Njilembera
JF-Expert Member
- May 10, 2008
- 1,496
- 607
Japo siungani na msomali moja kwa moja, lakini hoja ya msingi ina mantiki tuu tusibakie kulaumu, kulalamika na kulalama tuu, bali kampeni ziseme tutafanya nini.
Yaani zisibakie kampeni za fault finding mission, bali trend setting mission, hayo mabaya ya nyjuma/CCM yatumike kama sababu, cause ya kutufikisha hapa tulipo, na isiwe ndio the only finger pointing CCM, CCM, tunawapa free publicity hawa CCM kwenye kampeni zetu.
Nitarudia yaliyokwisha semwa humu jamvini, kinachotokea, watafuta kura wanatumia muda mwingi kuelezea sera zao na jinsi watakavyokabiliana na matatizo ya maendeleo. Ila kama vile 'by the way' wanagusia mabomu yaliyokwisha elekezwa kwao. Sasa waandishi wa habari wanakuza hilo wanasahau hata lile lililoweka hadharani. Tatizo naliona ni kwa waandishi, wanapenda mno sensational news! Angalia Habarileo alichoweza kuona ni Dr Slaa akiwa na 'wachumba' wake wawili! Ni nani hapa wa kulaumu? Sio huyu kwa makusudi kabisa anapotosha uma! Yaani inakuwa kama vile Slaa alijiandaa kwenda kuwaonyesha hao. Tatizo ni poor and biased reporting, na hii inatokana na taaluma ya uandishi wa habari kukosa maadili; ndio maana wamekuwa wakinunuliwa kushoto na kulia na tycoons kama RA, EL, BWM na JK!