Kisa cha Rais Ali Hassan Mwinyi kipigwa kibao akihutubia

Nimeshuhudia kwa macho yangu tbc one mwinyi akilambwa kibao, ni kama ilikuwa sinema, kijana huyo alipanda jukwaani na kumlamba kibao, na wakati akishuka jukwaani ndipo alipobanwa na kuanza kushuhulikiwa, hata ahivyo mwinyi alikuwa mpole na kuhimiza hadhira ilyokuwa inamsikiliza kuendela na mdahalo, huku mbaya wake akishuhulikiwa chini ya miguu yake



akina mwinyi na viongozi wengine wa siasa , wanapaswa kutambua vizuri hadhira inayowazunguka, yeye kuhimiza matumizi ya kondomu ni sawa na kuwaambia waislamu wale nguruwe, yote ni haramu , yaani kujamiana kabla ya ndoa na kula nguruwe zote ni haramu, ni sawa pia ukikaribishwa vatican uanze kuhubiri kutoa mimba na hata kutumia kondomu.

Viongozi wa siasa watumie vizuri majukwaa yao, na wanapokuwa kwenye majukwaa ya kidini wawe macho. Mambo ya kidini ni very sensitive, huenda kijana aliyempa kibano tayari ana thawabu according to holy quaran

mfano mimi ni mkatoliki, nikifa kwa kukemea kutoa mimba tayari nimekufa kama shahidi wa kuitetea nchi yangu

pia, nawalaumu wanaozidi kumfuata mzee kama mwenye at his age of 80s, tayari amechoka kiakili

Si kweli kwamba Uislamu unakataza categorically matumizi ya condom, si kweli matumizi ya condom huwa tu wakati wa nje ya ndoa.

Ukosefu wa elimu ya dini unasababisha tafsiri hii. rejea tundiko langu la hapo juu # 33
 
Du tz kweli noma---Pole msee wetu.

Naomba kuuliza pia Mauldi na kesho inaendelea kama siku ya mapumziko ama vipi?
 
=====

Ndugu DSM

Kumbuka Mzee Mwinyi alikuwa anamwakilisha Rais Kikwete katika hafla hiyo.
Kikwete alialikwa kama Mkuu wa nchi lakini akawa na hudhuru na kumtuma Mzee Mwinyi. Hata kama wote wawili ni waislam, lakini kuwapo kwao pale waliwakilisha serikali kuonyesha mshikamano wa dini na serikali. Mchapaji kibao amechemsha, na ashukuru Mungu hakuwa JK kwani shaba ingewaka na labda jamaa sasa angekuwa "paradiso" na kupata thawabu yake aliyoahidiwa kwa kujitoa mhanga kumchapa kibao Mkuu wa nchi.

Kama ni kweli kaleta jipya ambalo haliruhusiwi katika uIslam basi namuunga mkono mchapaji.

Lakini najikumbusha kuwa, kwenye halaiki ya watu, wengine ni machizi, pengine Mwinyi hakuleta chochote kipya au cha kuudhi bali tuu, jamaa ni chizi. Kama ni hivyo basi nampa pole Mzee Mwinyi na jamaa akapimwe akili.
 
Nimeona tendo hili la kishenzi ndani ya ITV. Kwenye picha inaonekana hata mzee Mwinyi alimshitukia mtu aliyekuja bila kutarajiwa. Alimpiga jicho kidogo halafu akaendelea na mambo yake. Jamaa akavunga kidogo halafu akamwasha kibao ambacho kimetoa hata echo.

I think this is really barbaric na I froze like ice. Watu wote niliokuwa nao really walikuwa embarassed. Kuna watu wanaongelea dini, siasa, .... Tuache upuzi tuwe wakweli katika nafsi zetu. Kitendo hicho ni cha kishenzi kabisa na aliyefanya lazima alipanga.

Suala ni kuwa tendo hili lime-expose security systems zetu vibaya mno. Hivi kweli viongozi wetu wana ulinzi wowote? Kwa jinsi nilivyoona kwenye picha.... assessment yangu inaniambia kuwa hakuna ulinzi. Yule mtu mzee Mwinyi alionekana kumsitukia. Lakini jambo rahisi, huyo mtu alikuwa kati ya watu wanaotakiwa kuonekana high table wakishughulikia vipaaza sauti? Hivi tuna ulinzi?

Siku raisi wa China alipofungua uwanja wa Taifa pale uwanjani Kikwete alilalamikia jinsi vipaaza sauti vilivyo kuwa vimewekwa. Kama vile aliyeviweka hajui urefu wa Kikwete. Hili la Mwinyi kupigwa si jambo dogo hata kidogo!

HIVI USALAMA WA TAIFA NI GENGE LA MAFISADI?
 
Nasikia watu wanaohusika na usalama walimpiga mtuhumiwa mtama na kuanza kumpiga --- sasa kama huyo mtu ana support nyuma yake basi itakuwa balaa haya ni mambo ya kuongea na kuelewana viongozi hawa wawe wanashauriwa cha kuongea kutokana n hali halisi
 
Kama ni kweli kaleta jipya ambalo haliruhusiwi katika uIslam basi namuunga mkono mchapaji.

Lakini najikumbusha kuwa, kwenye halaiki ya watu wengine ni machizi, pengine Mwinyi hakuleta chochote kipya au cha kuudhi bali tuu, jamaa ni chizi. Kama ni hivyo basi nampa pole Mzee Mwinyi na jamaa akapimwe akili.

Kama hujui kama ni kweli Mwinyi kaleta kipya, ku speculate kuhusu kumuunga mkono "mchapaji" ni hatari. Unaunga mkono uchapaji bila kujua msingi wake? Hapo kuna a very central BUT.

Inabidi ujue kwanza, halafu unatoa maamuzi, sio unatoa maamuzi yaliyo na conditionalities kibao kama program ya computer.
 
Kama kazabwa kibao kwenye sherehe ya kiIslam na yeye ni muIslam na kenda kuwaambia waIslam wenzake wavae kondom, wakati kama ni muIslam anatakiwa ajuwe kuwa uIslam hauruhusu kabisa ngono bila ndoa, iwe kwa kondom au bila kondom, basi hilo ni kosa, hata kama ni Rais hayuko juu ya uIslam, hawezi kuleta mafundisho mapya kwenye uIslam.

Kama ni kwa hayo niliyoyaeleza hapo juu, nampa pongezi huyo muIslam na kama si kwa hayo kuna data zingine zaidi ya hayo, basi ntaamuwa ntakapozipata.

Mzee kala chumvi nyingi na ametumia busara zake kuwaaza waamini wenzake watumie KONDOM kwa sababu ameshaona maadili ya UISLAM hayafuatwi na wengi.Hivyo ni bora awanusuru kwa hilo ili kama watamrudia tena MUUMBA WAO wafanya hivyo wakiwa free from HIV/aids and STDI
 
Jamani nina ombi: Kuna mtu humu ana picha ya Bush akirushiwa kiatu. Sasa tuna mtu kamchapa Mzee Mwinyi kofi: JK aliwahi kuanguka jukwaani. Je twaweza kupata picha hizi kwenye jamvi?
 
fikiria kama angekuwa na silaha sasa hivi ungekuwa msiba mkubwa bado turudi tusichanganye siasa na masuala ya dini kama viongozi wengi wanavyojaribu kufanya
 
jamani nina ombi: Kuna mtu humu ana picha ya bush akirushiwa kiatu. Sasa tuna mtu kamchapa mzee mwinyi kofi: Jk aliwahi kuanguka jukwaani. Je twaweza kupata picha hizi kwenye jamvi?

raisi wa china nae aliwahi kurushiwa kiatu na siku za karibuni raisi wa iran nae alirushiwa
 
fikiria kama angekuwa na silaha sasa hivi ungekuwa msiba mkubwa bado turudi tusichanganye siasa na masuala ya dini kama viongozi wengi wanavyojaribu kufanya

Umesema kweli. Jana tumeona kwenye vyombo vya habari, kuwa Mchungaji wa Illinois, USA aliyeuawa kanisani na muumini aliyeenda mbele kama anataka kumsalimia. Mnakumbuka mtu aliyemwua Rais Kabila mkubwa Ikulu. Mnakumbuka Mtu aliyemfokea Rais Mkapa wakati wa uzinduzi wa mfuko wa Waislamu, DSM. Mambo haya ni ya kuangalia sana, yanaweza kuleta msiba mkubwa kwa taifa. Idara ya Usalama wa Taifa imetekwa na mafisadi, inahangaika kuwalinda huku ulinzi wa viongozi ukiwekwa mashakani.
 
Bado natafakari vipi kama angepigwa hayo makofi na Mkristu? Pole mzee ruksa!

Nasikia jamaa alijifanya kama anakwenda kurekebisha microphone, akayeyusha kisha kamwachia bao.Kwahiyo body guard wake akabaki anaduwaa. Zikapigwa Takbir kadhaa, jamaa akashambuliwa kama mpira wa kona na waumini wenzie. Naona na yeye amepata ujira wake wa kutosha
 
....Kuna watu wanaongelea dini, siasa, .... Tuache upuzi tuwe wakweli katika nafsi zetu. Kitendo hicho ni cha kishenzi kabisa na aliyefanya lazima alipanga.

Suala ni kuwa tendo hili lime-expose security systems zetu vibaya mno. Hivi kweli viongozi wetu wana ulinzi wowote? Kwa jinsi nilivyoona kwenye picha.... assessment yangu inaniambia kuwa hakuna ulinzi. Yule mtu mzee Mwinyi alionekana kumsitukia. Lakini jambo rahisi, huyo mtu alikuwa kati ya watu wanaotakiwa kuonekana high table wakishughulikia vipaaza sauti? Hivi tuna ulinzi?

Siku raisi wa China alipofungua uwanja wa Taifa pale uwanjani Kikwete alilalamikia jinsi vipaaza sauti vilivyo kuwa vimewekwa. Kama vile aliyeviweka hajui urefu wa Kikwete. Hili la Mwinyi kupigwa si jambo dogo hata kidogo!

HIVI USALAMA WA TAIFA NI GENGE LA MAFISADI?

Kipimapembe

Umepima pembe vema. Usalama wa Taifa watake wasitake na hata watuchukie hapa JF tutaendelea kuwaonyesha kuwa wako dhaifu.

Walikwishaona tukio lililomkuta Bush, walitakiwa na hadhari kwa kipindi hiki. Au Mwinyi hana ulinzi wa UwT?
 
Dar,

Argument yako inateleza pale unapofikiri kwamba condom zinatumika nje ya ndoa tu, condom zina matumizi mengi, ikiwapo uzazi wa mpango, ambapo hata ndani ya ndoa hutumika.

Swala la uislam ni gumu na linahitaji mjadala zaidi, kwa sababu vitabu vyenyewe vina tafsiri nyingi, kuna sehemu wanasema huwezi kukojoa ukielekeza utupu kibla, sehemu nyingine msomi wa dini akakutwa anakojoa huku utupu kauelekeza kibla akasema unaweza kukojoa ukiuelekeza utupu kibla kama kuna jengo au kitu kati yako na kibla, kwa hiyo kuna hadithi na tafsiri nyingi, kwa hiyo hatujui Mzee Ruksa alikuwa anaongelea katika context gani, na mpaka tukijua hilo, na kuangalia misahafu, tafsiri za hadithi na miongozo mingine ya masheikhs wasomi wa uislamu, ndipo tutajua.

Ona hapa, ukisoma utaona ukosefu wa elimu ya dini unaweza kusababisha mambo ya aibu kama hili la kumpiga kibao mzee wa watu, mzee aliyelitumika taifa kwa muda mrefu na ingawa mabaya mengi yametendeka chini yake, kuna mazuri mengi aliyafanya na mfano wake wa kuigwa wa kujiuzulu kwa integrity unawasuta ma fisadi wanaong'ang'ania madaraka katika scandals zote za leo.

Islam: Condom, sustenance, condoms


Question
As Salaam Walikum Sir
I am sorry to ask can i use condom with my wife because with the grace of ALLAH i have one child at present i dont want another so please tell me can i use or not?
And if not tell me what is the way not to have a child now because the frist child is not at complete one years aslo
please give me proper islamic way

Jazak ALLAH kahir
MOHAMMED

Answer
Yes, you may use temporary contraception, like condoms, to space yur children. Doing so isn't taking a child's life which what is condemned. 17:31 Kill not your children for fear of want: We shall provide sustenance for them as well as for you. Verily the killing of them is a great sin.
Also for the mother's health you may use condoms- there is no harming of oneself in Islam.

Na kama Mwinyi alikuwa akiizungumzia Kondom kwa uzazi wa majira au kwa afya ya mama ndani ya ndoa basi you have got the point, otherwise, jibu unalo nadhani.
 
This is a very serious issue kwa usalama wa viongozi wetu wa kitaifa. Kama huyu mtu ameweza kumzaba kofi, ina maana kama angekua na kisu cha mfukoni angeweza kumuua.

Nashangaa mjadala huu unapoangaliwa kidini. So far, hakuna sehemu iliyoripotiwa kuwa huyo jamaa alimpiga kibao mwinyi kwa kupinga alichosema. Hakuna sehemu iliyoripotiwa dhehebu lake la kiimani. Hivyo basi mpaka sasa, hili suala linabaki kua la kiusalama na uzembe kwenye ulinzi wa viongozi wetu. Na kinachoshtua zaidi ni mtu kumfuata kiongozi mpaka high table na kufanikisha azma yake... Najua TISS watasingizia jamaa kichaa kuua noma.

Hiyo security detail yake ilikua wapi? au kumwaga mbwembwe tu na viearpeace...maana utakuta mtu yuko over 55yrs, mwili unamkaribia kapteni Komba anang'ang'ania kuwa bodyguard wa viongozi, ilimradi tu asipitwe na safari za nje au sababu ni "zamu" yake.

Mkuu Icadon ametuonyesha rika la walinzi wa viongozi wa nchi mbalimbali, mfano mzuri Israel. Jamaa ni vijana wadogo 20-30yrs, wako fit, na well armed. Kuwa openly armed in itself ni detterence tosha kwa wakorofi kama hawa.

Its about time the whole TISS iwe overhauled kabla makubwa zaidi hayajatokea.
 
Kama kazabwa kibao kwenye sherehe ya kiIslam na yeye ni muIslam na kenda kuwaambia waIslam wenzake wavae kondom, wakati kama ni muIslam anatakiwa ajuwe kuwa uIslam hauruhusu kabisa ngono bila ndoa, iwe kwa kondom au bila kondom, basi hilo ni kosa, hata kama ni Rais hayuko juu ya uIslam, hawezi kuleta mafundisho mapya kwenye uIslam.

Kama ni kwa hayo niliyoyaeleza hapo juu, nampa pongezi huyo muIslam na kama si kwa hayo kuna data zingine zaidi ya hayo, basi ntaamuwa ntakapozipata.

Mkuu mimi nafikiri kwa maisha ya sasa sioni Kosa la Mzee Mwinyi na naamini kabisa kwamba you cant compete with nature na hili ndilo waumini wa madhehebu yote hawataki kulikubali. Issue ya ngono ni very complex hasa kwa sisi waafrika na wengineo sasa kama tutafumbia macho issue ya kondom nafikiri tutazidi kuangamia ingawa naelewa kusema kwamba watu wavae kondom kwenye dini ni kuchochea ngono ila nafikiri akili inakuwa kumkichwa kwa kila muhusika.
 
Nimeona tendo hili la kishenzi ndani ya ITV. Kwenye picha inaonekana hata mzee Mwinyi alimshitukia mtu aliyekuja bila kutarajiwa. Alimpiga jicho kidogo halafu akaendelea na mambo yake. Jamaa akavunga kidogo halafu akamwasha kibao ambacho kimetoa hata echo.

I think this is really barbaric na I froze like ice. Watu wote niliokuwa nao really walikuwa embarassed. Kuna watu wanaongelea dini, siasa, .... Tuache upuzi tuwe wakweli katika nafsi zetu. Kitendo hicho ni cha kishenzi kabisa na aliyefanya lazima alipanga.

Suala ni kuwa tendo hili lime-expose security systems zetu vibaya mno. Hivi kweli viongozi wetu wana ulinzi wowote? Kwa jinsi nilivyoona kwenye picha.... assessment yangu inaniambia kuwa hakuna ulinzi. Yule mtu mzee Mwinyi alionekana kumsitukia. Lakini jambo rahisi, huyo mtu alikuwa kati ya watu wanaotakiwa kuonekana high table wakishughulikia vipaaza sauti? Hivi tuna ulinzi?

Siku raisi wa China alipofungua uwanja wa Taifa pale uwanjani Kikwete alilalamikia jinsi vipaaza sauti vilivyo kuwa vimewekwa. Kama vile aliyeviweka hajui urefu wa Kikwete. Hili la Mwinyi kupigwa si jambo dogo hata kidogo!

HIVI USALAMA WA TAIFA NI GENGE LA MAFISADI?

Apparently feeble and fragmented organization. What a shame on you TISS!
 
Kama hujui kama ni kweli Mwinyi kaleta kipya, ku speculate kuhusu kumuunga mkono "mchapaji" ni hatari. Unaunga mkono uchapaji bila kujua msingi wake? Hapo kuna a very central BUT.

Inabidi ujue kwanza, halafu unatoa maamuzi, sio unatoa maamuzi yaliyo na conditionalities kibao kama program ya computer.

Nimekusikia, lakini msimamo wangu uko palapale, kama Mwinyi kaleta jipya la kuwapotosha waIslam ndio akazabwa kibao, basi astahili yake. Lakini kama huyo ni chizi au muhuni tuu basi nampa pole sana Mzee Mwinyi.

Huo ndio msimamo wangu, wako baki nao ungojee data zaidi.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom