Scolari Ndenga
JF-Expert Member
- Aug 4, 2008
- 271
- 43
Operesheni Sangara ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA inayoendelea mkoani Morogoro imeendelea kuwa mwiba mchungu kwa CCM na serikali baada ya viongozi wa serikali za vijiji mbalimbali kuamua kujiuzulu nyadhifa zao na kujiunga na CHADEMA. Walioamua kujiuzulu nayadhifa zoa ni pamoja na aliyekua katibu mwenezi wa CCM kata ya Muhonda Mzee Ngoya, Mwenyekiti wa serikali ya kitongoji cha Kododo kata ya Luwale bwana Charles Kiwaga, Mwenyekiti wa serikali ya Mlali Lucas Membe na Alexander John wa kijiji cha Ng'ungulu. Katibu mwenezi wa kata ya Luwale na Mwenyekiti wa Kitongoji kupitia CCM walijiuzulu nyadhifa zao mbele ya Katibu Mkuu wa BAVICHA, Deogratias Munishi na kukabidhiwa kadi za CHADEMA kama inavyoonekana hapa H@ki Ngowi: Operesheni Sangara Ya Chadema ndani ya Mvomero-Morogoro Yazidi Kupasua Vijiji! Wakati CHADEMA ikiendelea kuchanja mbuga ya kuhamasisha wananchi kijiji kwa kijiji na ikitarajia kufunga operesheni yake kwa maandamano makubwa na ya kihistoria mjini Morogoro tarehe 27/08/2012, kwa upande wake Chama Cha Mapinduzi kinahaha kuhakikisha mikutano ya mjini Morogoro ukiwamo na ule wa kufunga haufanikiwi. Wiki iliyopita, katibu wa itikadi na uenezi wa chama hicho Nape Nnauye kwa kile kilichoitwa kuwafuturisha mabalozi wa CCM wa mjini Morogoro, aliagiza mabalozi hao kufanya juu chini ili CHADEMA wapate aibu ya mwaka ikiwamo kuandaa vijana wa CCM watakaovaa Kombati za CHADEMA wafanye vurugu katika mikutano hiyo. Katika kuweka msisitizo wa mbinu chafu hizo, tarehe 21/08/2012, mweka hazina wa CCM ambaye anadaiwa na CHADEMA kukodisha vijana wahuni kutoka manzese Dar es Salaam walifanya vurugu katika mikutano ya chama hicho mkoani Singida mwezi wa saba mwaka huu, Mwigulu Nchemba alikua mkoani Morogoro kusuka mipango hiyo ya kuihujumu CHADEMA jambo linaloonekana kushindwa mpaka sasa hivi.