Kiswahili na maneno

Che Kalizozele

JF-Expert Member
Jul 20, 2008
777
49
Kuna wakati huwa nahisi labda kiswahili kina upungufu wa maneno, ingawa kuna nyakati zingine huwa nagundua ni uchovu wangu tu katika kuifahamu lugha hii adhimu ndo unanisumbua ila kiswahili kuna uwezekano kikawa kimekamilika.

Kwa sasa nina tatizo la kiswahili kutumia vitu katika kueleza aina za rangi. Hii inanipa shida kwa kuhisi inawezekana kiswahili hakina maneno ya kuelezea rangi hizi. Mfano rangi ya zambarau, rangi ya damu ya mzee, rangi ya kijivu. Kama kuna mtu anajua maneno yanayotambulisha rangi hizi, tafadhari naomba unielimishe.
 
Mkuu hiyo ni kawaida tu kwenye lugha kwani hata kiingereza kinafanya vivyohivyo, mfano chocolate color. Na siyo kwenye rangi tu, kama ambavyo maisha ya viumbe hai yanategemeana (equal system) ndivyo hivyo na lugha, angalia hapa; kwenye ujio wa teknolojia ya habari na mawasiliano wataalamu waliamua kutumia neno web site-neno web- walililinganisha na nyumba ya buibui. Kwa hiyo usione tabu Shekh wangu, ndo lugha zinavyoishi na kukua.
 
Kuna wakati uwa nahisi labda kiswahili kina upungufu wa maneno,ingawa kuna nyakati zingine uwa nagundua ni uchovu wangu tu katika kuifahamu lugha hii adhimu ndo unanisumbua ila kiswahili kuna uwezekano kikawa kimekamilika.
Kwa sasa nina tatizo la kiswahili kutumia vitu katika kueleza aina za rangi.Hii inanipa shida kwa kuhisi inawezekana kiswahili hakina maneno ya kuelezea rangi hizi.Mfano rangi ya zambarau,rangi ya damu ya mzee,rangi ya kijivu.Kama kuna mtu anajua maneno yanayotambulisha rangi hizi,tafadhari naomba unielimishe.


Hii list inaweza kukusaidia? English (Swahili):

White (Nyeupe)
Grey (Kijivujivu, Majivu)
Black (Nyeusi)
Yellow (Manjano)
Gold (Dhahabu)
Orange (Rangi ya machungwa)
Deep orange (Rangi ya balungi)
Red (Nyekundu)
Pink (Pinki)
Purple/violet (Samawi (samawati?), Zambarau)
Red violet (Zambarau mbivu)
Blue (Bluu, Buluu)
Light blue (Buluu nyepesi)
Navy blue (Bluu nzito)
Green (Kijani, Majani)
Light green (Kijani nyepesi)
Emerald green (Kijani kibichi)
Sea green/blue (Kijani/bluu bahari)
Yellow green (Jani la mgomba)
Brown (Kahawia, Hadharani)
Cream (Mtindi)
Silver (Fedha)
 
Asanteni sana wakuu,kwa kunitoa tongotongo,mana kama ningeenda na kuanza kubishana mbele za watu ndo nilikuwa naumbuka mtu mzima.Mbarikiwe sana
 
Asanteni sana wakuu,kwa kunitoa tongotongo,mana kama ningeenda na kuanza kubishana mbele za watu ndo nilikuwa naumbuka mtu mzima.Mbarikiwe sana

Mkuu, siku zote uhitaji kubishana kwa kitu ambacho huna uhakika nacho. Pia sidhani kama ubishani ni sehemu ya kujua vitu. Uliza tu jibu linapatikana kirahisi sana. Ikishindikana nenda google. Tena hapo mnaweza kujadili na si kubishana
 
Mkuu, siku zote uhitaji kubishana kwa kitu ambacho huna uhakika nacho. Pia sidhani kama ubishani ni sehemu ya kujua vitu. Uliza tu jibu linapatikana kirahisi sana. Ikishindikana nenda google. Tena hapo mnaweza kujadili na si kubishana

Nafikiri ni ushauri mzuri,nitajaribu kuufuata.Binafsi uwa nina tatizo moja,uwa sikubali kirahisi hasa kama yale unayoyasema hayana mashiko,ingawa si kila kinachoonekana kukosa mashiko ni cha uongo.Na kutokujua haimaanishi ndo ukubali kila kitu.
 
Kuna wakati uwa nahisi labda kiswahili kina upungufu wa maneno,ingawa kuna nyakati zingine uwa nagundua ni uchovu wangu tu katika kuifahamu lugha hii adhimu ndo unanisumbua ila kiswahili kuna uwezekano kikawa kimekamilika.
Kwa sasa nina tatizo la kiswahili kutumia vitu katika kueleza aina za rangi.Hii inanipa shida kwa kuhisi inawezekana kiswahili hakina maneno ya kuelezea rangi hizi.Mfano rangi ya zambarau,rangi ya damu ya mzee,rangi ya kijivu.Kama kuna mtu anajua maneno yanayotambulisha rangi hizi,tafadhari naomba unielimishe.

Tafadhali rekebisha hayo maneno niliyoyatia rangi ya hudhurungi, yamenitatiza kidogo katika kuyasoma.
uwa linamaana ya kuoa uhai, huwa linamaana ya jambo litokealo mara kwa mara.
ndo ni chombo maalum cha kuchote/kubebea/kuhifadhia Maji. ndio inamaana ya kukubali/kuitikia jambo sahihi.
 
Mkuu, siku zote uhitaji kubishana kwa kitu ambacho huna uhakika nacho. Pia sidhani kama ubishani ni sehemu ya kujua vitu. Uliza tu jibu linapatikana kirahisi sana. Ikishindikana nenda google. Tena hapo mnaweza kujadili na si kubishana

Mwanjelwa tujitahidini kukienzi kiswahili kwa kukitumia kwa usahihi wake.
neno UHITAJI linamaana ya kuwa katika hali ya kuhitajia jambo. matakwa mahitajio.

wewe ulitakiwa kutumia neno HUHITAJI ukimaanisha hali ya kukanusha mahitajio/matakwa. huhitaji = hutakiwi/hutaki yaani huna hitajio.
kuacha herufi H katika kanushi hupoteza maana ya kanushi na pengine maana ya neno lenyewe kubadilika.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom