Kiongozi wa makarani wa sensa ashughulikiwa

Hapa ndipo tunapotofautiana. Kazi nyingine tunaambiwa tutangulize utaifa mbele, wakati wengine wanatakiwa watangulize maslahi mbele. Juzi wabunge wamapewa 1Milioni kila mmoja kwa ajili ya kuhamasisha sensa, wakati ambapo wabunge haohao hadi sasa tangu wamalize kikao cha bunge, wamebana huko mijini, na huku majimboni hawajafika. Hiyo milioni waliyopewa haijafanyiwa kazi, na wala haitarejeshwa. wakati huohuo, karani analazimishwa aende kituoni bila kulipwa, eti atangulize utaifa, akale nini huko????, akalale wapi????, akafanye nini????. Hivi utaifa ni kutesana????
Tunaambiwa eti Ualimu ni kazi ya wito, Udaktari ni kazi ya wito, je! ubunge si kazi ya wito??????? Tuache siasa, tufanye kazi.
Ndugu yangu Mangaline, kama umeona post nyingi za juu hapo wapumbavu wakubwa wamefurahia huyu jamaa kunyimwa alichokuwa anadai.

Huyo alijitolea kuongoza wenzie kudai haki amekatwa jina, na wengine wamelipwa kupitia mgongo wake wapumbavu wengine wanalifurahia hilo, ndio uone ni aina gani ya mijitu mijinga imejaa huku uraiani, yaani hatuwezi kutoka kwa kuwa na wapuuzi kama hawa wasioelewa nini maana ya kudai stahiki zao!
 
Wamechakachuliwa pesa za nauli za semina siku 11,pesa za kwenda vituoni kabla ya siku ya sensa.pia mratibu ameeleza kukosekana kwa mavazi. Maalumu ya sensa.

Mkuu huku kwetu hiyo hela ya nauli mpaka muda huu hakuna cha NAULI (ya kwenda na kurudi kwenye semina), hakuna MABEGI, T.SHIRT, VITAMBULISHO, NA MADODOSO yaliyopo ni nusu ya kila EA, pia hakuna vibao, penseli na makarani mpaka sasa wanajiuliza sijui waanzie wapi! Suala nafikiri ni nchi nzima vifaa haviko kamili.
 
Aiseeee babaangu hapa nimeshaona dalili ya kuambiwa watanzania wapo m 25 wangi wamekufa

ngoja nipate mbege mie
 
Tuambie ni vituo vya wap na wapi,maana kama mimi kituo changu ni Iyunga na nimepewe kilakitu pamoja na makarani wengine.
 
sijui kwa nini watanzania ni maskini na sijui watanzania wako wangapi!
 
Nimepata habari za kuaminika kutoka kwa rafiki yangu ambaye naye ni karani wa sensa hapa DSM kuwa yule kiongozi wao aliyeonekana kupitia tv mbalimbali(kijana mnene mweupe hv) akisisitiza serikali kuwalipa pesa yao yote ya semina ya siku saba jina lake limekatwa,na sasa hajapangiwa kituo na hajaripwa posho ya ukarani wa sensa.

mytake:Hawa makarani wanapaswa kutanguliza utaifa mbele na sio maslahi yao,wakumbuke walimu na madaktari n.k wote wako kazini kwa kutanguliza uzalendo
Wizi mtupu, wacheni kuonea watu, hiyo ni haki yake. Wezi wakubwa kabisa.
 
Hivi na wale watakao lala Club watahesabiwa Wapi? au kuna utaratibu wowote utakao fanywa?
 
iringa wamepewa vifaa nusu hakuna vitambulisho,kofia ,wala tshirt kwa ajili ya makarani .jk maskini yeye anawaza kwenda msibani Ethiopia na huku nyumbani mambo hayapo sawa.kweli serikali yetu imekurupuka kufanya hii sensa.

Takwimu hazitakuwa sahihi hata kidogo.Pole yetu watanzania kwa kuwa na serikali kama ya ccm
 
Hahaha! Hivi Mukulu kaenda msibani tayari ama anangoja kuhesabiwa? Aisee, chadema watakuwa wame-subbotage vifaa vya cancer (I mean sensa). Imefikia mahali priority ni polisi, manake wamejisifia wako kamili gado utasema tuko south sudan!
 
iringa wamepewa vifaa nusu hakuna vitambulisho,kofia ,wala tshirt kwa ajili ya makarani .jk maskini yeye anawaza kwenda msibani Ethiopia na huku nyumbani mambo hayapo sawa.kweli serikali yetu imekurupuka kufanya hii sensa.Takwimu hazitakuwa sahihi hata kidogo.Pole yetu watanzania kwa kuwa na serikali kama ya ccm

Watavaa t shirt na kofia za ccm
 
Back
Top Bottom