Kigarama
JF-Expert Member
- Apr 23, 2007
- 2,492
- 1,230
Kuna mitazamo tofauti kuhusu ni kwa nini msajili wa vyama vya siasa nchi hataki kukisajili Chama Cha Jamii (CCJ).
Kwa mitazamo yangu na uchunguzi binafsi ndani ya ngazi za juu za uongozi wa CCM nimefikia kuamini kuwa hofu ya CCM si chama chenyewe cha CCJ bali ni Jina la chama hicho.
CCM kwa miaka mingi tangu mwaka 1995 imekuwa ikifaidika kuwekwa mwanzoni mwa karatasi ya kupigia kura kwenye kila uchaguzi kutokana na jina lake kuwa na herufi inazoipa nafasi ya kialfabeti kukaa mwanzoni mwa karatasi za kupigia kura. Kwa kusajliwa kwa CCJ nafasi hiyo ya kukaa mwanzoni mwa karatasi ya kupigia kura itapotea.
Kama utafiti wa REDET ulivyowahi kuonyesha ni kwamba wanaoichagua CCM wengi wao ni wale wasiojua kusoma na kuandika, kwa hiyo ilikuwa ni rahisi kwa CCM kuwaelekeza kwamba kazi yao ni kumchagua mgombea ambaye picha yake ni ya kwanza kwenye karatasi ya kupigia kura, sasa CCJ ikisajiliwa itakuwaje?
Kwa hivyo hofu ya CCM siyo kwenye nguvu ya CCJ kama chama bali ni nguvu ya kiuchawi wa kialfabeti (Alphabetical Magic) iliyonayo CCJ kwa kuwa "J" imeitangulia "M" katika alfabeti. kwa maana nyingine kama CCJ ikisimamisha mgombea wa Urais basi jina na picha yake vitamtangulia yule wa CCM (Kikwete?)
Kwa mitazamo yangu na uchunguzi binafsi ndani ya ngazi za juu za uongozi wa CCM nimefikia kuamini kuwa hofu ya CCM si chama chenyewe cha CCJ bali ni Jina la chama hicho.
CCM kwa miaka mingi tangu mwaka 1995 imekuwa ikifaidika kuwekwa mwanzoni mwa karatasi ya kupigia kura kwenye kila uchaguzi kutokana na jina lake kuwa na herufi inazoipa nafasi ya kialfabeti kukaa mwanzoni mwa karatasi za kupigia kura. Kwa kusajliwa kwa CCJ nafasi hiyo ya kukaa mwanzoni mwa karatasi ya kupigia kura itapotea.
Kama utafiti wa REDET ulivyowahi kuonyesha ni kwamba wanaoichagua CCM wengi wao ni wale wasiojua kusoma na kuandika, kwa hiyo ilikuwa ni rahisi kwa CCM kuwaelekeza kwamba kazi yao ni kumchagua mgombea ambaye picha yake ni ya kwanza kwenye karatasi ya kupigia kura, sasa CCJ ikisajiliwa itakuwaje?
Kwa hivyo hofu ya CCM siyo kwenye nguvu ya CCJ kama chama bali ni nguvu ya kiuchawi wa kialfabeti (Alphabetical Magic) iliyonayo CCJ kwa kuwa "J" imeitangulia "M" katika alfabeti. kwa maana nyingine kama CCJ ikisimamisha mgombea wa Urais basi jina na picha yake vitamtangulia yule wa CCM (Kikwete?)