Tuna kesi nzuri sana dhidi ya hawa wezi hata katika mahakama za Kimataifa tutashinda maana huku siyo kuinvest bali ni kuiba. Tukakusanye ushahidi wa mikataba ya wenzetu ya uchimbaji wa madini yao kule Ghana, South Africa na Botswana na mikataba hiyo yote ina maslahi na nchi za wenzetu. Kama hawa wezi hawataki kutii sheria zetu za uwekezaji basi wamwage FFU katika machimbo yote ya madini na hakuna kuendelea kuchimba mpaka wakubali au wafunge virago vyao na asilimia kubwa ya Watanzania wataunga mkono uamuzi kama hao kwa nderemo na vifijo. Wakati umefika sasa wa kutetea maslahi ya nchi yetu bila woga wa aina yoyote ile.