Ninaendelea kukiangalia. Taabu ni kwamba watayarishaji hawana habari kabisa kwamba tatizo bungeni ni suala la Kanuni. Mijadala kama hii hawa ITV walitakiwa ku-dowload Kanuni za Bunge ndiyo ziwe nguzo ya mjadala. Hapa hakuna hata mmoja mwenye kanuni wala anayetaja kanuni. Hawa nao ni tatizo.
Kuna watu wanataka kujenga chama pale kilicho kibovu.
Hata asiyejua miongozo anajua kuwa kuna shida. Kiti cha spika kinatekeleza maslahi ya chama. Kiti hicho kiwe kwa mtu asiye mwanachama wa chama chochote. Katiba mpya ifanye hilo badiliko.
Mwanaharakati mmoja kachangia vizuri sana. Bahati baya sikuweza kulinukuu jina lake lakini ni mwana-Mama.
Anasema ndani ya Bunge hakuna mazingira ya kutendeka haki maana Mawaziri ni Wabunge na wamekaa mle mle Bungeni, Spika ni Mbunge na Naibu wake na wa chama hicho hicho kimoja, unategemea haki itendeke kweli? Kwahiyo ametumia fursa hiyo kukumbusha Watanzania kutumia fursa hii ya kujadili Katiba ili haya mambo yapate kurekebishwa na Katiba mpya.
Mchango wake huyu Mama ulikuwa makini sana.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.