Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,299
- 33,080
Rashid Mwinshehe Kingwendu Saturday, August 22, 2009 7:40 AM
Komedian aliyekwenda eji Bongo, Rashid Mwinshehe Kingwendu ameingizwa mjini na promota mmoja jijini Mwanza. Kingwendu akiongea na Showbiz mapema wiki hii alisema kwamba, promota huyo amemtia ndani kiasi cha fedha shilingi milioni 1.5 ambazo aliziingiza baada ya kupiga mzigo Kanda ya Ziwa.
Said: (anataja jina la mtu aliyemliza) amenifanyia kitu kibaya sana, alinichukua vizuri Bongo akanipa advance, kula, kulala haikuwa na matatizo, kwahiyo nikamuamini lakini kumbe siyo mtu kihivyo.
Baada ya kupiga shoo kwenye vijiji vya Zalagula, Kasaratu, Nyanango na Kanyala jijini Mwanza, nilikuwa nimekusanya shilingi milioni 1.5 kibindoni lakini juu kwa juu nilipata dili kwahiyo nikaunganisha shoo.
Promota wangu aliniomba nimpe pesa hizo ili akaniwekee kwenye akaunti yangu, mimi kwa sababu nilikuwa nimeshamuamini nilimpa lakini huwezi kuamini, baada ya hapo kila nikimpigia simu ni stori tu.
Hivi sasa nimemfungulia mashataka polisi kwa kosa la wizi wa kuaminiwa. alisema Kingwendu.
http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsId=2883326&&Cat=1