Kiongozi Msafi wa Africa na Aseme - Mugabe

Mimi nikisema Waafrika Ndivyo Tulivyo naambiwa nina inferiority complex. Hivi huyo waziri wa mambo ya nje ya Kenya yeye ana haki gani ya kuhoji uchaguzi wa Zimbabwe? Kama Mugabe asitambuliwe then Kenya (Kibaki) should be held to the same standard......

...two wrongs dont make one right!
 
Ila Comrage Mugabe ni Kamanda. Tuache yote, muhimu kamaliza jeuri ya wazungu!!!!!

Njaa, dhiki na hiyo inflation rate yenu ya 2,000,000% ni ya wazungu wala si mugabe. Yale mazungu yaliyonyang'anywa ardhi yamegoma kuzalisha, yamefunga viwanda na huku wajomba zao wa yuropa na marekani wakihimiza vikwazo. Ni upumbavu tupu, kudhani mugabe ndie anaeleta shida Zimbabwe!!!!! Ameongoza tokea 1980, Zimbabwe ilikuwa safi, uchumi bomba. Leo kaleta haki HAFAI!!!!

Ni ukoloni na utumwa. Kwamba mzungu amiliki ardhi, Mshona kibarua!!!!! Kinyume chake, Mugabe fashisti, dikteta, muuaji etc etc!!!!

Kweli mugabe amechoka, na ingekuwa busara apumzike, ila si kwa staili wanayotaka wazungu. Kama kweli wazungu wanataka demokrasia, mbona hawajaitambua HAMMAS palestine????

Kaza buti babaa!!!!

Bokassa,

Jean Bedel Bokassa na Robert Mugabe - Afrika itawakumbuka.
 
Nziku,

..Kenya wamekuwa kama kichwa cha mwendawazimu.

..Raila anazungumza kupeleka majeshi. VP Kalonzo Musyoka anazungumzia serikali ya mseto. Waziri wa Mambo ya Nje Watengula anapendekeza Kenya ikasuluhishe mgogoro.
 
Nchi ikishauzwa ni vituko tu!
Mmesahau ya kina MKULO NA WENZAKE KINA MEMBE!
Nyie hamjui kinachoendelea!
Mugabe
 
Viongozi ambao wanashindwa kumpa ukweli Bob ni wapumbavu, na upumbavu wao huo hauna maana kujustfy kukubali upumbavu alioufanya Bob................one has to draw a line......aagghh
 
Tunaolalama humu wote ni waTZ.Wazimbabwe wao haaa wanaona sawa tu.Mbona kwenye mikutano ya Mugabe nimeona watu kibao tuuu wakimshangilia????Hivi wao hawaoni hiyo hali ngumu mnayoisema????Wazimbabwe wamechagua style hiyo ya kuishi ninyi WaTZ mnakereekwa ama kweli waTZ ndo tulivyo.

Kama mna uchungu na Zimbabwe kajiandikisheni mpige kura basi.Ya kwenu yamewashinda mnakosoa ya Zimbabwe mna akili ninyi???Hayo ma muafaka yenu ya Makamba na Seifu ya nini sasa kama nyie mnajiona mnajua demokrasia.
Kama ni uzee mbona hamjaandamana KINGUNGE astaafu????Mnataka kuniambia kuwa nyie CCM mlikosa Makamu kijana hadi mmchukue Msekwa aliyekuwa amestaafu kwa hiari yake??????
 
Ndio maana anajeuri kwa sababu anajua hakuna anaweza kumkosoa kwa kuwa nao walifanya kitu kinachofanana na alichokifanya. Naona hata Bush na Brown, walioingia madarakani kwa wizi na fitna hawezi kusema kitu mbele yake.
 
Tunaolalama humu wote ni waTZ.Wazimbabwe wao haaa wanaona sawa tu.Mbona kwenye mikutano ya Mugabe nimeona watu kibao tuuu wakimshangilia????Hivi wao hawaoni hiyo hali ngumu mnayoisema????Wazimbabwe wamechagua style hiyo ya kuishi ninyi WaTZ mnakereekwa ama kweli waTZ ndo tulivyo.

Kama mna uchungu na Zimbabwe kajiandikisheni mpige kura basi.Ya kwenu yamewashinda mnakosoa ya Zimbabwe mna akili ninyi???Hayo ma muafaka yenu ya Makamba na Seifu ya nini sasa kama nyie mnajiona mnajua demokrasia.
Kama ni uzee mbona hamjaandamana KINGUNGE astaafu????Mnataka kuniambia kuwa nyie CCM mlikosa Makamu kijana hadi mmchukue Msekwa aliyekuwa amestaafu kwa hiari yake??????

Majita
Ukifahamu ukweli wa mambo utatambua kuwa watu walikuwa wanalazimishwa kwenda kwenye mikutano au rallies, na pia walilazimishwa hata kujitokeza kupiga kura. Tatizo sio uzee wa Mugabe tatizo ni kwamba hafai, ameprove kuwa hafai kutokana na uongozi wake, kama ilivyo kawaida anajaribu kuwasingizia wengine udhaifu wake.
Sisi Tanzania ni kama tuna desturi ya kuiga mabaya. Kwa sababu mwenyekiti wa ZANU PF ni mzee kwa hiyo CCM nao wanataka kuwa na makamu mzee, au kuwa na vinginge wengi kwenye chama. Matokeo yake tunayaona.
 
Mugabe kamaliza kazi

Mugabe Warmly Welcomed, Gently Criticized at Open of AU Summit
By Peter Heinlein
Sharm el Sheikh
30 June 2008

Heinlein report - Download (MP3)
Heinlein report - Listen (MP3)


Zimbabwe's Robert Mugabe has been warmly welcomed at a summit of African leaders, despite international concerns about the legitimacy of his re-election. From the summit in Sharm el Sheikh, Egypt, VOA's Peter Heinlein reports that in their opening speeches, Mr. Mugabe's colleagues offered only gentle criticism of the conduct of the election, and none of the man himself.

http://voanews.com/english/2008-06-30-voa26.cfm
 
Hivi Kuna Kiongozi Yeyote Katika Hii Dunia Anaingia Madarakani Kihalali?
 
Mugabe tatizo sio kuingia madarakani kihalali, tatizo ni wewe hauko tayari kutoa tax holiday kwa 'wawekezaji', tatizo lako hauko tayari kuingia mikataba ya Buzwagi, tatizo lako hauko tayari kutengenezewa marafiki wa dizaini ya Sinclair, tatizo lako hauko tayari kuruhsu mapesa ya EPA kuwekezwa kwenye mabenki ya 'wafadhili', tatizo lako hauko tayari kumwakikishia mkoloni access ya ulaji kama madikteta wenzio wanavyofanya. Rudi nyuma anza kugawa ardhi, machimbo ya madini na mashirika kwa 'wawekezaji' harafu usikie kama kutakuwa na kelele za human rights au democracy.

Dah Mafuchila wa Ukweli sana wewe.

Hapa naona umenena sana. Pamoja na huyu mzee wetu kuwa unorthodox lakini nadhani kafanya lile ambalo anaamini ni bora kwa Wazimbabwe. Kifupi ni kwamba kagoma kuwa kibaraka wa mtu na kama 'Frank Lucas' he is Representing Mugabe and his beliefs for a better Zimbabwe...
 
According To Bbc Jana Usiku, Less Than Half Of African Head Of States, Were Not Democratically Elected
 
Two wrongs don't make one right! Mugabe ni fisadi, dikteta, mwuuaji! He has to go na on top of that AMEIBA KURA!!!!!!!! HE HAS TO GO!!!!!!! And in fact he should be tried and shot like Ceaucescu! Kumbukeni naye alikuwa 80 something na fisadi mkubwa na mke wake! Mugabe's days are numbered!

Wizi wa kura hivi nao ni wizi? sidhani kama ni kweli kwamba watawala wa sasa wa Africa ukliwaambia kwamba Mugabe kaiba kura watashtuka!

TIA
 
I personal get sick the way waafrika tunakubali brainstorming za western media when it comes to politics za Zimbabwe, hizo stereotyping sidhani kama factor ya mimi binafi kuamini kuwa STILL MUGABE HE IS RIGHT!!, no matter what we will say upon him and what is happening in Zimbabwe so far!!

Hivi when it comes to kunauchaguzi BOMU in Africa uliotokea hivi karibuni kama wa Nigeria?, kama wa Kenya?, hivi kuna violater mkubwa wa Human Rights Duniani kama Zenawi?, Mu7?, what are talking jamani?, juzi naangalia CNN nakutana na picha ya political casuality wa vurugu, hiyo clip since December wanairudia tena na tena!, waulize Wakenya ODM esp. what the policemen did for them!!

This is Africa jamani!!, the definition of ''democracy'' in Africa is not the same as in America, as in Europe, As in Pakistan, as in Afghanstan, as in Palestina......etc etc..

Kitu ambacho i was thinking personally, ni kwa SADC kupitia Mbeki wajaribu kumshawishi(last time), kuwa for the sake of the country as a whole Mugabe should step down, na amsimamishe candidate mwingine.....'coz for me is the war btn the WEST and Mugabe na not ZAFU-PF per se!

Stand up!! viva Mugabe&Obama hata yakiwashinda mmeonesha sisi sio vilaza kihivo bwana!!
 
Subirini uchanguzi wa Uganda nani zaidi. UGANDA au Zimbabwe, maana ya Kenya ilikuwa ni Appetizer tu!
 
Quote fro BBC (http://news.bbc.co.uk/2/hi/africa/7481857.stm)

President Jakaya Kikwete of Tanzania, the African Union chairman, pointedly congratulated the people of Zimbabwe over the election, but not Mr Mugabe himself.

Africa's longest serving leader, Gabon President Omar Bongo, has given the strongest suggestion of recognising Mr Mugabe as president, saying "he was elected, he took an oath, and he is here with us, so he is president".

Huu ndio unafiki wenyewe...

Kwa nini mtu usiamue kuonyesha rangi zako halisi badala ya kusimama on the sidelines hoping that whoever that will happen to take for a ride will consider you a friend... Alitakiwa ampongeze Mugabe ama apingane nae!!!

Unawapongeza wananchi kwa Uchaguzi wa Wabunge ama Rais? Na Rais mwenyewe kwa nini usimpongeze kwa kuchaguliwa... He is the one who deserved those Pongezi!!! Na kama anampinga Mugabe angewapongeza Wazimbabwe kwa uchaguzi kisha kusema anapinga Mugabe kukikalia kiti cha Urais wa Zimbabwe. Yeye si mwenyekiti wa AU!!!
 
Afungue kiongozi yeyote mdomo wake kuhusiana na mabaya ya Mugabe, aone jinsi Mugabe atakavyomgeuzia kibao na kuyataja mabaya mbali mbali ndani ya nchi anayotoka kiongozi huyo. Wacha JK aingie mitini!! Mugabe yuko tayari kumkabili na ana data zote za uozo ndani ya Tanzania

Date::7/1/2008
Viongozi Afrika wamgwaya Mugabe
Sharm El-Shaikh, Misri
Mwananchi

RAIS Robert Mugabe amehudhuria mkutano wa Viongozi wa Umoja wa Afrika unaofanyika nchini Misri, huku washiriki wa mkutano huo wakionekana kumgwaya katika hotuba zao.

Baadhi ya marais akiwemo mwenyekiti wa AU, Jakaya Kikwete walipatwa na kigugumizi kwani hakuna aliyethubutu kumnyooshea Mugabe kidole, badala yake walikuwa wakikosoa kwa upole baadhi ya kasoro zilizojitokeza wakati wa uchaguzi Mugabe aliwasili katika mji wa Sharm El-Shaikh, nchini humo na kupokewa vizuri na viongozi wenzake na kisha kuhudhuria kikao hicho, ambacho wachunguzi wanahisi sehemu kubwa ya mjadala itahusu matatizo ya kisiasa yanayoendelea nchini Zimbabwe.

Wakati akiingia katika Ukumbi wa Mkutano, Mugabe aliongozana na Mwenyekiti wa AU, Rais Jakaya Kikwete na Hosni Mubarak ambaye ni mwenyeji wa mkutano huo wa siku mbili. Akizungumza kwa tahadhari kwa kutumia lugha ya Kiswahili Rais Kikwete aliwasifu wananchi wa Zimbabwe kwa kile alichokieleza kama mafanikio kwao.

Tumeshuhudia chaguzi za kihistoria zilizofanywa katika awamu mbili, kulikuwepo na mambo mazuri na changamoto pia. Lakini kwa sasa baada ya kwisha kwa uchaguzi uliofanyika siku mbili zilizopita kuna changamoto nyingi zaidi zinazohitaji kuzungumzwa, alisema Rais Kikwete.

Wakati huo huo, Mugabe amesema hatasita kuwanyooshea kidole viongozi wote watakaothubutu kusema kuwa alichofanya halikuwa jambo sahihi. Sauti ya Amerika (VOA) Habari zaidi Uk.24 Imeandaliwa na Abeid Poyo kwa msaada wa mtandao wa kompyuta. E&P......2008/06/30
 
Hakuna kiongozi msafi Africa la sivyo tusingekuwa hapa tulipo!Hasa viongozi wa sub saharan Africa!Haiwezekani tuwe na matatizo yanayofanana!Viongozi safi walikuwa kina PATRICE LUMUMBA,Nkwame Nkurumah na SEKOE TOURE!Wengine ni vibaraka tu wa wazungu!Ndo mambo ya ukoloni mamboleo
 
..Dr.Migiro amezungumza kwa niaba ya Ban Ki Moon na amesisitiza suala hili litatuliwe KIDIPLOMASIA.

..Kikwete inabidi awe careful na Mugabe. tena naona amefanya vizuri kuongea kiswahili. Hakuna anayeweza kusimama "pound-for-pound" na huyu Mzee.
 
Back
Top Bottom