Kisingizio cha kubakwa

Bubu Msemaovyo

JF-Expert Member
May 9, 2007
3,832
2,790
Habari hii inasikitisha sana na nadhani kuna haja Bunge letu lifanye marekebisho ya sheria ya kujamihiana kwani imekuwa ni kawaida kwa akina mama kusingizia kubakwa wakati si kweli: Kwa habari za kina soma hapa chini.

http://www.mwananchi.co.tz/newsre.asp?id=5278

Mwanamke asakwa kwa kuidanganya mahakama kuwa amebakwa
Na Awila Silla , Singida

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Singida, inamsaka mwanamke mwenye umri wa miaka 38 aliyefungua kesi ya uongo akidai kubakwa na wanaume wawili.

Uchunguzi wa mahakama hiyo umebaini mwanamke huyo alidanganya kwa nia ya kutaka kujipatia kiasi cha Sh1.5 milioni 1.5 kutoka kwa ndugu wa washitakiwa waliyemtuma afanye hivyo.

Mwanamke huyo ambaye ni mkazi wa Majengo katika Halmashauri ya Manispaa ya Singida baada ya kugundua mahakama imebaini kuwa ni muongo, anadaiwa kutorokea kusikojulikana.

Agosti 16 mwaka juzi, mwanamke huyo aliyejulikana kwa jina la Tatu alifungua kesi ya madai ya kubakwa kwa zamu na wanaume na kupatwa maumivu makali sehemu zake za siri.

Kesi hiyo alifungua dhidi ya Ramadhani Lisu (42), mkazi wa Manga na Mohamed Majengo (45), wa Misinko- Singida Vijijini.

Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Agatta Chigullu alisisitiza kuwa, mwanamke huyo hakubakwa bali alifanya hivyo ili kutimiza ahadi aliyoahidiwa ya kupatiwa Sh1.5 milioni na ndugu wa washitakiwa waliotaka wanaume hao wafungwe jela ili wamiliki mashamba yao.

Baada ya makubaliano na ndugu wa washitakiwa hao, Tatu alitumia maarifa mengine ya kujitongozesha kwa Yusuf Msaghaa (68) kwa kumweleza kila kitu na kumtaka afanye naye mapenzi bila kinga ili apate uchafu au mbegu za kiuume ambazo zingetumika kama ushahidi kwa ahadi ya malipo ya Sh300,000.

Alisema baada ya tendo hilo, mwanamke huyo, alitoka mbio hadi jirani na nyumba za washitakiwa hao kisha kuanza kulia na kupiga yowe kuomba msaada huku akigaragara kwa madai kuwa amebakwa kwa zamu.

Alisema mayowe hayo, yalimaidia kupata msaada wa jirani akiwemo mmoja wa washtakiwa hao na kudai kuwa amebakwa.

Hakimu aliongeza kuwa, washtakiwa hao, walikamatwa na kupelekwa polisi na Tatu hospitali kwa uchunguzi zaidi na kukutwa akiwa na mbegu za kiume sehemu za siri.

Alisema wakati mahakama hiyo ikiwa katika harakati za kutoa hukumu dhidi ya washitakiwa hao , siri ilifichuka baada ya mwanamke huyo kugundulika kushindwa kumlipa fedha zote mzee aliyefanya naye mapenzi baada ya kufika mahakamani kutoa siri na vielelezo vya maandishi.

Kutokana na hali hiyo, mahakama hiyo ilifuta kesi hiyo na kuamuru Tatu kukamatwa na kufikishwa mahakamani hapo kujibu mashtaka ya kusema uongo.
 
Sasa iliwezekanaje watu hao walitiwa hatiani hadi yule mzee alipotoa siri?

Naona Kuna tatizo hapa kwenye taasisi zetu zinazohusika na mambo ya prosecution.

Na hao wahanga wanaweza kudai fidia yoyote?
 
Finger print????? fafanua!!!!!

Bubu usemaye

DNA finger prints is a technique that use DNA sequences to determine whether two DNA samples are from the same person, related people, or non-related people. Kila mtu ana DNA zake ambazo ziko tofauti na mwingine, in forensic science ama kuondoa utata wa mbakaji ni kuchukua DNA sampli za wahuhumiwa na kulinganisha DNA za kwenye shahawa alizokutwa nazo mwanamama, zikimatch basi utakuwa umemkamata mbakaji. Hii hutumika hata kukamata wababa wanaokimbia watoto wao...ama kujua wamama wanaosingizia akina BUBU watoto... umenielewa mkubwa?

if your more interested revisit this link http://www.accessexcellence.org/RC/AB/BA/DNA_Fingerprinting_Basics.html
 
Forensics experts please!!?
help needed

mkuu duh!!
mbegu na finger prints???

Kama mtuhumiwa aliacha traces za mbegu, ama nywele, ama damu DNA huweza tolewa kutoka kwenye moja wapo ya tissue ambazo mtuhumiwa aliacha...halafu DNA finger printing hufanyika soma link hiyo hapo juu....
 
Kama mtuhumiwa aliacha traces za mbegu, ama nywele, ama damu DNA huweza tolewa kutoka kwenye moja wapo ya tissue ambazo mtuhumiwa aliacha...halafu DNA finger printing hufanyika soma link hiyo hapo juu....

Pia unaweza angalia DNA za mtuhumiwa toka kwenye nguo za victim/mbakwaji au kama tendo lilitendeka kitandani basi ukikuta mavuzi yaliyokatika na kudondoka kwenye shuka pia waweza ku trace DNA za mtuhumiwa vizuri tu. lakini hoja kuu hapa je Polisi na Mahakama zetu zinaangalia kwa undani kesi kubwa kama hii? nakumbuka miaka ya nyuma katika Mahakama moja.... Mama mmoja aliangua kilio na kutoa siri baada ya mume wake kusukumwa jela miaka mingi tu (sikumbuki idadi), kumbe yeye na mumewe walikua na ugomvi wa siku nyingi ndani ya nyumba na alitegemea adhabu ndogo tu kwa kumsingizia mumewe kumbaka mtoto wao wa mgongoni. Pia kumbukeni kuwa bila DNA madaktari wetu ni bei ndogo sanasanasana kuidhinisha kuwa mbakwaji amekutwa na michubuko na shahawa kwenye sehemu za siri.NAWAOMBEA MUNGU AWASAIDIE WOTE WALIOTIWA HATIANI NA KUFUNGWA KUTOKANA NA USHAHIDI WA MADAKTARI ZETU
 
Genetic Fingerprinting (also called DNA testing, DNA typing, or DNA profiling) is a technique used to distinguish between individuals of the same species using only samples of their DNA.

Nadhani imeeleweka kwamba DNA fingerprinting inayazungumzwa hapa si alama za vidole.

Tuje kwenye hoja ya msingi.... kusingizia kubakwa (au kiujumla kumsingizia mtu kesi).
Ni kweli (japo sina takwimu) watu wanabambikwa sana kesi mbali mbali kwa kutumia udhaifu wa sheria zetu ama udhaifu wa watekelezaji wa sheria zenyewe. Kubakwa inaonekana kwamba ina madhara makubwa sana kwa mbambikiwa kwa sababu ya ukubwa wa adhabu na kushuka hadhi ya mhusika. Ukishtakiwa kwa ubakaji hata ukishinda kesi heshima yako katika jamii yako inakua imeshuka sana, achilia mbali muda utakaokuwa umekaa mahabusu!

Swali langu ni hili.... je, ukibambikiwa kesi ni adhabu gani inaweza kumkabili yule ambaye kwa malengo yake amekubambikia kesi husika? Kwa hili anayeongopa kubakwa anaweza kupata adhabu gani akingundulika?

Binafsi napendekeza mtu anayemsingizia mtu mwingine kosa fulani basi huyo msingiziaji apewe ile adhabu (maximum) ambayo angepewa yule msingiziwa (pamoja na fidia ya deformation). Sheria inasemaje hapa? Je, vipi kuhusu polisi wanabambikia watu kesi za mauaji?
 
Back
Top Bottom