Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana...

hivi tumefikia hatua ya kuidharau mahakama! nchi tunaipeleka wapi? kama kakamatwa na vyombo vya dola kwa kuidharau mahakama, hilo ni jambo la kawaida.
 
Huyo hana maana kabisa serikali imemsomesha ili asaidie jamii yeye kaweka maslahi yake binafsi kwanza kuua watanzania waliomsomesha kwa kodi zao ni kosa kubwa sana,fanya kazi kwa bidii upate fedha, siyo kushawishi na wenzako wagome Hehehee! ili tufe? tena kwa maslahi binafsi!

Haiwezekani anataka utajiri bila kufanyia kazi,mtu mbaya kabisa aliyejitokeza TZ karne hii ya 21 ni huyu,serkali ilishakubali kuwa yanazungumzika kuwa na subira wakati yakitekelezwa siyo kulazimisha tena kwa kusababisha vifo vya wagonjwa huu siyo udaktari ni uhujumu tena mbaya kuliko ukimwi,ingelikuwa China leo hii asingekuwepo duniani,nashauri hivyo mbona kina Kombe,Mahiza e.t.c hawapo na nchi inaendelea.
 
Unajuwa ndani ya nchi kuna vyombo vingi vya usalama.vingine vinafanya kazi waziwazi na vinajulikana kwa watu.vingine vinafanya kazi kwa kificho na havitakiwi kujulikana na ofisi zao unaweza ukakuta ni mahandaki na vyote hivyo vinamiliki silaha kihalali na lengo lao ni moja.

Kwa hoja ya mleta taarifa kutekwa nineno zito sana halilingani na nguvu iliotumika kumchukuwa huyu dr.kutekwa lazima itumika nguvu kubwa.nguvu iliotumika hapa ni ya kawaida hivyo atakuwa amekamatwa na baadhi vyombo vya usalama ambavyo unaweza ukakuta hata vyenyewe havijuwani.

Kwa ajili ya kuhojiwa kuhusu mgomo wa madaktari unaoendelea.

Huo ni mtazamo na speculation tu mkuu,hatuna uhakika kama amechukuliwa na vyombo vya usalama au la, kumbuka unaweza ukafikiria hivyo kwa sababu tukio hilo limetokea wakati huu ambao kuna mgomo wa madaktari na yeye ni kiongozi, lakini ingetokea wakati mwingine wowote usingesema hivyo.

Suala la kuwa utekaji hutumia nguvu kubwa sio kweli mkuu, inategemeana na mtu anayetekwa na anavyofahamika kwa watekaji. We should not take this matter for granted tujiaminishe kuwa amekamatwa na vyombo vya usalama anahojiwa kama hatujui ni nani waliomkamata na wanamhoji kwa lipi!? Unless uwe mmoja wao na utuhakikishie hilo, otherwise serikali kupitia vyombo vya usalama inawajibika kujua huyu mtu yuko wapi na usalama wake ukoje!!
 
Watakuwa wapuuzi kweli wakimteka. Labda kukamatwa kwa kuvunja sheria. But does it help?
Akamatwe kwa kuvunja sheria ipi? Maana kugoma ni haki ya kila mtu, kama ingekuwa kudai haki yako ni kuvunja sheria basi tusingekuwa tunamsifu Nyerere, maana angekuwa ndo mhalifu kuwashinda wahalifu nchini Tanzania. Lets believe kwamba hawatamfanya kitu kibaya. Maana isije ikatokea kesho tukasikia mwili wake umekutwa kando kando ya barabara. Na kwa watz walivyo waoga, kila mtu atafyata mkia, halafu aliyekufa inakuwa ni hasara yake na familia yake.
 
[h=6]Dr. Ulimboka inadaiwa amekamatwa na polisi usiku kwenye majira ya saa saba kasoro hivi akiwa na wenzake. Watu ambao hawakujitambulisha na wakiwa na mavazi ya kiraia lakini wakiwa na silaha walimchukua Dr. Ulimboka mkukumkuku kwenda kusikojulikana. JItihada za awali za kufuatilia zilionekana kugonga mwamba. Hata hivyo, habari ambazo tumeweza kuzipata sasa hivi ni kuwa watu waliomchukua wanadaiwa ni polisi na kuwa yuko kwenye kituo cha Bunju nje ya jiji la Dar kupita maeneo ya Mbezi. Sasa hivi wanasheria na vyombo vya haki za binadamu vinafuatilia kujua hali yake huko aliko kwani juhudi za kutaka kuzungumza naye kwa simu zimeshindikana.

Ni matumaini yangu - na bila ya shaka ya wengine - kuwa Dr. Ulimboka ambaye ameonekana kama kiongozi wa mgomo wa madaktari unaondelea nchini hatodhurika kwa namna yoyote ile na kuwa sheria zote zinafuatwa siyo na wale wanaotaka wengine wafuate sheria bali na wale wanaopaswa kufuata sheria.

Kwa niaba yangu na CCTI tunalaani vitendo hivi ambavyo vinaonekana kutaka kugeuza Tanzania kuwa police state hasa baada ya kushindwa kutafuta suluhisho la kawaida. Na zaidi kama kuna jambo lolote ambalo limefanywa kinyume na sheria au haki au utawala wa sheria tunataka wahusika wote wawajibishwe mara moja.

Free Dr. Ulimboka Now!
[/h]
 
Dr. Ulimboka inadaiwa amekamatwa na polisi usiku kwenye majira ya saa saba kasoro hivi akiwa na wenzake. Watu ambao hawakujitambulisha na wakiwa na mavazi ya kiraia lakini wakiwa na silaha walimchukua Dr. Ulimboka mkukumkuku kwenda kusikojulikana. JItihada za awali za kufuatilia zilionekana kugonga mwamba. Hata hivyo, habari ambazo tumeweza kuzipata sasa hivi ni kuwa watu waliomchukua wanadaiwa ni polisi na kuwa yuko kwenye kituo cha Bunju nje ya jiji la Dar kupita maeneo ya Mbezi. Sasa hivi wanasheria na vyombo vya haki za binadamu vinafuatilia kujua hali yake huko aliko kwani juhudi za kutaka kuzungumza naye kwa simu zimeshindikana.

Ni matumaini yangu - na bila ya shaka ya wengine - kuwa Dr. Ulimboka ambaye ameonekana kama kiongozi wa mgomo wa madaktari unaondelea nchini hatodhurika kwa namna yoyote ile na kuwa sheria zote zinafuatwa siyo na wale wanaotaka wengine wafuate sheria bali na wale wanaopaswa kufuata sheria.

Kwa niaba yangu na CCTI tunalaani vitendo hivi ambavyo vinaonekana kutaka kugeuza Tanzania kuwa police state hasa baada ya kushindwa kutafuta suluhisho la kawaida. Na zaidi kama kuna jambo lolote ambalo limefanywa kinyume na sheria au haki au utawala wa sheria tunataka wahusika wote wawajibishwe mara moja.
 
Ni kweli katemwana askari mbaya zaidi kapigwa vibaya na kapewa vitiaho
 
Asante kwa taarifa Mkuu.
Tumefikia hapa tulipo, ambapo mpaka madaktari wamekuwa tishio kwa serikali kutokana na udhaifu wa Rais wa nchi hii.
Sioni sababu za msingi kwanini serikali inashindwa kushughulikia madai ya madaktari kwa njia sahihi. Serikali inashindwa vipi kujifunza kutoka kwa madaktari wa nchi zinazoendelea wanatatuaje matatizo ya madaktari.
And for sure, baada ya madaktari itakuwa zamu ya wengine. Kikwete ategemee kumaliza hiki kipindi vibaya sana!

Free Dr. Ulimboka now!!!!!!!!

I support the doctors!
 
kweli serikali imepoteza mwelekeo.yaani aibu ,udhaifu uliosemwa,ndo viashilia vyake hivi.
 
Ni upungufu wa akili na busara kudhani kuwa kumkamata Dr Ulimboka ndio kutaleta uvumbuzi wa mgomo wa madaktari!!!
Simple answers for tough questions
 
Ni kweli Dr. Olimboka katekwa na askari polisi na kapigwa na kwa sasa yupo kituo cha polisi cha uchochoroni tunakifuatilia kujua kama ndipo walipo mficha. Sasa hii imetuamsha hasira na mgomo kamili ndo utafuata.

Nimepata nafasi ya kufuatilia suala la Dr. Ulimboka. Naweza kuthibitisha kuwa amepatikana baadaya kuwa kupigwa kwa takribani masaa matatu, kujeruhiwa na kupoteza damu nyingi. Sasa hivi anakimbizwa hospitali kuokoa maisha yake bila ya shaka katika kumtumia ujumbe wa aina yake kama kiongozi wa mgomo wa madaktari.

Hii ni aibu ya taifa!

Tumwombee anusurike lakini vile vile wengine watiwe moyo kuwa wapo mashujaa katika Tanzania!!

Viva Dr. Ulimboka!! - M. M. Mwanakijiji
 
mh! sidhani kama that can be the case, labda useme amekamatwa. kutekwa?


uko sahihi kutekwa ni neno la maharamia wa kisomali..... kakamatwa linaonyesha kuwa yuko mikononi mwa dola kutekwa ina maana kwa lengo baya hata kuuawa pia
 
Tuweke shinikizo aachiliwe mara moja na bila madhara yoyote; utawala wetu umewekwa kwenye kona na sasa unatafuta namna ya kutokea...
 
It takes two to make a quarrel,but it might take the whole public to settle the damage of the quarrel.

Free dr.Ulimboka.
 
Yule kiongozi wa migomo TRL late Rwegasira yupo wapi?
Huu udikteta sasa.. Utamaliza wangapi?
 
[h=6]Hata hivyo, habari ambazo tumeweza kuzipata sasa hivi ni kuwa watu waliomchukua wanadaiwa ni polisi na kuwa yuko kwenye kituo cha Bunju nje ya jiji la Dar kupita maeneo ya Mbezi. Sasa hivi wanasheria na vyombo vya haki za binadamu vinafuatilia kujua hali yake huko aliko kwani juhudi za kutaka kuzungumza naye kwa simu zimeshindikana.

Ni matumaini yangu - na bila ya shaka ya wengine - kuwa Dr. Ulimboka ambaye ameonekana kama kiongozi wa mgomo wa madaktari unaondelea nchini hatodhurika kwa namna yoyote ile na kuwa sheria zote zinafuatwa siyo na wale wanaotaka wengine wafuate sheria bali na wale wanaopaswa kufuata sheria.

Kwa niaba yangu na CCTI tunalaani vitendo hivi ambavyo vinaonekana kutaka kugeuza Tanzania kuwa police state hasa baada ya kushindwa kutafuta suluhisho la kawaida. Na zaidi kama kuna jambo lolote ambalo limefanywa kinyume na sheria au haki au utawala wa sheria tunataka wahusika wote wawajibishwe mara moja.

Free Dr. Ulimboka Now![/h]
 
Imefikia huko tena, wameshindwa kutatua tatizo na wanakimbilia kutumia mabavu..........wanafanya hali iwe mbaya zaidi, vitisho na mabavu si suluhisho hata mara moja!
 
Back
Top Bottom