Ninaomba kuanzisha hii mada baada ya kusikia kwamba kuna mahali walimu wamefukuzwa kwa sababu ya kuongea kiswahili katika mazingira ya shule.
Niseme tu kwamba naunga mkono jambo hilo kwa asilimia mia. Sababu ni hizi hapa.
1. Tutambue kuwa kiswahili ni lugha inayozungumzwa sana Tanzania na ukitoka nje ya mipaka ya Tanzania kiswahili chako unaweka mfukoni! Lazima tujufunze lugha za kimataifa(English) ili tulahisishe mawasiliano na mataifa mengine.
2. Wageni wakija Tanzania wanapata taabu kweli, matangazo ya biashara yameandikwa kwa kiswahili, barabara nazo unakuta vibao vimeandikwa kwa kiswahil mfano PITA KUSHOTO. Sasa jamani wageni wetu ambao wengi wanakuja kwa maswala ya biashara inakuwa ngumu sana.Mgeni kuendesha gari tanzania ni ngumu sana. Mgeni kufanya biashara Tanzania ni ngumu sana!! Kuna jamaa wafanyabiashara wengi sana nawafahamu wanaprefer kwenda Kenya na Uganda kuchukua bidhaa kuliko Tanzania na sababu wanazozitoa ni ugumu wa Lugha.wanasema kwenda Tanzania ni gharama zaidi maana inabidi umtafute mkalimani ambaye utamlipa.
3. Kenya inatangaza mlima kilimanjaro kwa sababu ya Lugha wanayotumia inaeleweka duniani kote. Sisi tunatangaza mlima kilimanjaro kwa kiswahili wataelewa nini wageni?
4.Tunawasanii wazuri sana wa muziki, tamthiliya, vichekesho, ambao wangesaidia sana kuitangaza nchi yetu kimataifa na wao pia kufaidika, lakini wamebaki eti wasanii wa BONGO. (Kwa wale mliobahatika kuangalia stand up Zambia kilichorushwa na Africa magic channel mtakubaliana na mimi wale jamaa 3 walioshinda sasa hivi ni comedian wakimataifa wanazunguka nchi mabalimabali sababu ni lugha tu, maana kwa ukweli hawawezi kumfikia Joti, Masanja.
5.Tuna wachungaji wazuri sana(Pastors) lakini mahubiri yao ni kwa kiswahili. T.B Joshua anajulikana kila mahali kwa sababu mahubiri yake ni ya kiingeraza. Si kwamba Joshua unaupako kuliko wengine.
6. Mikataba mibovu tunayoingia na wawekezaji ni kwa sababu ya lugha tunashindwa kuilewa vizuri Wawekezaji wanapokuja ilitusionekane ni mbumbumbu wa kiingereza tunabaki kusema YES, YES YES!
7. Kwa watazamaji wenzangu wa aljazeera kuna kipindi kinaitwa 'Tea cafe (kama sijakosea)kinaongelea maswala mbalimbali yanayohusu nchi husika kipindi hicho kinapofanyika. Kipindi hicho kimefanyika,Kenya, Uganda zambia lakini Tanzania hakuna na hata katika ratiba yao Tanzania haimo simply because hakuna watu kama wanasiasa na baadhi ya watu mahalufu ambao wako tayari kujadili kwa kimombo! Sasa dunia itatuelewa vipi matatizo na mipango yetu ?
Nchi nyingi sasa hivi zinajifunza Kiingera hata china taifa kubwa wako busy kujifunza kiingereza Sisi masikini wakutupwa tunangangana na kiswahili ambacho mwisho wake ni mipakani tu! Viongozi wetu lazima pia waanalie hiyo watu waanza kufundishwa kiingereza tangu chekechea, maofisini lugha ya kiingereza isisitizwe, mikutano maofisini ifanyike kwa kiingereza. WITHOUT ENGLISH YOU ARE MARGINALIZED YOURSELF
Niseme tu kwamba naunga mkono jambo hilo kwa asilimia mia. Sababu ni hizi hapa.
1. Tutambue kuwa kiswahili ni lugha inayozungumzwa sana Tanzania na ukitoka nje ya mipaka ya Tanzania kiswahili chako unaweka mfukoni! Lazima tujufunze lugha za kimataifa(English) ili tulahisishe mawasiliano na mataifa mengine.
2. Wageni wakija Tanzania wanapata taabu kweli, matangazo ya biashara yameandikwa kwa kiswahili, barabara nazo unakuta vibao vimeandikwa kwa kiswahil mfano PITA KUSHOTO. Sasa jamani wageni wetu ambao wengi wanakuja kwa maswala ya biashara inakuwa ngumu sana.Mgeni kuendesha gari tanzania ni ngumu sana. Mgeni kufanya biashara Tanzania ni ngumu sana!! Kuna jamaa wafanyabiashara wengi sana nawafahamu wanaprefer kwenda Kenya na Uganda kuchukua bidhaa kuliko Tanzania na sababu wanazozitoa ni ugumu wa Lugha.wanasema kwenda Tanzania ni gharama zaidi maana inabidi umtafute mkalimani ambaye utamlipa.
3. Kenya inatangaza mlima kilimanjaro kwa sababu ya Lugha wanayotumia inaeleweka duniani kote. Sisi tunatangaza mlima kilimanjaro kwa kiswahili wataelewa nini wageni?
4.Tunawasanii wazuri sana wa muziki, tamthiliya, vichekesho, ambao wangesaidia sana kuitangaza nchi yetu kimataifa na wao pia kufaidika, lakini wamebaki eti wasanii wa BONGO. (Kwa wale mliobahatika kuangalia stand up Zambia kilichorushwa na Africa magic channel mtakubaliana na mimi wale jamaa 3 walioshinda sasa hivi ni comedian wakimataifa wanazunguka nchi mabalimabali sababu ni lugha tu, maana kwa ukweli hawawezi kumfikia Joti, Masanja.
5.Tuna wachungaji wazuri sana(Pastors) lakini mahubiri yao ni kwa kiswahili. T.B Joshua anajulikana kila mahali kwa sababu mahubiri yake ni ya kiingeraza. Si kwamba Joshua unaupako kuliko wengine.
6. Mikataba mibovu tunayoingia na wawekezaji ni kwa sababu ya lugha tunashindwa kuilewa vizuri Wawekezaji wanapokuja ilitusionekane ni mbumbumbu wa kiingereza tunabaki kusema YES, YES YES!
7. Kwa watazamaji wenzangu wa aljazeera kuna kipindi kinaitwa 'Tea cafe (kama sijakosea)kinaongelea maswala mbalimbali yanayohusu nchi husika kipindi hicho kinapofanyika. Kipindi hicho kimefanyika,Kenya, Uganda zambia lakini Tanzania hakuna na hata katika ratiba yao Tanzania haimo simply because hakuna watu kama wanasiasa na baadhi ya watu mahalufu ambao wako tayari kujadili kwa kimombo! Sasa dunia itatuelewa vipi matatizo na mipango yetu ?
Nchi nyingi sasa hivi zinajifunza Kiingera hata china taifa kubwa wako busy kujifunza kiingereza Sisi masikini wakutupwa tunangangana na kiswahili ambacho mwisho wake ni mipakani tu! Viongozi wetu lazima pia waanalie hiyo watu waanza kufundishwa kiingereza tangu chekechea, maofisini lugha ya kiingereza isisitizwe, mikutano maofisini ifanyike kwa kiingereza. WITHOUT ENGLISH YOU ARE MARGINALIZED YOURSELF