Kinachotokea Zanzibar ni kushindwa kwa uongozi wa CCM

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
[video=youtube_share;J_3Y2TNSTb0]http://youtu.be/J_3Y2TNSTb0[/video]
Yaliyotokea Zanzibar leo na yale yanayoendelea ni matokeo ya kushindwa kwa utawala wa CCM kutatua matatizo ya Muungano. Lakini pia ni ishara ya kushindwa kwa viongozi wetu wa kisiasa nchini kuutetea Muungano na kujenga hoja za kwanini yapaswa uendelee. Kwa muda mrefu kikundi cha watu wachache kimekuwe kikisukumiza hoja dhidi ya Muungano na baadhi yao kuzawadiwa nafasi za uongozi licha ya msimamo wao juu ya Muungano kujulikana. Hivyo siku baada ya Muungani (A Day After the Union) itakapofika siyo Wananchi wa kawaida watakaolalamikiwa bali viongozi wale ambao wameacha siku hiyo ifike. Ukimya wa Wazanzibari wenye kuamini katika Muungano kumewachochea kundi hilo dogo. Tusije kushangaa tunashuhudia kuzaliwa kwa kikundi cha "Boko Haram" cha Tanzania!!! Yote yatakuwa ni kwa sababu ya kushindwa kwa utawala wa CCM kutoa uongozi!

Hatujasikia viongozi wa CCM wakitetea Muungano kama wanavyotetea chama chao; hatujawasikia wakiwapinga anti-unionists kwa hoja zenye nguvu bali wamekuwa wakiwapa baraza huru; na hatujawaona hata viongozi wao wa serikali - walioapa kulinda Katiba ya Muungano - wakitetea Muungano huo.

Ni kana kwamba wameshakubali kisichoepukika - kufa kwa Muungano. Sasa, kama hili ndilo wanalolitaka hakuna haja ya kuumizana, kupigana mabomu, wala kushindana. Kama kuvunjika kwa Muungano ni inevitable - basi hekima inatutaka tuweke mfumo wa kuvunja Muungano huu vizuri na kwa makusudi ili mahusiano ya kidiplomasia baina ya nchi mbili yaanze. Jamani, Muungano uwepo au usikuwepo watu wa Zanzibar hawaendi popote na watu wa bara hawaendi popote. Hata watu waombee vipi Wazanzibar wataendelea kuwepo na watu wa bara wataendelea kuwepo. Sasa kama hii ni kweli basi ni kushindwa tu kwa viongozi wetu na hasa kushindwa kwa sera zao mbovu ndiko kunakofanya mgogoro huu uwe mkubwa kuliko inavyopaswa.

Tusizungushe maneno! Kuvunjika kwa Muungano kutakuja si kwa sababu ya Uamsho au vikundi vya kidini; kutakuja kwa sababu wanasiasa wetu wameshindwa!

Let me be very blunt: Ajenda ya kisiasa ya Zanzibar sasa hivi inaendeshwa na watu wa CUF; wana CCM Zanzibar wamefyata mkia. hawawezi kuwapinga CUF bila kuonekana "hawaitakii mema Zanzibar" na wale wanaoamini katika Muungano hawana ujasiri wa kuwapinga hawa wengine. CUF ndio wanaendesha siasa za Zanzibar sasa.Tumeona katika jaribio lao la kuwapiga marufuku watu wa bara kufanya kazi Zanzibar. CCM imedhoofika siyo bara tu bali hadi Zanzibar!
 
Mm muungano mioyoni mwa watu watanganyika na wazanzibar uliisha kufa, uko mioyoni kwa viongozi wa ccm tuu!
 
Actually most of us hate the so called muungano, it doesnt benefit tanganyikans! I hate it! It only helps zanzibaris!
 
Yaliyotokea Zanzibar leo na yale yanayoendelea ni matokeo ya kushindwa kwa utawala wa CCM kutatua matatizo ya Muungano. Lakini pia ni ishara ya kushindwa kwa viongozi wetu wa kisiasa nchini kuutetea Muungano na kujenga hoja za kwanini yapaswa uendelee. Kwa muda mrefu kikundi cha watu wachache kimekuwe kikisukumiza hoja dhidi ya Muungano na baadhi yao kuzawadiwa nafasi za uongozi licha ya msimamo wao juu ya Muungano kujulikana. Hivyo siku baada ya Muungani (A Day After the Union) itakapofika siyo Wananchi wa kawaida watakaolalamikiwa bali viongozi wale ambao wameacha siku hiyo ifike. Ukimya wa Wazanzibari wenye kuamini katika Muungano kumewachochea kundi hilo dogo. Tusije kushangaa tunashuhudia kuzaliwa kwa kikundi cha "Boko Haram" cha Tanzania!!! Yote yatakuwa ni kwa sababu ya kushindwa kwa utawala wa CCM kutoa uongozi!

Hatujasikia viongozi wa CCM wakitetea Muungano kama wanavyotetea chama chao; hatujawasikia wakiwapinga anti-unionists kwa hoja zenye nguvu bali wamekuwa wakiwapa baraza huru; na hatujawaona hata viongozi wao wa serikali - walioapa kulinda Katiba ya Muungano - wakitetea Muungano huo.

Ni kana kwamba wameshakubali kisichoepukika - kufa kwa Muungano. Sasa, kama hili ndilo wanalolitaka hakuna haja ya kuumizana, kupigana mabomu, wala kushindana. Kama kuvunjika kwa Muungano ni inevitable - basi hekima inatutaka tuweke mfumo wa kuvunja Muungano huu vizuri na kwa makusudi ili mahusiano ya kidiplomasia baina ya nchi mbili yaanze. Jamani, Muungano uwepo au usikuwepo watu wa Zanzibar hawaendi popote na watu wa bara hawaendi popote. Hata watu waombee vipi Wazanzibar wataendelea kuwepo na watu wa bara wataendelea kuwepo. Sasa kama hii ni kweli basi ni kushindwa tu kwa viongozi wetu na hasa kushindwa kwa sera zao mbovu ndiko kunakofanya mgogoro huu uwe mkubwa kuliko inavyopaswa.

Tusizungushe maneno! Kuvunjika kwa Muungano kutakuja si kwa sababu ya Uamsho au vikundi vya kidini; kutakuja kwa sababu wanasiasa wetu wameshindwa!

Well said. haya ni matunda ya viongozi wetu kuweka pamba masikioni na kujali maslahi yao binafsi. Sasa hali imefikia ambapo ndani ya nchi moja hakuna maelewano, kisa viongozi wetu hawako tayari kuongolea na kushughulikia kero za Muungano kwa hoja hafifu kwamba huko ndiko kuulinda muungano.

Hivi CCM na serikali yake itatumia nguvu ya DOLA kulazimisha vitu mpaka lini? hivi kuna ugumu gani jambo hili likijadiliwa kwa uwazi na ufumbuzi wa kudumu ukapatikana? Hivi serikali ya CCM inaamini kwamba njia sahihi ni kutumia DOLA? je mpaka lini? je Dola iliwahi kushinda nguvu za UMMA?

Inasikitisha sana na hii ni kwasababu ya AINA ya Viongozi tulionao ambao wengi wao wamepewa majukumu na mkuu wa Nchi bila kuzingatia vigezo vinavyotakiwa na badala yake Uswahiba, urafiki, undugu, ukabila, udini, n.k ndiyo vigezo vinavyotumika na sasa haya ndiyo matokeo ya Uongozi usiojua nini maana ya kuwajibika.
 
Muungano hauna tija kwangu hata chembe,,,maisha yangu kwa asilimia zote hayategemei muungano,,,leo hii sina cha kufata zanzibar,hakuna chuo useme elim ntaipata huko,hakuna hosptal useme ndo kuna ya rufaa sa apollo,hakuna ajira kule useme natifata,,,,VUNJENI MUUNGANO,NI MZIGO KWA WATANGANYIKA,TUMEWASAIDIA VYA KUTOSHA HAWA WAPEMBA
 
303313_10150805900486176_721596175_9887001_1467272456_n.jpg
 
Mwanakijiji, tatizo kubwa la viongozi wetu waliopo madarakani ni hisia kwamba kila mmoja anahisi viongozi wa pande nyingine ya muungano wanwapunguzia nafasi zao za kuongoza, mawazo ni kwamba muungano ukivunjika basi watakuwa na nafasi zaidi. Ombi letu kwao, hatuhitaji kugeuka Sudan kusini na kaskazini, wavunje muungano huu kwa amani (kama ni lazima kama wanavyofikiri) ili tuendelee kuishi kidugu hatuhitaji mapambano kwa faida zao!!
 
Mwanakijiji, tatizo kubwa la viongozi wetu waliopo madarakani ni hisia kwamba kila mmoja anahisi viongozi wa pande nyingine ya muungano wanwapunguzia nafasi zao za kuongoza, mawazo ni kwamba muungano ukivunjika basi watakuwa na nafasi zaidi. Ombi letu kwao, hatuhitaji kugeuka Sudan kusini na kaskazini, wavunje muungano huu kwa amani (kama ni lazima kama wanavyofikiri) ili tuendelee kuishi kidugu hatuhitaji mapambano kwa faida zao!!
 
muungano uvunjike...hakuna kuumizana wala kuumiza vichwa hapa...
 
Yaliyotokea Zanzibar leo na yale yanayoendelea ni matokeo ya kushindwa kwa utawala wa CCM kutatua matatizo ya Muungano. Lakini pia ni ishara ya kushindwa kwa viongozi wetu wa kisiasa nchini kuutetea Muungano na kujenga hoja za kwanini yapaswa uendelee. Kwa muda mrefu kikundi cha watu wachache kimekuwe kikisukumiza hoja dhidi ya Muungano na baadhi yao kuzawadiwa nafasi za uongozi licha ya msimamo wao juu ya Muungano kujulikana. Hivyo siku baada ya Muungani (A Day After the Union) itakapofika siyo Wananchi wa kawaida watakaolalamikiwa bali viongozi wale ambao wameacha siku hiyo ifike. Ukimya wa Wazanzibari wenye kuamini katika Muungano kumewachochea kundi hilo dogo. Tusije kushangaa tunashuhudia kuzaliwa kwa kikundi cha "Boko Haram" cha Tanzania!!! Yote yatakuwa ni kwa sababu ya kushindwa kwa utawala wa CCM kutoa uongozi!

Hatujasikia viongozi wa CCM wakitetea Muungano kama wanavyotetea chama chao; hatujawasikia wakiwapinga anti-unionists kwa hoja zenye nguvu bali wamekuwa wakiwapa baraza huru; na hatujawaona hata viongozi wao wa serikali - walioapa kulinda Katiba ya Muungano - wakitetea Muungano huo.

Ni kana kwamba wameshakubali kisichoepukika - kufa kwa Muungano. Sasa, kama hili ndilo wanalolitaka hakuna haja ya kuumizana, kupigana mabomu, wala kushindana. Kama kuvunjika kwa Muungano ni inevitable - basi hekima inatutaka tuweke mfumo wa kuvunja Muungano huu vizuri na kwa makusudi ili mahusiano ya kidiplomasia baina ya nchi mbili yaanze. Jamani, Muungano uwepo au usikuwepo watu wa Zanzibar hawaendi popote na watu wa bara hawaendi popote. Hata watu waombee vipi Wazanzibar wataendelea kuwepo na watu wa bara wataendelea kuwepo. Sasa kama hii ni kweli basi ni kushindwa tu kwa viongozi wetu na hasa kushindwa kwa sera zao mbovu ndiko kunakofanya mgogoro huu uwe mkubwa kuliko inavyopaswa.

Tusizungushe maneno! Kuvunjika kwa Muungano kutakuja si kwa sababu ya Uamsho au vikundi vya kidini; kutakuja kwa sababu wanasiasa wetu wameshindwa!

mkuu wa magogoni anamaliza kipindi chake kwa style ya kipekee. sisiem inakufa mikononi mwake na muungano unavunjika mbele yake. mwl. JK atakuwa na hasira sana huko aliko.
kwanini JK anapiga kimya!!!!!!!!! ndo mambo ya kufa na tai shingoni - kwa manufaa ya nani?
Tatizo alijifanya kidume kuwaweka pembeni wastaafu (Mkapa, Mwinyi and others) na kung'ang'ania wana mtandao. hakujua mtandao ulikuwa na nia moja tu ya kurudisha jasho lao baada ya ushindi (ufisadi). Ukishanyea kambi, utarudi tena ukanyage makimba yako!!? na amini kabisa wastaafu wanashangilia jamaa anavyosulubiwa.
Kufa na tai shingoni si suluhisho - aombe msaada hata kwa viongozi wapinzani. wapinzani pia ni watanzania wanaopenda Taif lao. hakuna uadui hapa ktk suala lenye maslahi kwa Taifa. Tabia yake ya chuki na visasi haijengi hata siku moja.
 
CC na hata NEC ya CCM ilikutana lakini wakaishia kuunda mikoa ya chama chao vyuo vikuu. Maalim Seif aliposema waziwazi kuwa lazima Zanzibar iwe na sarafu yake hakuna kiongozi alihoji? Na hakuna asiyejua kuwa Maalim Seif akisaidiwa na Jusa ni ndio vinara wa hizi harakati. Huko nyuma (wakati wa campaign nadhani ilikuwa 2005) kiongozi mmoja wa CUF akihutubia wananchi alisema hivi '... huu utakuwa ni mwisho ngozi nyeusi kutawala"
 
Kwa sababu kubwa mbili:

a. It is a bad precedence
b. Zanzibar was not annexed or forced into the union.

c. They are afraiding that once the referendum favours the end of the union, they will be painted as leaders who killed the union. No CCM leader want that to happend under his watch!. That's why you will always hear them 'I will protect the union' - Means using forces

Protection of the union cannot be done by tear gases or live ammunitions, but by making it pleasant to everyone!. You cannot say you are going to bath but don't want water to touch certain part of your body, that's not bathing. If you want to enact a new constitution, then everyview should be on the table whether its negative or positive on your side.
 
muungano uvunjike...hakuna kuumizana wala kuumiza vichwa hapa...
Sidhani Hilo ndio **** letu! Uongozi unapokaa na kudhani wanaweza kufikiria na Kamugisha masuala muhimu ya jamii kwa niaba ya wananchi bila ridhaa yao ndio musings aw matatizo yote.

Kwa nini wanna hi wasiruhusiwe kuhoji muungano? Kuhoji sio kusema hakutakuwepo muungano bali ni Njie bora ya kupata mwafaka mzuri wa muungano unaohitajika. Mh Kikwete alifanya kosa kubwa kuonya kuhoji muungano.
 
Back
Top Bottom