Kiruka njia??

Dark City

JF-Expert Member
Oct 18, 2008
16,253
11,598
Naomba wana MMU mnijuvye...Hivi kiruka njia ni mtu wa namna gani??


Babu DC!!
 
Anaependa kuzurura sana....na wakati mwingine inatumika kumtambulisha mtu ambae ni mhuni (anaehama toka kwa mwanamke/mwanaume mmoja kwenda kwa mwingine kila mara).

Kwahiyo ni mtu asiyetulia sehemu moja iwe kimahusiano au kimazingira!!
 
BAbu yangu Kiruka njia nadhani ni mtu ambaye hajatulia, hashikiki, .............sijui kama mcharuko au mapepe vinawezatumika kwa mtu wa aina hii
 
Anaependa kuzurura sana....na wakati mwingine inatumika kumtambulisha mtu ambae ni mhuni (anaehama toka kwa mwanamke/mwanaume mmoja kwenda kwa mwingine kila mara).

Kwahiyo ni mtu asiyetulia sehemu moja iwe kimahusiano au kimazingira!!

Sawa Lizzy,

Cut-off ni watu wangapi mtu anatakiwa awe amewapitia au kuwa nao ili aitwe kiruka njia??
 
BAbu yangu Kiruka njia nadhani ni mtu ambaye hajatulia, hashikiki, .............sijui kama mcharuko au mapepe vinawezatumika kwa mtu wa aina hii

Una maana hilo neno halina mrengo wa jinsia i.e linatumika kwa ME na KE wote?
 
kuwa na mapepe... kutotulia... mcharuko.... fujo.... muhuni... mzurulaji..etc

May be..

Ila nimekutana na jambo ambalo limenifanya nipate msinyao wa ubongo..

Hivi mwanamume akio mke wa kwanza ila akakuta mama mwenyewe ni Tyson..kila siku baba hakosi vinundu usoni. Akaamua kubwaga manyanga na kumpata namba 2..huko nako akukana na moto wa aina nyingine...huyoooo akang'atuka kiaina na kupata namba 3....Labda bahati pia ikawa mbaya na huyo akawa si riziki!!

Au mdada wa watu ambaye ailiuvaa mkenge na kuolewa na jamaa mwenye wake 2 (yeye wa 3) kwa sababu hakumueleza ukweli...Baada ya vitimbi kibao naye akaamua kupanda dala dala ya 2...Hivyo hivyo hadi anafikia chuo cha 4 au 5 (married to 4 or 5 different men)!!!

Hawa watu wana-qualify kuitwa viruka njia???
 
May be..

Ila nimekutana na jambo ambalo limenifanya nipate msinyao wa ubongo..

Hivi mwanamume akio mke wa kwanza ila akakuta mama mwenyewe ni Tyson..kila siku baba hakosi vinundu usoni. Akaamua kubwaga manyanga na kumpata namba 2..huko nako akukana na moto wa aina nyingine...huyoooo akang'atuka kiaina na kupata namba 3....Labda bahati pia ikawa mbaya na huyo akawa si riziki!!

Au mdada wa watu ambaye ailiuvaa mkenge na kuolewa na jamaa mwenye wake 2 (yeye wa 3) kwa sababu hakumueleza ukweli...Baada ya vitimbi kibao naye akaamua kupanda dala dala ya 2...Hivyo hivyo hadi anafikia chuo cha 4 au 5 (married to 4 or 5 different men)!!!

Hawa watu wana-qualify kuitwa viruka njia???

Exactly.....!!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom