Kina mama wenye watoto daima wanaitwa kwa majina ya watoto wao, mf. kama mtoto wake anaitwa "Mfaume" basi mama yake ataitwa "Mama Mfaume". Miaka ya karibuni - kama sikosei - kina mama wamekuwa wakiitwa kwa majina ya waume zao pia. Mfano utasikia "Mama Kikwete" wakimaanisha mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Swali 1. Kiswahili kipi ni sahihi kati ya misimamo hiyo miwili hapo juu?
Swali 2: Kwa nini kina baba wanaitwa kwa majina ya watoto wao tu na si ya wake zao? Mf. utasikia "Baba Mfaume" lakini si "baba . . . (likitajwa jina la mkewe)?
Swali 1. Kiswahili kipi ni sahihi kati ya misimamo hiyo miwili hapo juu?
Swali 2: Kwa nini kina baba wanaitwa kwa majina ya watoto wao tu na si ya wake zao? Mf. utasikia "Baba Mfaume" lakini si "baba . . . (likitajwa jina la mkewe)?