King'amuzi cha Digitek

Vinapatikana wapi hapa Dar-es-salaam kwa uhakika zaidi? au ofisi yao iko wapi?
 
Ngoja tuende huko ofisini kwao tupate more and clear information ........... hapa JF naona ni malumbano tu
information ya kutosha ZERO
 
kama hakuna soka vizimwe tu nchi kwani ni maigizo tu.

Ndiyo nyie mnaoshindana kwa ubishi hata kupigana kwa sabau ya timu za ulaya wakati rasilimali za nchi zinaibiwa، nilidhani kipaumbele chako kingekua habari (news channels) ambayo inakuongezea ufahamu wa kumla, halafu mpira kwakua ni burudani ikawa chaguo la pili,
ukumbuke mpira ni ajira kwa anayecheza kwa mtu wa aina yako mpira ni burudani, kwahiyo uburudike baada ya kuingiza kitu kichwani (ufahamu) na mfukoni (pesa kwa kufanya kazi)
 
Ngoja tuende huko ofisini kwao tupate more and clear information ........... hapa JF naona ni malumbano tu
information ya kutosha ZERO


Kweli akili nywele! Penye malumbano ndiyo penye fursa nzuri ya kupata elimu ya kutosha. Kumbuka katika hawa wanaolumbana wengine wana ufahamu mkubwa zaidi wa haya mambo kuliko mimi na wewe. Ndiyo maana umeona hata huyo mtu wa TCRA amekuja kuclarify some issues kwa kuthamini arguments za wanaolumbana.Haya wewe nenda huko ofisini kama haujaishia kurudi tena hapa JF kuuliza wakati mambo yameshaenda kombo,tafakari!
 
Ngoja tuende huko ofisini kwao tupate more and clear information ........... hapa JF naona ni malumbano tu
information ya kutosha ZERO

Nenda pale karibu na kijiji cha makumbusho mwenyewe nikekifuata last week connection simple and clear hakuna kugeuza anntena kisarawe
 
Kampuni zote zilizopewa leseni kutoa huduma ya dijitali zote zina ofisi Tanzania Na ni moja ya Masharti ya leseni. Kama matangazo yetu yalivyoobesha huko nyuma wakati wa kutoa leseni wamiliki walitangazwa. Agape Associates walionesha ni consortium ya Watanzania asilimia 100, hii ni pamoja na kampuni Tanzu ya kuuza Kingamuzi chao Cha Ting. Badic Transmission kina shareholder watatu, wazawa wawili na mbia toka nje na wamegawana asilimia kwa mujibu wa makubaliano yao. Star Media Tanzania hali kadhalika kina wabia wawili, Serikali ya Tanzania kupitia TBC na kampuni ya Star Media International ya China. Kampuni yao Tanzu ya kuuza vingamuzi pamoja na channel za kulipia (leseni tofauti) Star Times.
Mkuu TCRA nashukuru kwa ufafanuzi wa kiutalamu unaoutoa kuondoa mkanganyiko kwa wananchi. Ninaomba kueleweshwa kama ile kauli yenu ya local chanels kuonyeshwa bure mbona utaratibu huo umeanza kukiukwa na kampuni moja bado mapema kwa kuwasainisha wateja mkataba wa lazima kulipia tshs 6000 kwa mwezi bila hivyo uoni chochote?

Kwa kuwa nchi yetu imejiunga na ushirikiano wa Afrika mashariki,ili kudumisha ushirikiano huo na kujua wenzetu wanafanya nini ili tusiwe wasindikizaji kwenye ushirikiano huo hauoni umuhimu wa local channels za KENYA ,UGANDA,RUANDA NA BURUNDI Zikajumuishwa kenye list ya local channels?
 
Muonekano wake ni mzuri sana nani wa HD na kinatumia antena ya ndani tu yoyote.Bei ni Tsh 160,000 pamoja na atena na kifurushi cha mwezi mmoja.Na bill yake kwa mwezi ni elfu 6 tu, kimajumuisha local 10 na International news kidogo.Kwa sasa kama unaitaji waweza kunijulisha au piga no 0784635662.Get connectes with Digteck
Elfu 6 tena si tunatangaziwa kuwa hakuna kulipia mwisho wa mwezi ukinunua.Hebu fafanua hiyo 6000 inatoka wapi tena?
 
Hiki si hakitumii satelaiti?kwa hiyo ni sawa na Startimes,ambayo mpaka uelekeze antenna Kisarawe ,sasa hii Dig Tek sijui antenna inaelekezwa wapi,na si ajabu ni maeneo yalio karibu tu ndio hupata signal,hebu mtueleze na coverage yake kwa mfano hapa jijini Dar
 
Mkulu
King'amuzi hicho ni HD kwani kina HDMI port, sasa wewe unavyosema "WANAKIITA HD" una maana gani??!!

Generally, HD quality depends on the Camera involved in the shooting.... unategemea picha za akina Charles Bronson zilizopigwa na kamera za 1947 unategemea zionekane kwa ubora wa HD?...haiwezekani.


Mengi ameweza kufanya kitu tofauti sana.
BTL subsidiary ya IPP imepewa jukumu la kusimamia king'amuzi kinachofahamika kama "DigiTek". Kampuni hii, ni ya kwanza yenye makao makuu hapa Tanzania.

Kwa tafsiri nyingine, Mengi ni mtanzania "mzanea" i.e NATIVE ( Mzanea >"mzawa" i.e "by birth") wa kwanza kuleta huduma ya aina hii.Makampuni mengine yote yametoka nje.

Tumuunge mkono mzanea mwenzetu, hasa tukimpima kwa kuzingatia ubora wa king'amuzi chenyewe vs washindani wake.

Take note.

Kwa ajili ya kumbukumbu:
SERA YA UZANEA ilizungumzwa vizuri sana... kipindi kile cha mageuzi ya kisiasa hapa nchini na Mh W. Mwakitwange(RIP). Kwa wale wenye interest na hiyo sera, wafuatilie....basically inahusu "EMPOWERMENT YA WATANZANIA HALISI". MTANZANIA HALISI NI YULE AMBAYE HISTORIA YA UKOO WAKE NI ZAIDI YA VIZAZI SABA

Ili uone HD unahitaji source zako zote ziwe HD...kwa mfano HD movie lazima uwe na hd tv,hd dvd player na hd dvd[blue ray].....ili uone hd tv broadcast unatakiwa uwe na hd tv...hd set top box[digitek au dstv pvr] na tv broadcaster arushe matangazo kwa HD format....swali la msingi...Je ITV na local channel nyingine wanarusha matangazo kwa HD format??i dont think so.....sasa basi hao itv wakisema utaona matangazo yao kwa HD just bcoz digitek decoder ni HD ni upotoshaji.
 
Mkuu TCRA nashukuru kwa ufafanuzi wa kiutalamu unaoutoa kuondoa mkanganyiko kwa wananchi. Ninaomba kueleweshwa kama ile kauli yenu ya local chanels kuonyeshwa bure mbona utaratibu huo umeanza kukiukwa na kampuni moja bado mapema kwa kuwasainisha wateja mkataba wa lazima kulipia tshs 6000 kwa mwezi bila hivyo uoni chochote?

Kwa kuwa nchi yetu imejiunga na ushirikiano wa Afrika mashariki,ili kudumisha ushirikiano huo na kujua wenzetu wanafanya nini ili tusiwe wasindikizaji kwenye ushirikiano huo hauoni umuhimu wa local channels za KENYA ,UGANDA,RUANDA NA BURUNDI Zikajumuishwa kenye list ya local channels?

...Hajakujibu?? Ni bahati mbaya sana kwamba hawa Jamaa wa TCRA wakiona maswali mepesi mepesi wanakuja hapa kwa Mbwembwe kutoa Maelezo lakini wanapopigwa maswali muhimu na magumu kama uliyouliza, wanaingia mitini bila hata kuaga...So Sad.:nono:
 
Ili uone HD unahitaji source zako zote ziwe HD...
swali la msingi...Je ITV na local channel nyingine wanarusha matangazo kwa HD format??
TCRA alishajibu hilo mkuu!
Taarifa rasmi, ili kujibu maswali ya wengi hapa. Hakuna kituo chochote Cha Utangazaji Tanzania kinachotangaza kwa mfumo Wa High Definition. Content Service Provider wote hakuna anayetoa matangazo Kwa mfumo huo. Aidha, kiteknolojia haiwezekani Miltplex Operator akabadilisha signal kuipeleka HD.

Tuwasaidie Watanzania kwa kuelezea ubora kama ili yotolewa kuwa ni MPEG 4 nk ambayo ina quality nzuri zaidi.
 
Back
Top Bottom