Je, kipimo cha full blood pictures kinajumuisha vipimo vyote pamoja na Ukimwi?

Full blood picture ni kipimo kinachotumika kuelezea hali ya damu kwa ujumla wake hasa pale ugonjwa unapokuwa hauna chanzo kamili au unapokuwa na vyanzo vingi vinavyoingiliana. Humsaidia daktari kupunguza wigo wa kutafuta chanzo.

Damu inatengenezwa na Red blood cells, white blood cells na platelets ambazo kila kimoja kina kazi yake. Mfano red blood cells ni kwa ajili ya kubeba Oxyegen( Haem= Iron, globulin= protein).
White cells zimegawanyika katika makundi zaidi kama neutralphil, aesinophils, lymphocytes n.k. Kila kimoja katika kundi hili kinajihusisha na ulinzi wa mwili na kinapambana na wadudu maalum kwa mfano bacteria, virus, fungus, protozoa n.k.

Daktari anapoona wingi au upungufu wa kimoja katika hivyo hujikita zaidi kutafuta nini chanzo. Kwa mfano kuna magonjwa yanayoathiri lymphocytes tu na hapa daktari atajikita kufahamu kwanini mgonjwa ana lymphocytes nyingi kuliko au chache kuliko na tayari anakuwa anajua ni magonjwa gani yanayoweza kuleta hali hiyo na atakuwa amepunguza wigo mkubwa wa kutafuta kila kitu.

FBP haionyeshi wadudu bali ina suggest ni tatizo gani na limesababishwa na nini. Kwa mfano kuna cells zinaweza kuonekana katika hali isiyo ya kawaida lakini hazitokani na bacteria, virus au fungu bali inaweza kuwa ni auto immunity au vitu kama cancer. Isijeeleweka kuwa FBP inaonyesha ugonjwa halisi, hapana inatoa mwelekeo wa tatizo lilipo.

Baada ya kupata uelekeko Daktari anaweza kukuagiza kwenye kipimo halisi kinachohusiana na ugonjwa huo. Mfano akiona cells flani kama lymphocytes si za kawaida anaweza kukueleza ukapime makohozi. Kipimo kikirudi na kitu kama TB atajua una backeria wa TB. Atarudi kwenye FBP na kuangalia cells za immunity zipo sawa? akiona zina mushkeli atakuagiza ukapime kile kipimo cha hofu (HIV)

Huko wataangalia cells za immunity yako ndipo wanaweza kutoa majibu kuwa mambo nia aje.

Kwakuwa FBP inaangalia damu kwa ujumla basi hata red blood cells zinaweza kutoa mwelekeo. Mfano kama ni chache au nyingi atakuagiza ukapime Haemoglobin level ili kujua una damu kiasi gani au una tatizo gani linalosababisha ongezeko la damu au kwanini red blood cells haziko sawa.
Mfano kama ni haemogloni ni chache unaweza kuwa na upungufu wa damu(anemia) na hapo atajiuliza kwanini una anemia. Inaweza kuwa ni malaria na atakuagiza ukapime malaria, au zaweza kuwa zina umbo lislo la kawaida (sickle shape) hapo utakuwa na sickle cell.

Kwa ufupi ni kipimo kinachotoa mwonekano wa damu kwa ujumla wake ili kujua wapi pa kuelekeza nguvu.Mfano rahisi wa mtaani (msicheke) unapooona nyumba inafuka moshi kitu cha kwanza ni kufungua mlango ili ujue nini kinaungua (hapa unatafuta Full house picture). Ukisikia harufu ya mahindi utajua tatizo linaweza kuwa jikoni, ukisikia perfume utajua chumbani, ukisikia mbaya utajua chooni na ukisikia plastic utajua ni chumbani hasa kwa watoto kwenye ma-toy. Hapo itakupunguzi muda wa kuanza kufunua kila kila kitu bali utakwenda moja kwa moja kule unakojua harufu inapoweza kuwa inatokea.

senti sumuni.
 
Halafu madaktari wanapenda hicho kipimo jamani, yaani ukienda nakihoma lazima wakuandia FBP............. Wananiudhi sana. Na vile sipendi sindano, sichelewi kugaili na kwenda famasi kununua dawa mseto.
 
Full Blood Picture (FBP)...au kwa kitaalam zaidi inaitwa Full Blood Count (FBC) au Complete Blood Count (CBC) ni kipimo cha damu ambacho majibu yake yanaonyesha mgawanyiko au kiasi cha seli (cells) mbali mbali kwenye damu. The Idea is, mtu unapokuwa mgonjwa...

Riwa umeeleza vizuri nyongeza kidogo Full blood Count(FBC) vile vile inaweza kusaidia kugundua matatizo ya watu ambao wanamatatizo ya kutokwa na damu kunakosababishwa na kuchelewa kugandisha damu, hii husababishwa na upungufu wa chembe sahani (thrombocytopenia) ambazo pia kiasi chake hupimwa kwenye FBC.

Pia magonjwa ya kansa ya damu (lukemia) inaweza ikahisiwa kutokana na matokeo ya FBC, kama kipimo kikionyesha chembe hai za damu zitakuwa nyingi kuliko kawaida (hasa chembe nyeupe - white blood cells - leucocytes) hii inaweza kuonyesha uwezekano wa kansa ya damu (leukemia) . Lakini kama alivyosema Riwa hivi vipimo sio confirmatory, itabidi ufanyiwe vipimo vingine vya kucomfirm. The Boss....Msisitizo... hiki (FBC) sio kipimo cha HIV.
 
Nakushukuru sana pamoja na ugumu lkn umejitahidi tumekuelewa
Full blood picture ni kipimo kinachoonyesha hali ya damu, yaani kama kwenye damu kuna mapungufu/matatizo. Kunapimwa: haemoglobin (HB) level (yaani uwingi wa damu), uwingi wa red blood cells, uwingi wa white blood cells kwa jumla na aina mbalimbali. Kipimo cha HIV hakimo...

In God we Trust
 
Asante sana
Full blood picture ni kipimo kinachotumika kuelezea hali ya damu kwa ujumla wake hasa pale ugonjwa unapokuwa hauna chanzo kamili au unapokuwa na vyanzo vingi vinavyoingiliana. Humsaidia daktari kupunguza wigo wa kutafuta chanzo...

In God we Trust
 
Nimeenda kupima FBP nimeambiwa kila kitu kiko sawa. Je kuna haja ya kupima HIV?
Ndio ipo haja ya kupima HIV, kwa sababu unaweza kuwa na maambukizi ya HIV huku mwili wako ukiwa na kinga nyingi na kipimo cha FBP kinaweza kisibaini viashiria vya wewe kuwa na Viral infection.
 
Ndio ipo haja ya kupima HIV, kwa sababu unaweza kuwa na maambukizi ya HIV huku mwili wako ukiwa na kinga nyingi na kipimo cha FBP kinaweza kisibaini viashiria vya wewe kuwa na Viral infection.

Tatizo naogopa. Kuna mtu nishawah kufanya nae mapenzi mwaka jana 2019 hatukutumia condom halafu nikaja gundua mienendo yake ni hatarishi.
 
Tatizo naogopa. Kuna mtu nishawah kufanya nae mapenzi mwaka jana 2019 hatukutumia condom halafu nikaja gundua mienendo yake ni hatarishi.
Aisee!. Unajipa hofu ya kupima tu mwaka mzima!. Sikuhizi watu tunaogopa Corona na Sio HIV, nenda ukapime na si ajabu uko safi na hata Corona ikikutana na wewe haitakupa shida utapona vizuri tu.

Kupima na Kujua Afya yako ni jambo jema sana itakufanya uwe huru na kukufanya uwe na misimamo ya kujilinda zaidi.
 
Full blood count (FBC)
1. This is a test to check the types and numbers of cells in your blood, including redblood cells, white blood cells and platelets. This can help give an indication of your general health, as well as provide important clues about certain health problems you may have.

2. A routine complete blood count (CBC) test checks for levels of 10 different components of every major cell in your blood: white blood cells, red blood cells, and platelets. Important components measured by this test include red blood cell count, hemoglobin, and hematocrit.

3. The use of the full blood count and differential parameters to assess immune activation levels in asymptomatic, untreated HIV infection, Immune activation status is not routinely tested in HIV infection.
 
Join nowSign in
Silvanus Kidesi
Expand search


FAHAMU KIPIMO CHA FULL BLOOD PICTURE Na Silvanus Kidesi

FAHAMU KIPIMO CHA FULL BLOOD PICTURE Na Silvanus Kidesi​


Silvanus Kidesi
Silvanus Kidesi

Silvanus Kidesi​

Is a Medical Student @kcmucotz,MD…​

Published Jun 14, 2022
+ Follow

JE KIPIMO CHA FULL BLOOD PICTURE KINAHUSU NINI?​

Ni kipimo cha maabara kinachohitaji sampuli ya damu pale wataalamu na watabibu wanapohitaji kufahamu idadi ya seli zilizopo kwenye damu.

AINA ZA SELI KWENYE DAMU

SELI NYEKUNDU (RED BLOOD CELLS) :

No alt text provided for this image

Hizi ndizo hubeba oksijeni kwenye damu, kwa kutumia protini zake maalum zifahamikazo kama Haemoglobin. Jambo la muhimu ni uwepo wa chembechembe hizi za damu katika kwa idadi inayoleta uwiano unaohitajika na sehemu ya majimaji au ya damu (plasma).
Kuufahamu huu uwiano ndio Hematokriti (Hematocrit) huweza kufahamika. Hivyo kipimo hiki cha FULL BLOOD PICTURE kinaweza kusaidia kufahamu idadi ya seli nyekundu na uwiano wake na sehemu ya majimaji ya damu. Uwiano huu ndio utatujulisha kuwa damu ipo ya kutosha au la.
Seli nyekundu zinaweza kuwa hai (life span) hadi siku 120 yaani miezi minne,zikibeba hewa na kusaidia mfumo wa upumuaji.
IDADI
Wanaume huwa na idadi nyingi ya seli hizi kulinganisha na wanawake. Wingi wa seli hizi hupimwa kwa vipimo vya mamilioni kwa mili-lita kwani katika mili-lita moja ya damu zipo mamilioni ya seli nyekundu, yaani, zipo Milion 4.20 hadi Milion 5.8 kwa wanume, wanawake wakiwa na Millioni 3.8 hadi 5.20 kwa Kipimo mraba cha Mililita moja ya damu (m/ul)
UPUNGUFU WA DAMU

Hutambulika paale tu Protini zinazobeba oksijeni zinakuwa ndogo,Hupimwa kwa idadi ya uzito unaopatikana kwa sehemu ya kumi 1/10 ya damu g/dl. Huku wanaume wakiwa na kiwango cha gramu 13 hadi 17 na wanawake gramu 11 hadi 15. upungufu wa viwango hivi huashiria upungufu wa damu (ANEMIA) na wingi wa viwango hivi huashiria wingi au ongezeko la damu Primary Erythrocytosis (Polycythemia vera). Na wingi wa damu unapokua wa muda mrefu huwa ni changamoto ya magonjwa ya moyo (heart diseases, chronic hypoxia, COPD) au watu wanaoishi katika milima (High altitude) ama kuzaliwa na hii hali (malignancy elevated erythropoietin)
SELI NYEUPE (WHITE BLOOD CELLS) :
No alt text provided for this image

Zenyewe hupambana na maambukizi. Ni muhimu kufahamu idadi ya seli nyeupe za damu kwani zinaweza kuonesha wingi usio wa kawaida zinapopambana na maambukizi. Kipimo cha FULL BLOOD PICTURE kitamsaidia mtaalamu kujua kuwa una maambukizi kwa kuona idadi ya seli nyeupe isio ya kawaida. Mara nyingi huonekana katika hali mbalimbali mfano ni kansa ya damu (LEUKEMIA) Hivyo kipimo hiki kinaweza kutoa taarifa ya msingi endapo mtu anaweza pata kansa ya damu.
Seli nyeupe zinapambana na magonjwa kwa kuvamia Bacteria, Virusi (Virus) na vijidudu (germs) mbalimbali vinavyoweza leta maambukizi. Seli hizi zinaweza fanya kazi yake hadi siku 13 wakati mwingine siku 20 kutegemeana na muda zitakapofika kwenye mfumo wa Limfu (lymfatic system) ambapo zitaweza kuharibiwa ili nyingine kuzalishwa.
IDADI
Tofauti katika vipimo vya idadi ni kwamba seli nyekundu hupimwa kwa vipimo vya mamilioni ndani ya mili-lita mraba (m/ul), wakati seli nyeupe hupimwa kwa vipimo vya maelfu ndani ya mili-lita mraba yaani (k/ul). Seli hizi zinafahamika kuwa maelfu tatu hadi maelfukumi, yaani 3.5-10.5x 10^9 K/ul kila mraba wa mili-lita moja ya damu.
Zikiwa katika aina yake ongezeko la seli hizi huashiria aina ya vijidudu vinavyopelekea maambukizi, endapo kuna ongezeko la seli nyeupe aina ya Neutrophil basi inaashiria kuna maambukizi yanayoletwa na vijidudu kama ( bacteria, hali ya kuunguzwa, hali ya uvimbe (inflamation), maambukizi yanayoletwa na uvutaji wa sigara, matumizi ya baadhi madawa (cortocosteroids), kansa ya damu.) na upungufu waaina hii ya seli nyeupe huitwa Neutropenia, inaweza sababishwa na kuzalishwa kwa uchache, madhara ya madawa, au maambukizi ya muda mrefu.
Aina nyingine ya seli nyeupe ni Eosinophili, ongezeko la seli hizi huashiria maambukizi ya vimelea (parasite), hali ya aleji (allergies), aina ya uvimbe kwenye kuta za mishipa ya damu (vasculitis), huku upungufu wa seli hizi huashiria changamoto mbalimbali za mfumo wa kinga ya mwili kama vile sepsis inayoweza pelekea mwili mzima kuwa katika hali ya uvimbe.
Aina nyingine ni lymhocytes, ongezeko la seli nyeupe hizi huashiria maambukizi yanayoletwa na virusi, na huwa zinapanda juu kwa wagonjwa wa UKIMWI (HIV), EBV,CMV.. lakini pia upungufu wake unaweza sababishwa na maambukizi hayohayo ya virusi au matumizi ya madawa.
Aina nyingine huitwa Monocyte idadi ya seli nyeupe hizi huongezeka wakati wa ujauzito (pregnency), au wagonjwa wa TB (Tuberculosis) au syphilis na sarcoids., na upungufu huashiria kansa ya damu ama maambukizi ya ghafla.
PLATELETS:
No alt text provided for this image

Zenyewe ni chembechembe seli za damu zinazosaidia damu kuganda. Chembe chembe hizi ni ndogo mara tano kulinganisha na seli nyekundu , na zinaweza kuwa hai zikisaidia damu kuganda kwa siku 8 hadi 9 kisha zife na nyingine zizalishwe.
IDADI
Seli hizi kama seli nyeupe hupimwa kwa viwango vya maelfu yaani K/ul zikiwa seli 150 hadi 400 kwa idadi. Ongezeko la seli hizi (Thrombocytosis) huashiria upungufu wa damu unaosababishwa na upungufu wa madini chumvi, wengu kuharibika au kutolewa (splenectomy), wakati upungufu wa seli hizi huashiria upotefu wa damu (blood loss), uvimbe katika wengu (spleenomegaly), maambukizi ya virusi (viral infections), madawa au magonjwa ya mifupa (bone marrow disorders), na kansa ya damu (leukemia)
CHUPA INAYOTUMIKA KUKUSANYIA DAMU KWA AJILI YA KIPIMO CHA FULL BLLOD PICTURE
No alt text provided for this image

Damu hukusanywa kwenye chupa mbalimbali kulingana na mahitaji ya mtaalamu. Kuna vichupa mbalimbali (TUBES) vinavyotumika maabara vikitofautishwa kwa rangi zake kuanzia (nyeusi,bluu, dhambarau,nyekundu,kijivu,njano mpauko na kijani), kukusanyia damu kwa ajili ya Kipimo cha FULL BLLOD PICTURE hutumiwa chupa ya rangi ya dhambarau (Purpe Test Tube)
Kwa matibabu ya magonjwa ya damu, ushauri na maswali wasiliana nasi kwa namba +255 744 798 312 au barua pepe : silvanuskides@gmail.com.
 
Full blood picture ni kipimo kinachoonyesha hali ya damu, yaani kama kwenye damu kuna mapungufu/matatizo. Kunapimwa: haemoglobin (HB) level (yaani uwingi wa damu), uwingi wa red blood cells, uwingi wa white blood cells kwa jumla na aina mbalimbali.

Kipimo cha HIV hakimo. Ni kipimo cha jumla sana kwa sababu hakilengi ugonjwa wowote. Kama majibu yake hayatakuwa normal, itamaanisha kuwa mgonjwa ana tatizo la kiafya, lkn haitajulikana moja kwa moja ni tatizo gani. Vipimo vingine itabidi vifanywe ili kujua aina ya tatizo/ugonjwa.

Nadhani nimeeleweka, japo kidogo. Ni vigumu sana kufafanua mambo ya medicine kwa lugha ambayo kila mtu ataelewa
Jiamini na kwamba maelezo yako ni perfect.
Umeelezea kwa summary vizur sana ambavyo kila mtu lazima akuelewe.
 
Wataalam

Ningependa kujua kwa undani maana ya hiki kipimo cha full blood picture

Kinahusu vipimo vyote vya damu? including HIV?
Au ni vipi?

Je, kinamsaidia dokta kupata picha ya magonjwa mengine kabla ya kupima?
FBP inaweza kutoa mwanga kuhusu kinga yako ya mwili. Kama itaonesha kinga ipo chini sana daktari anaweza kukushauri ufanye kipimo cha HIV ili kufahamu chanzo cha kinga zako kushuka.

Lakini ukumbuke sio HIV tu inayoshusha kinga. Baadhi ya magonjwa kama pumu na kansa yanaweza kushusha kinga pia.

Kwa hiyo kama kinga zipo chini, usiogope sana mkuu.
 
Full Blood Picture (FBP)...au kwa kitaalam zaidi inaitwa Full Blood Count (FBC) au Complete Blood Count (CBC) ni kipimo cha damu ambacho majibu yake yanaonyesha mgawanyiko au kiasi cha seli (cells) mbali mbali kwenye damu.

The Idea is, mtu unapokuwa mgonjwa...mwili wako unarespond au kureact kwa kile kinachosababisha ugonjwa huo, mara nyingi kwa kutumia seli (cell mediated immunity) au chachu kama antibodies (Humoral immunity) kushambulia hicho chanzo cha ugonjwa mfano bacteria, virus etc.

Sasa FBP/FBC/CBC inaangalia mabadiliko ya seli katika damu ili kuweza kupata idea (sio kuconfirm) kama kuna infection, na kama ipo basi labda ni ya asili gani (mara nyingi seli zinazorespond kwa bacterial infection ni tofauti na za viral infection)...zaidi ya kutoa mgawanyo wa seli, test hiyo pia hutoa kiasi na size (in volume) ya seli nyekundu hivyo kutoa idea kwa wagonjwa wenye upungufu wa damu basi unaweza kuwa upungufu wa aina gani (microcytic/megaloblastic anaemia) ambao unaweza kusaidia kutambua aina tofauti za upungufu wa damu.

Kwenye ile fomu ya majibu, mgawanyiko/kiasi cha seli kwenye damu ya mgonjwa hulinganishwa na viwango standard (normal range) ambapo ukilinganisha unaweza jua kuwa viwango vimeongezeka au kupungua kutoka kwenye normal range. Pia kwa wataalamu waliobobea kwenye mambo ya damu wanaweza soma zile graphical presentation ili kuona mengi tu.

LAKINI: FBP/FBC/CBC haitoi majibu ya HIV. Test ya HIV inapima antibodies (Humoral), japo kuna madaktari kwa kuangalia mgawanyiko wa seli anaweza akahisi unaweza kuwa na chronic illness (kuna cells hasa Lymphocytes) huwa zinabadilika mganyiko wake kwenye damu kama mgonjwa ana ugonjwa sugu including HIV and TB. Hivyo Dr anaweza kutumia majibu ya FBP kukushauri ukafanye kipimo cha HIV ili kuthibitisha.
Mkuu umemaliza kila kitu. Uzi ufungwe.
 
Back
Top Bottom