Kisa cha Waziri Ngeleja na Mlinzi kwenye ATM

poor ngeleja..tulikuwa tunamfikiria kama anaweza kuwa kati ya kundi la mawaziri vijana ambao mwaka 2015 tutawafikiria kuwaunga mkono......lakini kumbe HAFAI ameshalewa ulevi wa ukubwa ....anatukana wanyonge matusi ya nguoni...,anavunja utaratibu..na kudharau watu ...na zaidi ya yote anangangania MNYONGE afukuzwe kazi.tena bila kosa ..kama adhabu....bila kuhesabu yeye amewatendea watanzania milioni 40 makosa mara ngapi yanayotugharimu kila siku....

kijana ngeleja ya have done a mistake which has just cost you your political future ....tunakuarifu kuwa tumefuta jina lako katika list ya potential runners wa 2015 na milele amina!!!!! forget that post!!!

Ngeleja Huna adabu!!!

Ninyi akina nani mlikuwa mnafikiria kwa ajili ya 2015? g'mme a break!! Hutakuwa na tofauti na yeye, kudhani kwamba kuna kundi la watu linaweza kuweka list ya potentials ya kutawala nchi hii.

As for Ngeleja, ninashangaa kama mtu yeyote yule anaweza kutoa maneno kama hayo, let alone kwa nafasi yake ya uwaziri.
Viongozi wengi wanadhani wako nje ya sheria na taratibu. Ni muda mwafaka akajiuzulu, hii si tu amekosa sifa ya kuwa waziri, bali amekosa sifa ya kuwa binadamu mstaarabu, tunaohitaji kuishi nao katika maisha ya kawaida.
 
Laligeni labda kama wewe ni learned sister/brother ujitoe kumsaidia!! vinginevyo usimuingize matatizoni mtanzania mwenzetu kwa kweli!!!

afu Ngeleja eti 'unanijua mimi ni nani'....who cares bana kwani hapo ulipo umanisaidia nini bana!! kwa taarifa yenu akija kwenye mgahawa wangu anapanga foleni kama mteja wangu yeyote(FIFO)!!! kwani zake ni za dhahabu!!!


Mkuu Umenena. I really hate a person who starts an mkwara wa 'Unanijua mimi ni nani?' Nikujue ili iweje bana? nakuona una mikono miwili, miguu miwili, macho mawili, sili kwako na kadhalika so definitely you are a fellow Human Being and not a Martian from a far, far away galaxy!SO WHAT? :mad:
 
Bahati yake mbaya sikuwa wa pili kwenye hiyo foleni, maana nisingesubiri mlinzi amtoe, ningemwambia mwenyewe i want to use this service so you can continue to talk in your car.

tena kwa kibluray?????!!!!! hahaaa angekupisha fasta (lakini ungeanza na eksichuzi mi saa). kwa mfano sasa ndo umwambie hivo afu ndo hiyo responsi iwe kwako carmel ungechukua hatua gani kwa muhishimiwa waziri kijana???
 
Kama ni kweli basi mhh sijui tunakoelekea na hii kauli mbiu yetu ya uongozi bora maana hapa kinachooonekana ni bora kiongozi anaweza akafanya alitakalo maana yeye ndiye ameshika mpini. wengine hawajui kuwa cheo ni dhamana na aliyekupa wewe cheo ndiye aliyempa huyo mwingine ulinzi wa ATM.

Ingekuwa busara kuona cheo chake kuwa hakistahili kumnyanyasa mtu mdogo na badala yake angewaomba radhi hao wananchi waliopanga foleni kumsubiri yeye tena hata kwa kuwadandanya tu. jamani ndugu zangu samahanini nilikuwa na dharura. angepungua nini? tena si ndio wangezidi kumpenda na kumheshimu. na huyo mlinzi angegundua kuwa he kumbe ni Waziri angemuomba radhi kwa kumsumbua bila kutarajia.

Tukilewa madaraka maskini siku zote atakuwa mnyonge na hatakuwa na wakumtetea. Awahurumie tu watoto wa huyo mlinzi ajue kuwa akisababisha huyo mlinzi afukuzwe kazi watoto wake watahangaika sana je kama ni yeye atafurahi, au dhamira yake itajisikiaje.

Ila kama huyo mlinzi anamakosa basi yawekwe hadharani kuwa amefanya hivi na hivi na adhabu yake ni hivi ili iwe fundisho kwa wengine. na dhana ya uonevu itoweke kuwa anaonewa bure.
 
Mkuu Umenena. I really hate a person who starts an mkwara wa 'Unanijua mimi ni nani?' Nikujue ili iweje bana? nakuona una mikono miwili, miguu miwili, macho mawili, sili kwako na kadhalika so definitely you are a fellow Human Being and not a Martian from a far, far away galaxy!SO WHAT? :mad:

aaah si ndo hapo sasa babadesi!!! hata nikujue inanisaidia nini mtanzania ninayeteseka na wewe unabonyoa tu PAYE inayoniumiza kila mwezi dispite ya kijisalary ambacho hainikidhi hata basic needs!!
 
aaah si ndo hapo sasa babadesi!!! hata nikujue inanisaidia nini mtanzania ninayeteseka na wewe unabonyoa tu PAYE inayoniumiza kila mwezi dispite ya kijisalary ambacho hainikidhi hata basic needs!!
ha ha ha bibie umeiandika kiuchungu sana kama angekua mbele yako ungempa makofi teh teh!! Ndio bongo ilivyo ye anajua wote tunaangalia TV so tht utakua unamjua tuu!! Heri ya mwaka mpya!
 
Nalazimika kuamini kuwa hii habari kuwa ni ya kweli. Iwapo huyo mlinzi atafukuzwa tumtetee na kuhakikisha anarudishwa kazini.

Naomba mwana JF yeyote ajitolee ili tuweze kupata taarifa kamili kwa kumuhoji kwa kina huyo mlinzi na waziri pia. Waandishi tunaomba mumtafute waziri ili atoe maelezo yake na aueleze umma wa watanzania kama hizo tuhuma ni za kweli au uongo. Pia aeleze kama alimtukana huyo mlinzi. Kama alimtukana tutaomba awaeleze Watanzania matusi aliyomtukana huyo mlinzi na kwa nini aliamua kumtukana kama alifanya hivyo.

Wana JF tuzo yetu ni nini kwa huyo mlinzi kama itadhihirika kuwa hii habari ni ya kweli na hakuna umbea wowote wala fitina?
 
Ole wako!!
Ole wako wewe trafiki ukimzuia Ngereja kwenye foleni kupisha magari mengine
Ole wako Dala dala usipompisha Waziri kijana, utamjua yeye nani
Ole wako pale kanisani usipompisha kiti, hujui yeye waziri?
Ole wako msoma mita wa Dawasa, ukisoma mita ya Ngereja kibarua hichooo!
Ole wako wewe mwananchi ukimwona Ngereja anakuja usimpishe njia
Hatimaye, OLE WAKO NGEREJA ANAKUJA!!!
 
ha ha ha bibie umeiandika kiuchungu sana kama angekua mbele yako ungempa makofi teh teh!! Ndio bongo ilivyo ye anajua wote tunaangalia TV so tht utakua unamjua tuu!! Heri ya mwaka mpya!

umenisoma kiundani wewe chaaaaaaaaaaa!! heri ya mwaka mpya wa uchaguzi Kimey!!! ila sijui kweli kama ntapoteza mda wangu kwenye foleni ya kupiga kura in the name of 'eksesaizing my voting right'

unanijua mimi....jamaa tv yenyewe anachabo kwa jirani tena michezo ya kuigiza sasa Ngeleja atamjuaje???

hata akimjua bana sasa ndo uwapotezee watanzania wengine wenye haraka ya kupata huduma na kwenda kuhanja huko, kisa unaongea na simu!!!

nyamabafu kwanza PAYE kubwa kuliko PPF na NSSF. ahhhhh mi naumia kweli
 
umenisoma kiundani wewe chaaaaaaaaaaa!! heri ya mwaka mpya wa uchaguzi Kimey!!! ila sijui kweli kama ntapoteza mda wangu kwenye foleni ya kupiga kura in the name of 'eksesaizing my voting right'

unanijua mimi....jamaa tv yenyewe anachabo kwa jirani tena michezo ya kuigiza sasa Ngeleja atamjuaje???

hata akimjua bana sasa ndo uwapotezee watanzania wengine wenye haraka ya kupata huduma na kwenda kuhanja huko, kisa unaongea na simu!!!

nyamabafu kwanza PAYE kubwa kuliko PPF na NSSF. ahhhhh mi naumia kweli
Hapo kwenye nyekundu hapo umepiga penyewe!! teh teh teh
 
Ninacholiomba kila mlinzi apewe ring(pingu) akija jinga jinga kama huyu kata funua halafu unaweka chini ya ulinzi na pingu tayari halafu habari nyengine itafuata baadae,

Unajuwa wadanganyika enzi zile shuleni ni lazima uwakariri viongozi wote tokea shina hadi taifa, sasa huyu jamaa bado yuko enzi za mwaka 47,

mlinzi naona amefanya usamaria sana tu hata kukubali et kumuomba msamaha mtu aliyekukosea, kweli huyu mtu analinda kibarua chake na so called WAZIRI bado anatowa kauli za longolongo eti mpaka apewe adhabu kali hivi yeye apewe adhabu kali au wewe upewe adhabu kali, Hivi uweze kuchaguliwa waziri kwa Danganyika, wanapimwa IQ zao
Now sishangai kwa mikataba mibovi kwa uongozi huu,
Ushauri kwa JK angalia watu wako kabla ya kuwapa uongozi, sio wote viongozi, wengine ni mizigo
 
Masikini mlinzi wa watu anaweza kufukuzwa kazi kwa kumwambia tu huyo waziri kuwa kuna watu wanataka kutumia ATM. Hawa ndio viongozi wetu mafisadi ambao hawajali utu wa wapiga kura!
 
Huyu the so called Ngereja anaonekana ni Mshamba sana na mambo ya ATM... Tangu lini aliona kwamba vibanda vya ATM ndio vya kufanyia maongezi ya simu... au alikuwa na mpango wa kufanya kama Wale Wa-bulgaria...

Halafu hii ya kumtishia mtu eti hivi hunijui... kwani yeye ni kiumbe adimu? Anajulikana kwamba yeye ni binadamuwa busara, na kilichokuwa kinafanyika ni kumkumbusha kwamba kulikuwa na msururu wa watu unangojea kutumia facility hiyo na sio peke yake...

Pia ya nini Ngereja kufanya yote hayo mpaka mlinzi wa watu kuitwa ofisini kwake? Haya ni matumizi mabaya sana ya ofisi ya Ngereja... Ofisi ni mali ya umma na inabidi iheshimiwe na si mahala pa kuingia kila kitu hata walinzi wa ATM. Inafaa ngereja aitwe NGEDELE maana ni huyu mnyama pekee anayerushiwa jiwe na kukurushia tena jiwe hilo...
Pia inafanaa awajibike kwa matumizi mabaya ya ofisi ya umma kwa kujiuzuru haraka sana... kama angekuwa na kasi ya kushughulikia matatizo yetu basi Umeme ungewaka TANZANIA masaa 24 siku 365 za mwaka...

Amenikera sana na namlaani kwa kitendo chake cha kutaka mwenzake aoteshe kibarua chake majani...

Who should go in Sir??? You are OFFF!!!!
 
Hapo kwenye nyekundu hapo umepiga penyewe!! teh teh teh
afu si unaona eeeh Ngeleja eti analeta jeuri usikute na yule askari aliyetukanwa tuhela twake tunakwatwa PAYE...aaah jamani nyie
 
- Demokrasia inataka kusikiwa kwa pande zote mbili, tumesikia moja ya Mlinzi na mashahidi wasiotaka kutajwa majina yao, huu ufisi ufisi wa kuogopa kutaja jina wakati unadai umeona kwa macho yako Waziri "akimu-abuse" malalahoi mwenzio ndio unatuponza na kuishia kulia lia ndani ya mablanketi, it stinks!

- Now this ni habari ya amesema hakusema, alifanya hakufanya mimi nimeuona lakini sitaki jina langu litajwe, the whole thing is pathetic!

- Mlinzi ametukanwa na Waziri bila sababu kwa nini asiwahi kwenye sheria na anajua kuna mashahidi waliosikia na kuona? Something is not right na hii habari!

Respect.

FMEs!
 
Haya mambo kwa watawala wa Tanzania mbona yapo siku nyingi sana, sema enzi hizo tulikuwa na magazeti ya chama na serikali tu si rahisi kuyajua. Hivi unafahamu kuwa Makamba alipokuwa mkuu wa mkoa wa Morogoro aliishamtandika vibao mama wa kihindi aliyekuwa anamwaga uchafu sehemu isiyostahili barabarani?.

Hivi mnajua kuwa watawala wengi wanatumia nafasi zao kuvunja ndoa za watu kwa kurubuni wake za watu waachane na waume zao walalahoi na kuishia kuishi nao.

Ngeleja alichochemsha hapa ni kuruhusu public kujua mambo yake kuwa naye ni mtovu wa nidhamu kama walivyo wenzake wengi tu. Ngeleja ni reflection ya watawala wengi wa nchi, wao kila siku wanajiona kuwa ni first class citizens.

Ingekuwa Tanzania kuna demokrasia ya kweli, yaani matokeo ya uchaguzi ni reflection ya matakwa ya wananchi, tungeshuhudia heshima kubwa sana wananchi wanapewa na viongozi. Ila kwa kuwa wananjua kuwa watajitangaza washindi wa uchaguzi wananchi hatuwababaishi
 
Waziri Ngeleja nusura azichape kwa adha ya ATM Dar Ochu
user_online.gif
Today, 05:52 AM
- Hivi hebu tuwe Great Thinkers japo kidogo tu, katika hii article ni wapi hasa panapoashiria kwamba Waziri alitaka kuzichapa? Mbona kama kichwa cha habari na habari hazifanani?

NI BAADA YA KUTAKIWA AWAPISHE WATEJA

Sadick Mtulya

WAZIRI wa Nishati na Madini, William Ngeleja, juzi alizua tafrani kwenye mashine ya kuchukulia fedha (ATM) ya benki ya Standard Chartered, jijini Dar es Salaam baada ya kutaka kumchapa makonde mlinzi wa mashine hiyo, Pascal Mnaku. Habari zilizolifikia gazeti hili jana na kuthibitishwa na mlinzi huyo wa kampuni ya Ultimate Security, zimeeleza kuwa tukio hilo lilitokea juzi saa 3:00 asubuhi kwenye jengo la Habour View, maarufu kama JMall.

Mnaku aliliambia gazeti hili kuwa alinusurika kupigwa na waziri huyo kijana aliyekuwa akizungumza na simu ndani ya kibanda hicho, baada ya kumtaka atoke kuwapisha wateja wengine kupata huduma hiyo. Mnaku alisema waziri huyo alikuwa anatumia muda mwingi kuzungumza na simu ndani ya mashine hiyo badala ya kuchukua fedha wakati msururu mrefu wa watu ukiwa unamsubiri atoke.

"Kwanza mimi sikujua kwamba mtu niliyemwambia awapishe wateja wengine ni waziri. Ni kweli nilimfuata na kumwambia awapishe kwa sababu alikuwa anatumia muda mwingi kuzungumza na simu, wala sikuwa na nia nyingine yoyote mbaya dhidi yake," alisema Mnaku na kuongeza:

"Lakini, waziri huyo ghafla aligeuka na kuanza kunifokea akiniambia wewe unanijua mimi nani?... hunijui mimi! na kunitusi, (matusi yasiyoweza kuandikika)."

Mnaku aliendelea kueleza kuwa; "Kutokana na hali hiyo nilipomjibu kwamba, mimi sikuwa na nia mbaya na nilifanya vile ili wateja wengine wapate huduma". Aliongeza: "Baada ya kumwambia hivyo akazidisha ukali, lakini watu walipoanza kukusanyika, huku wengine wakimwomba radhi kwa kumtaja jina, alianza kupunguza hasira na kuondoka".

Kwa mujibu wa mlinzi huyo, baada ya tafrani hiyo iliyodumu kwa takribani dakika nane, Waziri Ngeleja aliondoka na baadaye kunako majira ya saa 7:00 mchana uongozi wa kampuni yake ya ulinzi ulimwondoa katika kituo hicho cha kazi na kurudishwa makao makuu. Alisema saa 9:30 jioni, alichukuliwa na uongozi wa kampuni hiyo na kupelekwa ofisini kwa Ngeleja kwa ajili ya mazungumzo zaidi.

"Baada ya kutokea kwa tukio saa 9:30 jioni wakuu wangu walinipeleka ofisini kwa Ngeleja na kisha akazungumza mengi ambayo siwezi kukuambia na baada ya hapo wakuu wangu wakamuomba msamaha kwa niaba ya kampuni," alisema Mnaku. "Na kwa sasa maelekezo niliyopata kutoka kwa waajiri wangu ni kwamba, wanalifanyia upelelezi suala hili hivyo hatima ya kibarua changu kinategemeana na majibu ya upelelezi huo," alisema Mnaku

Mashuhuda wa tukio hilo walilieleza gazeti hili kuwa hali hiyo ilijitokeza baada ya Mnaku kuwahamishia wateja kutoka katika mashine ya ATM ya Barclays iliyoko katika jengo hilo ambayo wakati huo ilikuwa imeishiwa fedha.

"Baada ya Mnaku kuona mashine ya ATM ya Barclays kuwa haina fedha, ndipo akalazimika kuwaambia wateja wakatumie ATM ya Standard Chartered ambayo wakati huo Waziri Ngeleja alikuwa anaitumia na huku akizungumza na simu,” alisema shuhuda mmoja ambaye hakutaka jina lake liandikwe.

Shuhuda huyo alisema baada ya Mnaku kumtaka waziri kuwapisha wengine, ghafla na huku akiwa na hasira, Waziri Ngeleja alisema: "Ina maana hunijui mimi, hujui nafasi yangu, halafu...tusi," alisema shuhuda huyo.

Shuhuda huyo aliongeza: "Kutokana na maneno hayo, Mnaku akamjibu kwa kujitetea kwamba, mimi nimekuomba uwapishe wateja wengine, sikuwa na lingine".

Habari zaidi zinadai kwamba, katika kikao na waajiri wa Mnaku, Ngeleja alisema: "Siwezi kumsamehe (Mnaku) mpaka atakapopewe adhabu kali."

- Exactly ni wapi ambapo Waziri nusura amchape? Just trying aloud to be a Great Thinker!

REspect.


FMEs!
 
Back
Top Bottom