Kiranja Mkuu
JF-Expert Member
- Feb 18, 2010
- 4,063
- 4,058
Nilikuwa Mwanza na nilitembelea wilaya za Magu na Sengerema. Huko nilikutana na ngoma za kina Ng'wana Ituli,wanacheza MBINA. Hii ni ngoma inayochezwa kipindi cha kiangazi baada ya mavuno.
Wanajivunia uchawi na nguvu za miujiza walizonazo,wanawataja mashujaa wao kuwa ni kina Ng'wana Malundi, Iwambangulu, na Mtemi kapela.
Wanajivunia maajabu aliyoyafanya Ng'wana Malundi, ikiwa ni pamoja na kutembea juu ya bahari kule Zanzibar, kukausha misitu kwa kidole.
Kwa kweli ni historia nzuri sana na ya kujivunia na kuvutia pia, lakini kwa bahati mbaya hamna sehemu zilipo andikwa, ni masimulizi ya midomoni kwa watu.
Kuna haja sasa wataalam wetu wa historia, waende huko Usukumani wakasiklie na kuandika.
Inasikitisha kuona taifa letu halithamini historia yake yenyewe.
========================
Wanajivunia uchawi na nguvu za miujiza walizonazo,wanawataja mashujaa wao kuwa ni kina Ng'wana Malundi, Iwambangulu, na Mtemi kapela.
Wanajivunia maajabu aliyoyafanya Ng'wana Malundi, ikiwa ni pamoja na kutembea juu ya bahari kule Zanzibar, kukausha misitu kwa kidole.
Kwa kweli ni historia nzuri sana na ya kujivunia na kuvutia pia, lakini kwa bahati mbaya hamna sehemu zilipo andikwa, ni masimulizi ya midomoni kwa watu.
Kuna haja sasa wataalam wetu wa historia, waende huko Usukumani wakasiklie na kuandika.
Inasikitisha kuona taifa letu halithamini historia yake yenyewe.
========================
Hakuna hifadhi mahali alipokanyaga Ng'wanamalundi.
Wednesday, 13 July 2011 20:34
Na Charles Kayoka.
Kwa Watanzania wa umri wangu waliopata kusoma historian au kusikia hadithi za makabila, hasa ya Wasukuma na Wanyamwezi, hawakukosa kusikia habari ya Ng'wanamalundi. Aliyezaliwa katika ukoo wa kiuganga na uchifu aliyehesabiwa kuwa ni mmoja ya watu wenye miujiza mingi.
Ng'wanamalundi anaelezewa kuwa na uwezo wa kufika mahali mbali kutoka nyumbani kwa muda mfupi, sijui alitumia nguvu gani? Aliweza kutibu watu kwa
uganga wake kwani alifahamika sana kwa hilo; na alikuwa anaweza kuvuka maji marefu kwa kuweka dawa na maji yakajitenga na yeye akapita.
Nilipokuwa ziarani wilayani Kahama hivi karibuni,nikifuatilia mahali alipofia Mtemi Mirambo wa Unyamwezini (nitaelezea habari zake katika moja ya makala zijazo), nikaambiwa "huko nilikotoka, kijiji cha Nyandekwa, kuna jiwe ambako Ng'wanamalundi alikuwa amelikanya na alama ya unyayo wake hadi leo uko.
Siku ya pili nikafunga safari hadi kijijini Nyandekwa, kiasi cha kilomita kumi kutoka makao makuu ya wilaya ya Kahama katika njia iendayo Urambo kupitia Uyogu.
Hapa nilipofika na wenzangu tukabahatika kukutana na kaka wa umri wa makamo aliyejitolea kutupeleka kwenye "jiwe" hilo.
Ni kiasi cha kilomita moja toka barabara ya Uyogu na hakuna barabara ya gari zaidi ya njia za wafugaji wa ng'ombe. Tukaifuata njia hiyo tukiwa ndani ya Landcruiser,maana sidhani kama unaweza ukaenda na gari dogo zaidi ya hilo likarudi salama, hasa kama mvua imenyesha.
Ninaeleza hivyo kwa sababu nilidhani hiki ni moja ya kivutio kikubwa sana cha kiutamaduni na historia na kingejengewa barabara ili watalii wa ndani na nje wangeweza kufika kutembelea.
Hapo ni mahali penye mwamba mkubwa wa jiwe. Tukaona watoto na akina mama wakianika nafaka kwenye jiwe hilo.
Tulipofika na kuwauliza kama wanajua habari za Ng'wamamalundi na uhusiano wake na jiwe lile walisema hawajui chochote, na mwingine alisema yeye ni
mgeni eneo lile.
Tulipanda mpaka juu na kuona alama tatu za nyayo za binadamu. Alama ya tatu imefutikafutika lakini mbili zilizobaki zilikuwa bado zinaonyesha vizuri. Moja
ilikuwa ndogo, kiongozi wetu alisema kuwa ile ndogo ilikuwa ya mke wa Ng'wanamalundi.
Na ingine iliyokuwa kubwa ilikuwa ndiyo ya Ng'wanamalundi mwenyewe. Na hadithi zinasema Ng'wanamalundi alikuwa na miguu mikubwa, huenda ndio sababu ya kuitwa Malundi- miundi- Miguu. Yaani mtu mwenye "mamiguu". Alama ya unyayo huu ilikuwa kubwa, na ilikuwa na alama ya kukatwa katikati.
Tuliambiwa kuwa ni mkewe ndiye aliyeikata ile lama, hatukuelezwa ni kwa kusudi gani. Lakini fikiria binadamu kuwa na uwezo wa kukanyaga kwenye jiwe na kuweka alama iliyodumu kwa zaidi ya miaka sabini.
Pembeni yake palikuwa na jiwe la mviringo ambalo huwezi kulinyanyua, labda uwe na nguvu za Ng'wanamalundi mwenyewe. Jiwe hili lilikuwa na mashimo yaliyokuwa katika mistari iliyonyooka na nilipochunguza nilihisi kuwa ni mashimo ya kuchezea bao,ule mchezo wa kienyeji unaochezwa na watu wawili hadi wanne kwa kutumiamawe kwenye mashimo.
Niliona kuwa kulikuwa na mashimo ya kutosheleza watu wanne kucheza- yaani mabao mawili.
Tulielezwa kuwa hapo ndipo Ng'wanamalundi alipopenda kucheza bao na rafiki zake. Alitengeneza lile bao kwa kufinya mkono wake wenye nguvu za ajabu
kwenye lile jiwe na mashimo kutokezea.
(Hii sio hadithi ya kwanza kusikia, hata huko milima ya Uluguru kuna mahali ambapo Chifu Kingalu na wenzake walikuwa wakishindana kuonyeshana nguvu za uchawi KWA kutengeneza mashimo ya bao kwenye mawe kwa kutumia visigino vya miguu.
Moja ya bao hilo liko hadi leo pembeni ya mto huko milimani- Morogoro- picha ninazo). Na wengi kule Kahama wanasema kuwa mashimo kama hayo ya
Ng'wanamalundi aliyatengeneza sehemu nyingine nyingi, maeneo ya Shinyanga na Mwanza.
Mahali hapo pamesahaulika, huenda kwa waganga wachache wanapopakumbuka hapo kwa ajili ya matambiko yao. Lakini hakuna ulinzi, hakuna kumbukumbu, na miguu hii ya Ng'wanamalundi na mkewe inafutika kutokana na upepo, mchanga, jiwe kutumika na binadamu na mvua.
Huu ni utalii wa kihistoria lakini hautumiwi. Wiki ijayo tutazungumzia jiwe la "nyasaolo"katika kijiji cha Busolo, ambako ukifanya tambiko na kuliomba likatikisika ujue maombi yako yamekubalika.
utaliiupdate@gmail.com , 0766959349
siku moja bana mwanamalundi alikua kwenye mkutano watu wengi wamekusanyika kusikiliza kitu wenyewe wanaita mbina.
Basi watu wakamfata mwanamalundi na kumtaarifu kwamba kuni za kupikia chakula cha watu wa mkutano ule zimeisha.
Aliposikia hivyo aligeuka kuelekea upande ambapo ulikuwepo msitu akanyoosha mkono kuelekea huo msitu na kusema,''Batemagi pye abenaba''.
Yaani wakateni wote hawa..akimaanisha ile miti iliyokua msituni.Ghafla miti yote aliyoinyeshea mkono ilikauka yote.
Watu waliokua upande wa huo msitu nao walikauka pia.
Mkuu kwakweli nimekumbuka mbali sana. Nakumbuka kulikuwa na vitabu vya huyu ndugu yetu Ng'wanamalundi katika shule za msingi miaka ya nyuma na nilibahatika kuvisoma. Historia inakaliwa na watawala wetu.
REJEA: Kipindi cha Kambi Popote cha Clauds TV utatamani kulia. Na wengi wetu ni mashahidi wa utajiri wa kihistoria tulionao Watanzania karibia katika kila mkoa. Kuanzia historia ya Uumbaji na hata ile ya kikoloni. Inauma Sana!
Wanajamii Forum; picha hapo chini ni mti aina ya mkurunguunaodaiwa kuwa ulikauka miaka kadhaa iliopita baada ya magician with supernatural powers kupita katika kataiitwayo Usule hukooo&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];.kama unaelekea kusini mashariki mwa Shinyanga vijijini . alifikia kwa chief nakufuata taratibu zote za kiitifaki naanga yote ilitanda askari wa kutungua roketi, mabomu ya ardhini, silaha za nyuklia na kuthibiti dhahama ya aina yeyote ilewananzengona kama kawaida ya kabila langu la &[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];.. (ntuhu tabu, mawitogwa duhu koi hagalikoya&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG] walimwangusha ngondi lakini kuni za kuchomea zilikosekana baadawanawake kuzuiwa kuzurura hovyo kwenye maeneo ya ugeni . Hivyo mgeni rasmi alitoa tamkowenyeji waondoe hofu kwani kuni zipo,alitakiwa kutoa kuni mara aliamka na kulisota kidole mti wa mkurungu uliokuwajirani. Ulikauka palepale na kuni zikapatikana.
Rushia like hapa! nitaendeleaambaye yupo karibu na library ya shytown atupe details za huyu mtualikozikwa maana naskia ukigusa kaburi lake unapata super natural power kamayeye.
Kwa sasa nipo Njombena punde nitawaletea kuhusu &[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];'nyumba nitu''from Mlevela.
Kwa wale waliopata kusoma historia au kusikia hadithi za makabila, hasa ya Wasukuma na Wanyamwezi, hawakukosa kusikia habari ya Ng’wanamalundi.
Mtu huyo aliyewahi kuutingisha utawala wa Wajerumani, alizaliwa katika ukoo wa kawaida akiwa mcheza ngoma mashuhuri, mwaka wa kuzaliwa kwake haufahamiki ila alifariki dunia mwaka 1936, akiwa tayari mtu mzima.
Watu wengi wamekuwa wakimjadili kwa maoni tofauti, wengine wakimsifu kama shujaa huku wengine wakihusisha uwezo wake na nguvu za giza.
Katika makala hii usahihi wa historia yake unaelezwa na mjukuu wake wa pili, Kishosha Sitta (80) mkazi wa Kijiji cha Mwalugulu wilayani Kahama mkoani Shinyanga, anayesimulia alivyomfahamu babu yake huyo.
Sitta anaanza kueleza kuwa jina halisi la babu yake halikuwa Ng’wanamalundi bali lilikuwa Igulu Bugomola, ambaye alizaliwa katika Kijiji cha Mwakubunga Nera wilayani Kwimba mkoani Mwanza.
Ng’wanamalundi alikuwa mtoto pekee wa kiume na wa mwisho kati ya wanne, kwa baba yake Bugomola na mama yake, Ngolo Igulu.
Sitta anasema Igulu (Ng’wanamalundi), alikuwa na tabia ya uzururaji tangu utotoni na mara nyingi haikuwa rahisi kumkuta nyumbani. Alikuwa mashuhuri kutokana na umahiri wake wa kucheza ngoma na mara nyingi alipokuwa akitembea mitaani alifuatwa na kundi kubwa la watoto.
“Hali hiyo iliwachukiza wazazi wengi wenye watoto waliokuwa wakiambatana naye, kiasi cha kumchukia hata Ng’wanamalundi mwenyewe, kutokana na watoto wengi hasa waliokuwa wakitoka familia za wafugaji kutoweka na hiki kilikuwa chanzo cha mifugo mingi kupotea baada ya kutelekezwa na watoto hao,” anasema Sitta.
Hali ya kuchukiwa kwa Ng’wanamalundi ilienea pale kijijini kiasi cha kuanza kumkebehi, hasa kutokana na umbo lake refu na miguu yake myembamba kuanzia magotini hadi kwenye makanyagio, ikiwa mirefu kuliko kawaida.
Sitta anasema hali hiyo ilisababisha kumdhihaki na kumwongezea chuki zaidi kwa wanakijiji wa eneo hilo waliodiriki kumtukana kwa lugha ya Kisukuma; “Mamirundi galyo lilihumbura bana bise” ikiwa na maana ‘mamiguu yake marefu linarubuni watoto wetu”.
Hapo ndipo ukawa mwanzo wa kufutika kwa jina la Igulu na kuwa Ng’wanamalundi, jina ambalo lilitokana na urefu wa miguu yake na kila kona walimuita hivyo.
Kadiri siku zilivyosonga mbele Ng’wanamalundi alizidi kujiimarisha katika kikundi chake cha ngoma ambayo ilivuta vijana wengi, pia baadaye ilitumika kama jeshi la kukodiwa na Watemi inapotokea vita.
Pamoja na wazazi kumchukia sana, lakini vijana walimpenda na kikundi chake kikubwa cha ngoma kilipendwa na kutumika katika sherehe mbalimbali kwenye familia za Kitemi za wakati huo.
Mwanzo wa miujiza
Sitta anasema Ng’wanamalundi na wenzake wawili walikwenda kwa bibi kizee mmoja kutafuta dawa itakayowasaidia katika shughuli zao za kucheza ngoma, ambapo bibi kizee huyo alikubali kuwasaidia.
“Tujagi lolo ngh’wiporu bana bane akiwa na maana kwamba twendeni sasa porini watoto wangu. Mwanamalundi aliongozana na wenzake pamoja na kizee huyo mpaka porini.
“Walipofika porini bibi Kizee huyo alikamata vinyonga watatu na kuwaekea vichwani, kwa kila mmoja na kuendelea kusonga mbele porini, baada ya kufika katikati ya pori nene, kizee aliwaambia wote wasimame,” anasimulia Sitta.
Anasema baada ya kusimama aliamuru kila mmoja achimbe shimo lenye urefu hadi kiunoni, na baada ya kukamilika kwa mashimo hayo aliwaambia wakusanye kuni na kuzitumbukiza.
Baada ya kazi hiyo kukamilika Sitta anasema walipekecha moto na kuziwasha zile kuni na moto uliposhika kasi aliwachukua wale vinyonga watatu na kuwawekea dawa mdomoni na kisha aliwatupia ndani ya moto huo, wakateketea wote.
“Ng’wanamalundi na wenzake wakiwa bado wanashangaa vinyonga hao kuungua, ghafla alitokea kifaru kwenye moto huo na kuanza kuwakimbiza hovyo na wote wakasambaritika na bibi kizee wao,” anasema na kuongeza;
Ngw’anamalundi alikimbia akapanda juu ya mti, kifaru alifika kwenye shina la mti na kuanza kuliparua kwa hasira na baadaye aliondoka kabla hajafika mbali alimuona yule bibi kizee akikutana na faru huyo.”
Anasema Ng’wanamalundi alishuhudia kifaru akimrarua rarua bibi kizee mpaka akafa, kisha kifaru alitoweka kusikojulikana huku akimuacha Ng’wanamalundi asijue la kufanya juu ya mti.
Sitta anasema: “Ng’wanamalundi baada ya muda alishuka juu ya mti na kwenda kwenye maiti ya yule bibi kizee, akaamua aibebe mgongoni airejeshe nyumbani, lakini kabla hajafika mbali alisikia sauti ikisema, “Igulu bajahe abiyo akiwa na maana Igulu wenzako wamekwenda wapi”.
Sauti hiyo ilimshtua Ng’wanamalundi ambaye alimshusha bibi kizee mgongoni mwake na akashangaa kumuona akiwa hai asiyekuwa na jeraha lolote, kama alivyokuwa baada ya kushambuliwa na faru.
“Igulu tujage ahante ugo waliwalinaga, akiwa na maana Igulu twende kwenye mti uliokuwa umepanda, Ng’wanamalundi aliongozana na bibi kizee huyo mpaka kwenye ule mti aliyachukua magamba ya mti yaliyokuwa yameparuliwa na faru,” anasema Sitta.
Baada ya zoezi hilo kukamilika bibi kizee huyo alimtengenezea dawa aliyokuwa akihitaji, na kisha Mwanamalundi alirejea kwao kuendelea na shughuli zake za ngoma aina ya Kahena, ambayo mpaka leo inaendelea kwa jina lingine la Wigashe.
Anakutana na Mtemi Chlya
Sitta anaongeza kuwa, Ng’wanamalundi akiwa katika harakati zake za kujiimarisha katika masuala ya dawa zake za ngoma, alienda kuchimba kwenye pori la Mwandutu huko wilayani Maswa sasa ni Wilaya ya Kishapu, ambalo lilikuwa katika miliki ya Mtemi Chalya.
Imeelezwa kuwa baada ya kufika katika pori hilo akiwa na wafuasi wake wakiendelea kuchimba dawa, ghafla alitokea Mtemi Chalya na kumuuliza; “Ubebe nani wakuwilaga kwiza ngh’wiporu lyane” akiwa na maana; “Wewe nani amekuambia kuja kwenye pori langu?”
Mwanamalundi alimjibu; “ Ubebe ulintemi wa banhu pye nu nene nding’wenekele wa maporu pyee.” Akiwa na maana “Wewe ni Mtemi wa watu wote na mimi ni mmiliki wa mapori yote”. Kauli hiyo ilimuudhi Mtemi Chalya.
Anasema, kufuatia kauli hiyo Mtemi Chalya aliita jeshi lake kwa lengo la kuja kumkamata, lakini walishangaa baada ya kufika katika eneo waliloelezwa na Mtemi wao kuwa Ng’wanamalundi anatakiwa kukamatwa na kuuawa, lakini walishindwa baada ya kukuta simba wengi sana.
Jeshi hilo na Mtemi ilibidi kukimbia kujiokoa kwani simba hao walianza kuwashambulia, wengine walitawanyika ovyo na baadhi yao wachache tu ndiyo walionusurika.
Lakini cha kushangaza walipofika walimkuta Ng’wanamalundi na wafuasi wake wakimalizia kula chakula nyumbani kwa Mtemi Chalya, ambaye hata yeye alichanganyikiwa na kushindwa kuongea lolote.
Sitta anasema, Ng’wanamalundi baada ya kumaliza kula chakula kwa Mtemi Chalya aliondoka na wafuasi wake na akapitia kwenye lile pori akachimba dawa zake na kuondoka kwenda kuendelea na maisha yake.
“Katika ngoma zake; Ng’wanamalundi alikuwa na tabia ya kuwatahadharisha mashabiki wake kuacha kwenda wakiwa wamejipaka dawa yoyote ile, anasema. Aliwaambia: “Bing’we akwiziza munho wibilaga bugota bosebose ulu kutora akotora henaha,ulo nsabo akupandika heneha.”
Kauli hiyo ilikuwa na maana nyie asije mtu amejipaka dawa yoyote hapa kama ni kuoa, ataoa hapahapa kama ni mali atapata hapahapa, hata hivyo kuna wale walipuuza kauli hiyo kwa kuja wamejipaka dawa kwa lengo la kujipima uwezo wa dawa zao. Lakini hawakufanikiwa na badala yake walikufa.
Simulizi hii inaendelea
Akiwa anaendelea na ngoma yake wananchi wa Kijiji cha Sekke waliibiwa ng’ombe wengi sana na watu kutoka Kabila la Wamasai ambao walienda kuwahifadhi katika Pori la Mwanima karibu na Kijiji cha Bubiki. Ng’wanamalundi na kikosi chake waliondoka Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza na kuelekea Sekke wilayani Kishapu mkoani Shinyanga kwa lengo la kusaidia kuzikomboa ng’ombe zilizoibwa. Hata hivyo kabla hawajafika uwanja wa vita, Ng’wanamalundi alifanya utabiri wake uliotokana na nguvu ambazo alizipata kutoka kwa Bibi Kizee wa porini. Sitta anasema aliwaambia kuwa kabla ya vita, itatokea mvua kubwa sana na ikikatika watakuja ndege hai aina ya mwewe watakaokuwa wanazungukazunguka kwenye zile ng’ombe na hapo sasa wafuasi wake wakate miti mifupi mifupi (Lubugu).
Sitta anasema utabiri huo ulitimia, kwani mvua ilinyesha kubwa sana na baada ya kukatika wale mwewe walijitokeza wengi sana wakawa wanazunguka kwenye zile ng’ombe na ndipo yale mapigano ya Wamasai na wafuasi wake yalipoanza. Aliwaeleza kuwa baada ya kuwa na fimbo ya Lubugu wale wenye upinde na mishale watakaa nyuma na kazi yao watakuwa wanazipiga zile ngao za Kimasai na zikidondoka chini ndipo wenye pinde na mishale waanze kushambulia. Mwanamalundi alipigana hiyo vita ya Wamasai mpaka akazirejesha zile ng’ombe na aliwatokomeza Wamasai mpaka kwenye mpaka wa Mto Manonga unaotenganisha Tinde Shinyanga na Nzega mkoani Tabora. Hapo ndipo ilibainika Wamasai hao walikuwa wametumwa kuiba ng’ombe Usukumani na Mtemi Tinginya wa Busongo Nzega, ambapo baada ya vita hiyo Ng’wanamalundi na kundi lake walirudi Sekke na kupewa jina la Kishosha Mang’ombe tafsiri ikiwa ni mrudisha ng’ombe. Baada ya vita hiyo Ng’wanamalundi alirudi nyumbani kwao wilayani Kwimba kuoa, lakini bahati mbaya ilimkuta, kwani kila mke aliyejifungua, mtoto alikufa.
Baba yake Bugomola akaenda Ntuzu kwa sasa Bariadi kufanyiwa tambiko kuhusu uzazi kwa mwanaye. Akiwa huko Ntuzu, Bugomola alielezwa mwanaye Ng’wanamalundi hatapata mtoto kwa wake zake alionao. Hivyo aoe msichana atakayempata upande wa Mashariki ambaye atakuwa akiitwa Nkamba na atazaa watoto watatu; wa kwanza ataitwa Sitta, wa pili Ngassa na wa tatu Marieta. Baada ya kurudi Bugomola, haikumchukua muda mwanaye Ng’wanamalundi akapata msichana akaoa na akaendelea na shughuli yake ya kuendesha kikundi cha ngoma. Ng’wanamalundi kuwekwa kizuizini Akiwa anaendelea na ngoma zake katika maeneo ya Kanda ya Ziwa, Sitta anasema siku moja yeye na kikundi chake walipokuwa wakiburudisha katika maeneo ya Bukumbi mkoani Mwanza, wafuasi wake walipumzika kwenye mti mkubwa ambapo pia kilikuwa Kituo cha Wajerumani, Ng’wanamalundi aliwaambia wafuasi wake waondoke waende kwenye ngoma, wafuasi wake waligoma wakadai wanapumzika kwenye kivuli hicho ili wavute sigara. Baada ya kuwabembeleza vya kutosha akabaini hawataki kumsikiliza ndipo alipounyooshea kidole ule mti akisema “Ngh’walemelaga hanti gunugo aliyo gumaga,” akiwa na maana “Mmekatalia kwenye mti huo huku ukiwa umekauka.” Ghafla mti huo wote ulikauka.
Kuona hivyo wafuasi wake wakaondoka wote kwenye huo mti wakaenda kuendelea na ngoma yao ambayo walicheza katika eneo la Bukumbi na Busagara karibu na Mji wa Mwanza na walipomaliza walirejea Kwimba. Akiwa Kwimba alicheza ngoma moja na Gindu Nkima, ngoma hiyo ilikuwa ngumu kwake ilichezwa sehemu za Mwanagwa. Baada ya kuwa amezidiwa Ng’wanamalundi, wapishi wake walimfuata na kumtaka awasaidie namna ya kupata kuni za kupikia. Kutokana na uharaka aliokuwa nao Ng’wanamalundi alielekeza kidole chake kwenye miti ya minyaa iliyokuwa mbele yake huku akisema “Batemagi pye abenababa mkazugile,” akiwa na maana “Yakateni yote haya mkapikie.” Baada ya kauli hiyo minyaa yote ilikauka na kuwa kuni na wafuasi wake walikata wakaenda kupikia chakula. Akiwa katika ngoma hiyo wakati huo barabara ya kutoka Shinyanga kwenda Mwanza ilikuwa inachongwa na manamba waliokuwa wakikamatwa na Wajerumani kwa ajili ya kazi hiyo, Gavana wa Kijerumani wa eneo la Mwanza alipita eneo hilo akiwa amepanda punda alikuta kazi imesimama, alipohoji kwanini kazi imesimama alielezwa wananchi wote wamekwenda kwenye ngoma ya Ng’wanamalundi. Kitendo hicho kilimchukiza sana Mjerumani huyo, ambaye aliondoka akaenda Mwanza na baada ya siku mbili walikuja askari waliomkamata Ng’wanamalundi na kumfunga mnyororo na watuhumiwa wengine walipelekwa Mwanza na kuwekwa gerezani.
Kosa hilo kwa utawala wa Ujerumani lilihesabiwa kuwa ni uhaini wa kupinga utawala wao hivyo alitakiwa kupewa adhabu ya kunyongwa. Kabla hajapelekwa Mwanza, kwa kuwa ilikuwa ni safari ya kwenda kunyogwa, alipelekwa nyumbani kwa wazazi wake kuaga. Alipofika nyumbani kwao alimpa mama yake shoka aliloliweka pembezoni mwa ukuta chumbani na maziwa, huku akitoa maelekezo. “Mayu imbasa yeneye ulu yulina ng’wigulya mumhonatwalwa ulu yika hase mumhonashoka amabele genaya ulu guganda mumhonacha, ulu gita lububhi mumhonasata.” Akiwa na maana hii shoka ikipanda juu basi nitakuwa nimepelekwa ikishuka chini nitakuwa nimerudishwa.” Sitta anasema Ng’wanamalundi aliendelea kumpa maelekezo mama yake kuwa haya maziwa yakiganda atakuwa amekufa na pindi yakipata utando atakuwa anaumwa, baada ya maelezo hayo Ng’wanamalundi alipelekwa Mwanza gerezani ambako alikutana na Mtemi Makongoro wa Mwanza. Siku iliyofuata walitolewa wote ambapo Sitta alieleza kuwa walikutana pia na mganga aliyemtabiria kuzaa watoto watatu ambaye naye alikuwa amekamatwa kwa kosa la kupiga ramli iliyosababisha mauaji ya kishirikina.
Asubuhi kila mmoja alisomewa mashtaka yake ambapo Ng’wanamalundi alisomewa mashtaka matatu, shtaka la kwanza kuukausha mti uliokuwa ukitumiwa na maofisa wa utawala wa Wajerumani kama kituo cha kupumzikia huko Bukumbi Mwanza. Shtaka la pili kuwatungia na kuwaimbia nyimbo mbaya Wajerumani na la tatu ni kukwamisha ujenzi wa Barabara ya Mwanza kwenda Shinyanga. Ng’wanamalundi alidaiwa kuchezesha ngoma eneo la Mwanangwa hali iliyosababisha wafanyakazi wa manamba waliokuwa wakilima barabara hiyo kuacha na kwenda kuangalia ngoma yake hali iliyowachukiza Wajerumani…
Inaendelea