Jana jumamosi nilisikiliza kipindi cha watoto katika redio fulani lakini ilinisikitisha jinsi muongozaji (mtoto mwenzao) alivyokuwa anahribu kiswahili. Kwa mfanoalikuwa anawauliza wenzie "ukiamkaga asubuhi unafanyaga nini?" Je huwa unaamkiaga wazazi wako? n.k. Kwa uelewa wangu ni kwamba vyombo vya habari ni nyezo muhimu ya kueleimisha jamii. Inasikitisha kuona kuwa wasimamizi wa vyombo hivyo hawazingatii ubora wa waendeshaji wa vipindi hivyo. Au ni kwa sababu ni vya watoto?