Kioja weekend.

DEVINE

JF-Expert Member
Mar 11, 2011
536
86
Nikiwa maeneo ya kimara_resort jana usiku nilijikuta nashuhudia vurumai moja matata.Mwanamke mmoja anayesadikika kula na shemeji yake alafu pia kukimbiwa na mumewe na kukimbilia Marekani alizua varangati asiloliweza.Akiwa anavinjari na shemeji yake Safari-Resort,na kupeana mabusu motomoto pembeni kwenye garden karibu na parking gari iliyo egeshwa mbele yao iliwashwa na kuwamulika live.Mwanamke huyo alikasirishwa na hali hiyo,akaivamia gari nakutaka kuvunja vioo.Mwenye gari hiyo kutokana na maelezo yake nia yake ni kugeuza na kuondoka lkn si kummulika yule mwanamke na shemu wake.Sasa ilimbidi ashuke na kumzuia mama huyo kuvunja vioo,mara shemeji wa mwenye gari akaja na kumnyofoa yule mama asing'ang'a nie gari,cha ajabu mama yule alimng'ata yule kaka na kusababisha kupigwa ngumi za fasta palepale,hakujua anamfanyia fujo nani.Kesi ilienda mpaka polisi kimara baada ya mke wa alieng'atwa kufika na kundi lake.Mwanamke yule akakimbia na kujifungia nyumbani kwake jirani na hapo akiwa ndani alitupa maneno ya kejeli na matusi asijue ni kinanani anawatukana,majirani hadi wapangaji wenzie walisikika wakisema huyo nitabia yake kuzua mavarangati hata kutukana watu adharani.Sijui ilitokea wapi crew ya JWTZ yule mama ilikuwa ni kuchakazwa sawasawa na wajeda hao baada ya polisi kugoma kutoka kituoni kuja kusuruhisha varangati hilo.Bila ya shemeji yake au bwana wake kuja kupiga magoti na kulia,yule mwanamke alikuwa anaokotwa MOI.
*Jama wanawake chungeni maamuzi yenu na kauli zenu si wote lakini msije jutia,wajeda wameacha amri kwa askari leo wamkute yule mwanamke kituoni la sivyo sijui nini kitatokea*
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom