Kipindi cha mapitio ya magazeti cha ITV hakina mvuto kabisa!

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
234
Kipindi cha mapitio cha magazeti kinachorushwa na kituo cha ITV asubuhi hakina mvuto kabisa na bora kisitishwe kwa ajili ya marekebisho.

Kwanza kabisa magazeti wanayopitia ni machache sana, mengi yakiwa ya IPP Media yenyewe. Isitoshe kuna ubaguzi sana kwani magazeti kama Mwananchi, Citizen na yale ya New Habari Corp hayasomwi kabisa. Hali kadhalika Mwanahalisi siku zote huwa halipitiwi.

Mpitia magazeti Raifred Masakao hana mvuto kabisa -- anaongea sana maneno yasiyokuwa na maana.

Halafu magazeti yanayopitiwa hayaonwi na watazamaji kurasa zake za mbele maana mpitiaji akisha soma vichwa vya habari huliweka pembeni, au hulionyesha kwa mbali ambapo mtazamaji hawezi kusoma vichwa vya habari vingine vilivyopo.

Hii ni tofauti sana na kipindi cha mapitio ya magazeti cha Ch Ten ambapo mpitiaji husoma vichwa vya habari huku ukurasa wote wa mbele unaonyeshwa kwa watazamaji.

Hongera sana Ch Ten kwa kipindi chenu cha mapitio ya magazeti.
 
Mimi navutiwa sana na Start TV lakini nao of recent wana matatizo na kujiunga na dar kiasi kwamba huna uhakika wa kuwapata siku nyingine wanaishia kuweka vipipndi vingine kabisa bila hata kutujulisha na kuomba radhi kwa badiliko hivyo inakuwa kubahatisha. ITV nimeacha kuangalia wanaboa waache hakina maana.
 
halafu inakera mtu anapopitia gazeti la kingereza na kutoa tafsiri potofu!
 
Sawa usemayo. tatizo wabongo hatujifunzi kutoka kwa wenzetu au hata jirani. Wao wameshikilia yaleyale ya jadi hawabadiliki kuendana na nyakati.
 
Jamani huo ndio mkakati maalum wa ccm, kupitia kwa waziri wa habari ( Dr Nchimbi) ameanda mkakati malum wa kuzuia magazeti mengine kuwafikia wananchi, mkakati huo sio ITV pekeeeee, sikiliza Clouds Fm ndio kichefuchefu kabisa, siasa za Tanzania hizo................
 
ITV kwa ujumla hakuna kitu cha kuvutia. Ni bora hata mapitio ya magazeti,taarifa ya habari ndo haina mvuto kabisa utafikiri ni televisheni ya taifa siku hizi baada ya mhando kuondoka na kabla yake!

Clauds wamerambishwa hamna kitu pale wanatumikia matumbo tu amebaki Gerald lakini naye anazidiwa nguvu saa nyingine anajiumuma maneno tu.

Star tv afadhari na channel ten lakini kipindi cha wakuhenga sikipendi maana hujifanya kama ndo mwenye busara sana eti juzi anasema hakuna mwenyeuwezo wa kuiondoa serikali madarakani kasahau hata nguvu ya umma.
 
Suala la magazet sio itv pekee..clouds wanaboa sana sijui wana matatizo gani...utakuta habari leo,mtanzania,uhuru na rai halafu wanasifia eti rai wanaandika habari za uchunguzi upuuzi mtupu.....
 
Mimi navutiwa sana na Start TV lakini nao of recent wana matatizo na kujiunga na dar kiasi kwamba huna uhakika wa kuwapata siku nyingine wanaishia kuweka vipipndi vingine kabisa bila hata kutujulisha na kuomba radhi kwa badiliko hivyo inakuwa kubahatisha. ITV nimeacha kuangalia wanaboa waache hakina maana.
Mimi ombi langu ITV wampe masako vipindi vingine kuliko kusoma magazeti yaani Hana mvuto kabisa watu wengi wanalalamika kwa ajili yake au ITV waache kabisa kusoma magazeti.
 
Tatizo lenu mnataka msomewe habari zote za magazeti kwenye mapitio. Maiptio lengo lake ni kuwapa vichwa vya magazeti yaliyoifikia TV station. Sasa mnataka wasome magazeti ambayo hawana? Mimi sioni tatizo na choice ya ITV na kuyaacha magazeti ya Habari Corporation ( kama wanafanya hivyo kwa makusudi) kwa sababu kwanza magazeti yenyewe hayana mvuto. isitoshe, hata mmiliki wa magazeti hayo angefanya the same kwa magazeti ya IPP. Staili hii ya upitiaji wa magazeti hata Sky TV na BBC hufanya hivyo hivyo. Suala la mvuto wa mtangazaji hilo ni muono wa mtu binafsi. Wakati wewe unasema Masako hana mvuto, wako wanaokufa kumsubiri yeye asome habari hizo.
 
Kwangu mimi tatizo ni kubwa na pana zaidi ya kipindi hicho kimoja cha mapitio ya magazeti ITV. Utoaji mzima wa habari umejikita kwenye kutoa taarifa tu bila uchambuzi yakinifu. Ebu angalia vyombo vyetu vingi vya habari nchini, hasa magazeti ya jana na leo yalivyo 'copy and ku-paste' habari za mauaji ya Osama kutoka kwenye vyombo vya habari vya magharibi. Halafu angalia wanavyotoa habari kwa uhakika! Utadhani walikuwa na Obama chumba kimoja wakiangalia jinsi hiyo operesheni ilivyokwenda! na magazeti mengine yana ukakika zaidi na kilichojiri kuliko hata wale walioshiriki kwenye operesheni, maana hata wao maelezo yao yanajikanganya na hawatoi majibu kwa maswali mengine mpaka waende kujadili, kitu ambacho ni cha ajabu hasa kama operesheni nzima imeshuhudiwa. Kwa hiyo mbali na ushahabiki wa ki-siasa, vyombo vya habari vina hilo tatizo, na suluhisho lake sio kuwalaumu akina Masako au waandishi wa habari kwa ujumla bali ni sisi wadau wa habari kuvisaidia vyombo vya habari kuliangalia hilo tatizo na kulishughulikia ili ndani ya vyombo vya habari kuwe na hulka ya kuuliza maswali mengi na kutilia mashaka mambo mengi zaidi kuliko ilivyo sasa. Wakifanya hivyo watakuwa wamelisaidia sana taifa hili.
 
Tatizo lenu mnataka msomewe habari zote za magazeti kwenye mapitio. Maiptio lengo lake ni kuwapa vichwa vya magazeti yaliyoifikia TV station. Sasa mnataka wasome magazeti ambayo hawana? Mimi sioni tatizo na choice ya ITV na kuyaacha magazeti ya Habari Corporation ( kama wanafanya hivyo kwa makusudi) kwa sababu kwanza magazeti yenyewe hayana mvuto. isitoshe, hata mmiliki wa magazeti hayo angefanya the same kwa magazeti ya IPP. Staili hii ya upitiaji wa magazeti hata Sky TV na BBC hufanya hivyo hivyo. Suala la mvuto wa mtangazaji hilo ni muono wa mtu binafsi. Wakati wewe unasema Masako hana mvuto, wako wanaokufa kumsubiri yeye asome habari hizo.
Mkuu kama uko ITV kubali kukosolewa, kipindi chenu cha magazeti afadhali hata cha TBC.
Ni heri mgekifuta kabisa.
Siku hizi mimi nasikiliza redio MAGIC FM ambayo haichambui lakini unapata mwelekeo wa habari kamili iliyoandikwa.
Mgekuwa objective katika kipindi hiki angewekwa mtu mahiri zaidi wa kucomment kwa hizo habari na mapokeo yake na jamii kwa ujumla.
BBC huwezi kujilinganisha nayo nyie bado bwana.
 
Japo mwondoeni masako ktk mapitio ya magazeti na utaratibu wa usomaji uendelee kama mnavotaka. Hamwoni kuwa hamumtendei ipasavyo? Mpaka babu wa watu anajilazimisha kusoma kumbe bado anaimba tu!! Sote tunjajua Masako ananoga ktk vipindi vya namna ipi, na ITV mnavyo vingi si haba!
 
TBC1 leo wamesoma gazeti la Tanzania Daima la Jana ,ITV walikuwa na magazeti 3 kampuni inayoheshimmika kimataifa inawanyima watazamaji wake kwa uchoyo wa kusoma magazeti mengine eti watawanufaisha kibiashara kila siku lazima waanze kwa kusoma NIPASHE halafu UHURU na mwisho The guardian what a shame,kipindi hicho wakifute kabisa hawana maana aibu tupu,wakati Mengi ni mwenyekiti wa MOAT
Heko kwa Channel Ten na Star TV hawa wako neutral sana japo kuna wasomaji ambao kwa ukereketwa utashangaa habari zinazohusu vyama fulani huziruka lakini mtazamaji unaweza kuona kwenye display
 
Back
Top Bottom