rais wetu wa moyo dr slaa, aendelee kuwapa nguvu ya ukombozi wa tanzania wenzake
 
Back
Top Bottom