Kipindi usikuvu wa mwanasiasa

Radio Producer

JF-Expert Member
Feb 4, 2011
724
295
Habari ya wakati huu msikilizaji wangu! Karibu katika kipindi cjetu cha usikivu wa mwanasiasa! Hebu tuiangazie report hii ya EU! Ni mimi Producer karibuni!

DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com
press@ikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425


clip_image002.jpg

PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais Jakaya Mrisho Kikwete amesema ana matumaini kuwa Watanzania wengi zaidi watajitokeza kupiga kura katika uchaguzi mkuu ujao tofauti na uchaguzi mkuu uliopita, uliofanyika kote nchini tarehe 31, Octoba, 2010.
“Natumaini hali itakuwa tofauti kwa uchaguzi mkuu ujao ikizingatiwa kuwa pia kutakuwa na wagombea wapya, ” Rais amesema.
Rais Kikwete amesema hayo leo mchana mara baada ya kupokea taarifa ya uchaguzi iliyotolewa na Jumuiya ya Ulaya, iliyokabidhiwa kwake na Mwangalizi Mkuu wa Taasisi ya Uchaguzi ya Umoja wa Nchi za Ulaya, Bw. David Martin, katika Ikulu ya Dar-es-salaam.
Taarifa hiyo inasema kwa ujumla, Uchaguzi Mkuu wa Tanzania uliofanyika Oktoba 31, 2010 ulikua shwari na uliendeshwa kwa utaratibu mzuri.
Taarifa hiyo imeelezea kuwa idadi hiyo ndogo kwa Tanzania Bara inaweza kufafanuliwa kwa kutumia mchanganyiko wa sababu ambazo zifuatazo:
1. Hali ya watu kutojali pamoja na kuwa na imani kubwa kuwa CCM ingeshinda kwa vyovyote vile bila kujali ni idadi au ni kiasi gani cha wapiga kura ingejitokeza.
2. Upinzani kukosa uwezo wa kuwaridhisha wapiga kura,
3. Ukosefu wa shauku ya kupiga kura miongoni mwa watu katika nchi ambayo imekuwa ikitawaliwa na Chama kimoja cha Siasa.
4. Kipindi kirefu cha Kampeni ambacho kilitawaliwa mno na chama tawala.
5. Ukosefu wa elimu ya mpiga kura.
Kwa Upande wa Tanzania Visiwani, taarifa inasema wananchi wa visiwani walidumisha jadi yao ya kuwa na ushiriki mkubwa wa wapiga kura katika visiwa vya Pemba na Unguja.
Rais amesema anazijua changamoto na matatizo mbalimbali ambayo yanafanyiwa tathmini ya kutosha ili kurekebisha hali hiyo.
Rais pia amesisitiza kuwa ni vyema chaguzi za nchi zikaendeshwa kutokana na taratibu zilizopo kama zinavyoainishwa na Tume za Uchaguzi, na pia taratibu hizo zikazingatia mahitaji na matakwa ya nchi na wananchi wake wenyewe.

Imetolewa na Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi,
Ikulu
Dar es Salaam.
07 Februari, 2011



 
ripoti iko wapi au ndio hiyo taarifa kwa vyombo vya habari?........halafu hiyo Rais Msaidizi imekaaje?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom