Kingunge ataka Suluhu na Upinzani?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991
Mapema leo waziri wa Nchi ofisi ya Rais anayeshughulikia siasa alikutana na waandishi wa habari ofisini kwake. Alizungumza mengi na kubwa ambalo binafsi nililichukulia ni mwelekeo wa kiongozi huyo kutaka "suluhu" na upinzani. Msisitizo mkubwa aliuonesha pale alipozungumza kuhusu Uzalendo "wetu sote" na ya kuwa tofauti za sera na itikadi zisitufanya Watanzania kujiona siyo kitu kimoja. Alipojaribu kuelezea hiyo tofauti alishindwa kutaja neno ujamaa na kwa dakika chache alijiuma uma meno na kusema "Sisi CCM tunazo sera .. na itikadi.. za.. tunazo itikadi; na vyama vingine wanazo sera na itikadi zao".

Bila ya shaka lengo kubwa ni haja ya ofisi hiyo kuona kuwa licha ya tofauti zetu Watanzani tunaendelea kuwa kitu kimoja. Nilivyochukulia ni kuwa alikuwa anajibu mwelekeo unaoonekana sasa hivi ambapo "wazalendo" wanaonekana ni wale wa upinzani zaidi na walio weusi. Kiufupi, Kingunge naamini ametumwa kuja kutaka suluhu na wapinzani... wapatane naye?
 
Suluhu ya ugomvi upi? Mwkjj u just read too much on it... hence making storm in cup of tea!
 
how did you read it? a hand of reconciliation? ishara ya amani, na umoja au vipi... ?
 
Hakuna sababu ya kupatana nae kama chama chake (CCM) kitaendelea na mfumo wa kulindana (kuwalinda mafisadi kwa nguvu zote) huku nchi ikiendelea kuliwa na baadhi ya watu walio karibu na CCM.

Waweke karata mezani na siyo uvunguni mwa meza ili tuone kinachoendelea. Nadhani karata zikiwa mezani hakuna atakae lalamika kwamba kuna rafu zinaendelea. Hiyo ndiyo inaweza kuwa suluhu ya kweli.

Tofauti ya sera na itikadi sidhani kama ni swala kubwa sana mbele za watu kwa sasa. Wapinzani wamepata nguvu zaidi baada ya kuanza kuongelea swala la madini, rushwa, ufisadi na mengineyo ambayo yameichanganya serikali na kuonekana ikitoa matamko yanayokinzana. Kwa hiyo kwa mtazamo wangu, suluhu ya kweli inaweza kupatikana iwapo tu serikali itakubali iwe wazi na tuhuma zote za rushwa zifanywe kwa uwazi mkubwa bila ya kuficha ficha ili wananchi waelewe nani anasema ukweli na nani anasema uongo kwenye hizo tuhuma.

Sambamba na hayo taasisi nyeti kama PCCB na Polisi inabidi zifanye kazi kwa maslahi ya umma na si kwa maslahi ya serikali iliyo madarakani. Uteuzi wa IGP na DG wa PCCB inatakiwa ufanywe na Rais lakini kuwe na utaratibu wa ku-approve hizo appointments ili mteuliwa asiwajibike kwa Rais pekee bali awajibike kwa wananchi na Taifa lake kwa ujumla. Leo hii kila mtu analalamika kwamba Polisi na PCCB hawatendi haki, na utendaji kazi wao una macho kuna baadhi ya maeneo ambayo hawayagusi kabisa kwa kuwa ni maeneo ya wakubwa ama ni nyeti na hivyo wanaogopa kugusa maeneo ambayo vigogo wana maslahi yao.
 
Suluhu na Kingunge? Aachie madaraka kwanza maana amezeeka. Hayo ni maneno matupu, hao ndio jamaa wa SPINS wenyewe, achane naye afaidi walivyotuibia.
 
MZee vipi huyu, kwani kuna lipi baya? Kufichuliwa machafu yanayowakosesha usingizi ni ugomvi? Ina maana anataka wakae kimya ili wao waendelee kufyonza tu! aona hapa anazidi kuonesha uzee wake!
 
binafsi nililichukulia ni mwelekeo wa kiongozi huyo kutaka "suluhu" na upinzani. Msisitizo mkubwa aliuonesha pale alipozungumza kuhusu Uzalendo "wetu sote" na ya kuwa tofauti za sera na itikadi zisitufanya Watanzania kujiona siyo kitu kimoja.

Mkuu MMJ,

Heshima mbele, sasa hii ndio hasa political spin at work, huyu mzee anasema nini? Hivi unajua anachojaribu kufanya hapa ni kukwepa kwenda mahakamani kwa mafisadi, sasa anachojaribu hapa ni kujenga hoja ya kuwanusuru baadhi ya watuhumiwa ili atafute ujiko na Muungwana, kwamba yeye ana akili sana ya siasa mpaka ameweza kuanzisha hoja ya reconciliation ambayo in the end itawafanya mafiasdi wasiende mahakamani, NONESENSE!

Muungwana, hamuhitaji tena na yeye binafsi anajua hilo tayari, umuhimu wa kutumika kwake na Mtandao, kushinda uchaguzi wa 2005 sasa kinafikia ku-expire maana hata Mtandao wenyewe hawana uhakika wa the next move au hata kama bado wapo, huyu sasa anachojaribu ni kucheza surviving political games, hamuwakilishi Muungwana tena, hilo sio siri baada ya uchaguzi wa majuzi wa CCM, anyways acheze michezo yake huko ndani ya CCM, lakini sio kwenye taifa, ambako tunatka the respect kwa the rule of law, sio mambo ya mshikamano na huyu ni mwenzetu!

Mafisadi ni lazima waende mahakamani ili kuisafisha serikali, no matter how much spin zikiwekwa at work, ni waste of time kwa wananchi wengi ambao sasa hivi wana mashaka sana na serikali yao!,

Mkuu wangu Muungwana nakuomba usikie hiii, straight from my soul kuwa kusafishika kwa serikali yako kwenye tuhuma za ufisadi ni lazima watuhumiwa watinge mahakamani otherwise politically you are going down!
 
Wapinzani hawana ugomvi na CCM. Ugomvi mkubwa kati ya CCM na wapinzani ni chama hiho kuafumbia macho viongozi waroho wa utajiri wanaopenda kujilimbikizia mali kupitia nyadhifa zao ( Mkapa na wenzake).

Kusaini mikataba mibovu ya madini ambayo haina maslahi kwa Watanzania na kuamua kuifanya siri sijui kwa faida ya nini. Kufanya manunuzi ya Rada, ndege ya Rais, magari ya jeshi n.k katika mazingira yaliyojaa na kunuka rushwa.

Kuwalinda na kuwatetea waliohusika na upotevu mkubwa wa pesa pale BOT na kutotaka kuzichunguza gharama kubwa za ujenzi wa twin towers na pia kuwalinda waliohusika na kusaini mkataba wa Richmonduli.

Pia kuwaweka madarakani mawaziri ambao wameshaonyesha wazi kutokuwa watendaji wazuri wa kazi zao akina Karamagi, Magufuli, Meghji, Mramba, Msolla n.k.

CCM iwape takukuru uwezo wa kuwachunguza wote wanaotuhumiwa kuwa wamepata utajiri kwa njia zisizo halali akiwamo Mkapa, kama kuna ushahidi wa kutosha wafilisiwe mali zao na kufikishwa mahakamani. Mikataba yote ya madini iwekwe hadharani ili details zake zijulikane kwa Watanzania wote.

Mawaziri wabovu wote waondolowe madarakani mara moja na migodi yote inayomilikiwa na viongozi ikiwemo Kiwira Coal Mining irudishwe chini ya miliki ya serikali maana hao wenye miliki hawakuipata kwa njia halali.

CCM ikifanya hayo basi uadui kati yake na wapinzani utakwisha kabisa na wapinzani wanaweza hata kuwapa ruhusa ya kutawala milele ili mradi tu siku zote waweke mbele maslahi ya Watanzania badala ya matumbo yao.
 
Long way to freedom, hapa huyu mzee anatafuta jinsi ya kuweza kunusurui heshima yake kwani tangu awatetee mafisadi na hatimaye mafisadi wengine wakakiri na kusema kuwa hawataenda mahakamani, nahisi anajiona mjinga sana .

Kuna mzee mwenzake walikuwa naye TANU wiki iliyopita alimwandikia barua kali kwenmye gazeti la mwanahalisi na niliamini hiyo barua kwani alitaja hadi kadi yake ya CCM na hata ile ya TANU na pia majina yake na alipo.

Kingunge you have to go now,
 
Kingunge ni msanii tu, huo anaouita uzalendo ni nini hasa, kwa miaka mingi uzalendo kwa watawala wetu umekuwa ni kuwaogopa kuwapigia magoti na kuwasifu. kinyume cha hayo wewe si mzalendo. Na ni uzalendo wa jinsi hii ulioifanya nchi ikafika mahali ilipo. kingunge angekuwa mzalendo angekubali kuzungumzia katiba ya nchi, angekubali mjadala na kuwa tayari kufanya mabadiliko kwenye katiba yetu kwa mambo yote ambayo wengi tunadhani yako kinyume na haki za raia. sasa kama kingunge anasema hiyo si ilani ya ccm basi uzalendo wake uko kwenye chama zaidi ya nchi. ana uzalendo gani wakati karibu kwa maisha yake yote amekuwa akipotosha umma kwa kujaribu kuufanye uamini kuwa walikuwa wakifanya maendeleo huku akijua kuwa tulikuwa tunaporomoka? leo ana uzalendo gani maana hata hiyo ministrial post aliyo nayo anajua kuwa anapata mshahara wa bure maana hana kazi ya maana anayofanya, angekuwa mzalendo si angemshauri rais tu kuwa pesa anazotumia kama waziri zijenge vyoo pale azania secondary.

kumsikiliza kingunge ni kuendelea kupoteza mda na kuzidi kuongeza ujinga. kama kuna watu wa kulaumiwa kwa yanayoipata Tanzania ni pamoja na huyu mzee.
 
binafsi nililichukulia ni mwelekeo wa kiongozi huyo kutaka "suluhu" na upinzani. Msisitizo mkubwa aliuonesha pale alipozungumza kuhusu Uzalendo "wetu sote" na ya kuwa tofauti za sera na itikadi zisitufanya Watanzania kujiona siyo kitu kimoja.
Mkuu MMJ,

Heshima mbele, sasa hii ndio hasa political spin at work, huyu mzee anasema nini? Hivi unajua anachojaribu kufanya hapa ni kukwepa kwenda mahakamani kwa mafisadi, sasa anachojaribu hapa ni kujenga hoja ya kuwanusuru baadhi ya watuhumiwa ili atafute ujiko na Muungwana, kwamba yeye ana akili sana ya siasa mpaka ameweza kuanzisha hoja ya reconciliation ambayo in the end itawafanya mafiasdi wasiende mahakamani, NONESENSE!
Muungwana, hamuhitaji tena na yeye binafsi anajua hilo tayari, umuhimu wa kutumika kwake na Mtandao, kushinda uchaguzi wa 2005 sasa kinafikia ku-expire maana hata Mtandao wenyewe hawana uhakika wa the next move au hata kama bado wapo, huyu sasa anachojaribu ni kucheza surviving political games, hamuwakilishi Muungwana tena, hilo sio siri baada ya uchaguzi wa majuzi wa CCM, anyways acheze michezo yake huko ndani ya CCM, lakini sio kwenye taifa, ambako tunatka the respect kwa the rule of law, sio mambo ya mshikamano na huyu ni mwenzetu!

Mafisadi ni lazima waende mahakamani ili kuisafisha serikali, no matter how much spin zikiwekwa at work, ni waste of time kwa wananchi wengi ambao sasa hivi wana mashaka sana na serikali yao!,

Mkuu wangu Muungwana nakuomba usikie hiii, straight from my soul kuwa kusafishika kwa serikali yako kwenye tuhuma za ufisadi ni lazima watuhumiwa watinge mahakamani otherwise politically you are going down!

Mh.FEM ES.
Siku nyingi nilikuwa sijasoma maoni yako ya kizalendo ambayo yako Straight kama hii.Nilianza kuona badala ya kuembelea miguu sasa unatembelea kichwa.
Ilinibidi nifikiri kidogo,na nikadhani wakuu wa CCM waliokaribu nawe wamekushtukia kwa madongo yako ya kumkoma nyani kweupe na pengine kukuomba kupunguza hiyo kasi.Ukweli niliona umebadilika from 0 to 180 degree.Kwa sasa pale unapolazimika kusema ukweli,utaponda wote ila ukifika kwa JK,utambeba!!!??
 
Back
Top Bottom