Kitabu cha Kachero aliyetekwa Uganda kinapatikana wapi ?.

Ngongo

JF-Expert Member
Sep 20, 2008
18,921
31,161
Heshima sana wanajamvi,

Gazeti la Raia mwema limekuwa likichapisha makala ya Kachero wa jeshi la wananchi (JWTZ) aliyetekwa Uganda pamoja na wanajeshi wengine wawili ambao waliuwawa na majasusi wa Idd Amin kabla ya vita vya Kagera.

Nimekuwa nikifuatailia sana makala hizo kila Jumatano gazeti la Raia Mwema linapotolewa bahati mbaya kila nikimaliza kusoma naachwa na kiu kubwa kiasi naomba siku ziende haraka ili niweze kusoma makala zingine.

Natoa rai kwa wachapishaji wa gazeti la Raia Mwema kutuelekeza wapi tunaweza kupata nakala ya kitabu badala ya kuendelea kututesa na kutuacha na kiu isiyokuwa na sababu za msingi.

Nawasilisha.
 
Heshima sana wanajamvi,

Gazeti la Raia mwema limekuwa likichapisha makala ya Kachero wa jeshi la wananchi (JWTZ) aliyetekwa Uganda pamoja na wanajeshi wengine wawili ambao waliuwawa na majasusi wa Idd Amin kabla ya vita vya Kagera.

Nimekuwa nikifuatailia sana makala hizo kila Jumatano gazeti la Raia Mwema linapotolewa bahati mbaya kila nikimaliza kusoma naachwa na kiu kubwa kiasi naomba siku ziende haraka ili niweze kusoma makala zingine.

Natoa rai kwa wachapishaji wa gazeti la Raia Mwema kutuelekeza wapi tunaweza kupata nakala ya kitabu badala ya kuendelea kututesa na kutuacha na kiu isiyokuwa na sababu za msingi.

Nawasilisha.
mimi nimesoma leo,inasisimua sana,ni kama uko pale,haya mambo ifike wakati sasa hata watu kuandaliwa documentaries hivi,mambo ya kwetu yanasahaulika sana,ya kishujaa etc etc..
 
Yaan mkuu unataka Ray Kigosi ndo aigize kipande hiko unaxan ataeza kweli, ukimwambia ateswe kimuvi muvi unazan anajua basi
ehehe documentary si lazima awe kigosi,kwa kutumia kitabu tu,characters unawapata watu wengi wanaoendana na hali halisi,cha msingi sisi tunasahau sana kukumbuka michango ya wazee wetu kwa style ya kileo,vita ya kagera unaweza pata hata documentaries kibao,kwa matukio kadha wa kadha,mfano mzuri rwanda genocide,wana movies,ingawaje zilitengenezwa na wazungu,nyingine mnaweza kutengeneza kupitia kwa watu wenu,kwa stories tu za walioshiriki kwa namna moja ama nyingine,ubunifu tu
 
mimi nimesoma leo,inasisimua sana,ni kama uko pale,haya mambo ifike wakati sasa hata watu kuandaliwa documentaries hivi,mambo ya kwetu yanasahaulika sana,ya kishujaa etc etc..
mimi nimesoma leo,inasisimua sana,ni kama uko pale,haya mambo ifike wakati sasa hata watu kuandaliwa documentaries hivi,mambo ya kwetu yanasahaulika sana,ya kishujaa etc etc..
Mkuu hawa ndio mashujaa wa kuenziwa
 
Kesho nitatembelea maduka ya vitabu Dar es salaam nikikipata nitawapa taarifa.
Wale maaskari walipata mateso makali sana na yule luteni atakuwa ni komandoo.
Simulizi inasisimua sana.
 
Kesho nitatembelea maduka ya vitabu Dar es salaam nikikipata nitawapa taarifa.
Wale maaskari walipata mateso makali sana na yule luteni atakuwa ni komandoo.
Simulizi inasisimua sana.

Kweli kabisa mkuu wangu,naweza kusema pasipo shaka Kitabu kitafanya vizuri.Baada ya kuangaika bila majibu nimefanya mawasiliano na mkuu wa habari za kichunguzi amekiri simu za maulizo ya kitabu ni nyingi sana na kitabu kipo katika hatua za mwisho kutoka labda mwezi September.NB Nimefanya mawasiliano kupitia namba za simu zilizopo katika safu ya wakurugenzi ukurasa wa nane Gazeti la Raia Mwema.
 
mimi nimesoma leo,inasisimua sana,ni kama uko pale,haya mambo ifike wakati sasa hata watu kuandaliwa documentaries hivi,mambo ya kwetu yanasahaulika sana,ya kishujaa etc etc..
anzia makala ya kwanza kabsa u one utamu wake
 
....imefika sehemu ya ngapi hiyo stori wandugu?,mmenishawishi!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom