Kiby
JF-Expert Member
- Nov 16, 2009
- 6,897
- 4,620
Kukosekana kwa utawala wa sheria kunaligharimu sana bara la Africa. Border ya Kasumbaresa kwa sasa imefungwa kwa sababu ya raia wa Kongo kumchoma moto pamoja na track lake dereva mmoja wa Zambia. Dereva huyo akiendesha gari upande wa kungo alikutana na umati uliokuwa ukitoka kuzika na kuuparamia na kusababisha kifo cha watu watatu. Jambo lililopelekea wanakijiji hicho kulichoma moto gari na dereva akiwa amejifungia ndani. Sasa hivi kinachoendelea ni wakongo wamesimama upande wa kwao wakiwa wameshikilia mawe baada ya kupigwa marufuku kuingia upande wa zambia ambako kimsingi ndiko kuliko na biashara yao inayowapatia mlo wa kila siku. Msururu wa matraki pande zote unakaribia kilometa tano kwa urefu.
My take: Huku kukosekana kwa utawala wa kisheria katika nchi zetu za Africa hatuoni kunatugharimu sana kwa kuzuia maendeleo yetu kama siyo kuyarudisha nyuma?
.
My take: Huku kukosekana kwa utawala wa kisheria katika nchi zetu za Africa hatuoni kunatugharimu sana kwa kuzuia maendeleo yetu kama siyo kuyarudisha nyuma?
.