Kisa cha "Mjamaika" kimezua jambo! -

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Nusura nipost sehemu ya mwisho ya "Kumbatio" ndipo nimekutana na email ndefu yenye kunilalamikia na kunidokeza kuwa kisa hiki kimetokana na kisa cha kweli na kuwa yawezekana nimesimuliwa na mtu wa karibu wa wahusika. Na kwamba licha ya kujaribu kugeuza mambo mbalimbali kisa hicho ni kweli kimemkuta bosi fulani ambaye ni mwanasiasa maarufu.

Baada ya kuandika kwa kirefu, mwandishi (ambaye anajina la huyo bosi na nikitaja tu wote mtamjua) anamalizia kwa kunipa wito, kunitaka, kuniamuru or whatever have you...
....Ninakusihi usiendelee kubandika simulizi lako hilo kwani linanikumbusha machungu ambayo nimeyapitia na limeshazua mtafafuru kati yangu na baadhi ya marafiki ambao walikuwa wanajua undani wa kilichotokea kati yangu na mke wangu. Kilichotokea "Jumamosi" hakifai kusimuliwa wala kujulikana kwani ni ndiyo nimefanya makosa na nimeyalipia mara mia moja na pamoja na hayo tuliamua kuendelea kuwa pamoja.

Kukisoma kisa chako hadi kilipofikia kimeshatonesha madonda mengi na kurudisha kumbukumbu ya matukio ambayo tulishaamua kuyaacha yapite. Chonde, tafadhali mwanakijiji pamoja na kutumia mbinu zote za kiuandishi kuwaficha wasomaji wako watu wanaofahamu kisa chetu watagundua mapema kabisa kuwa ni nani anazungumziwa.

Naomba usimalizie hicho kisa na niko tayari kuzungumza nawe kwa herufi kubwa ili tuweze kuyamaliza kiutuzima. Tayari nimeshaabika siko tayari kuabika tena hasa kama magazeti ya udaku yatakipata kisa chako. ....

Baada ya kurudia rudia kijibarua hicho nimejikuta nina utata na kuanza kujiuliza maswali kwani ni kweli kisa hicho kimevuviwa na tukio la kweli japo simulizi lake ni la kutunga na manjonjo yamo humo humo lakini kwa asilimia 100 jina la huyo bwana halihusiani na kisa labda matukio yamefanana tu. Lakini hata hivyo kama anaamini ndiyo yeye basi ninajikuta kwenye utata. KUendelea na kumalizia au kujaribu kukibadilisha zaidi na kuruka simulizi la Jumamosi au kulibadilisha kabisa?

Naomba mpige kura kwa kuzingatia kiwango cha ukweli kilichomo ndani. Nataka nifikir uamuzi ifikapo J'pili ili kama kisa kitakuwa kimeisha niwaambia au kama ndio nikiposti kiishe niwapostie maana Jambo limezua Jambo!
 
AAAHHHHHHHHHHHHHHHHHHHHHH!!
Kwani kuna kisa ambacho ni cha kipekee hapa duniani? Maisha is just a big rehearsal and performance inafuata hahahah
Huyu Waziri au sijui mwanasiasa aanze mbele huko! SISI TUPATIE ILE KITU ROHO INATAKA..... HATA KAMA NI MAMA/BABA YANGU MZAZI MLIPUE TU!
 
Mmmh Mwanakijiji umeniacha hoi ...hee kumbe haya mambo yapo eeh?
Huo ni utunzi wako we endelea kutupa burudani,hadithi nyingi huwa ni mifano halisi iliyopo na inayoendelea kutokea
Gud Lucky
 
MMJ mambo kama hayo mbona yapo hata kama ni kiongozi gani yapo. We endelea tu kutupa uhondo wetu tujifunze na mambo mengine hususan ya ndoa kwa wale ambao bado hatujaingia anga hizo. haijalishi kama ni boss au nani yeye atulize tu.
 
Mpaka hapa hamna alisema usiendelee kwahiyoooo...tupe ile kitu roho inapenda!!:rofl:
 
Mwaga uhondo Mwanakijiji mwenzangu ikiwezekana toa kitabu kabisa ikishindikana mi naprint kopi zangu nikaweke kwenye ki maktaba changu hata junior wangu akikua akikute hichi kisa ili naye apate somo hapo.
 
haya mambo yapo na yataendelea kuwepo,huyo yaliyomkuta leo hatakuwa wa mwisho.
aandike kuumia,tupe burudani kama kawa
 
Mwanakijiji labda kwa akili tu za kawaida unadhani ni watu wangapi watakaosema usiendelee?hiyo Poll yako haina tofauti na zile za ITV zinazojua majibu lakini wanaendelea tu kuuliza.
 
Mwanakijiji ongeza; Asilimia 90 ukweli 10 Uongo- iendelee.

dhumuni ni kutuburudisha na kutuelimisha, kwa hivyo mi naona iendelee tu.
 
Mwanakijiji nadhani katika watu wa kwanza kuisoma na kuvutiwa moja kwa moja na kuichagiza kuwa usiiache kuandika hadithi hapa jukwaani mie ni mojawapo!

Maoni yangu ni kama ifuatavyo!

1. hadithi kama sehemu moja wapo ya fasihi inatumika kufundisha; hivyo iwavyo vyovyote lazima itachukua mifano halisia! sisi kama hadhira yako tunajifunza mengi humo na waliomo kwenye ndoa wataungana nami! Hivyo unao wajibu kwa hadhira yako!

2. Malipo ya dhambi ni mauti; ukisoma katikati ya mistari sio lazima ufe kwa maana ya kupoteza uhai; hata hayo majuto na machungu ndio sehemu ya malipo ya dhambi yako : Kwako MWANASIASA; Mwanakijiji hatekelezi hukumu yeye sio Mungu na wala hana nafasi ya ku-compromise nawe kuhusu hilo! jamii itamsuta na atakuwa ametenda dhambi kwa kutomalizia mafundisho yake; unapaswa ukamwombe Msamaha Mungu wako naye ndiye mwenye kukuponya na machungu yako utakapoupokea msamaha wa kweli na si kwa kuufunika uovu wako NO!

Mwanakijiji Kanyaga Twende mwanawane!
 
hadithi iendelee mi nilikuja kudownload chapter 6 ya jumamosi manake ndo fainali pale:drum:
 
hadithi iendelee mi nilikuja kudownload chapter 6 ya jumamosi manake ndo fainali pale:drum:

siamini kama wewe huwa unasoma hadithi ..inawezekana unaprint unapeleka kwa wife anasoma kisha anakusimulia...
 
Back
Top Bottom