Kilwa Road baada ya kumalizika imeanza kuharibika!

BARABARA ya Kilwa jijini Dar es Salaam itarudiwa kujengwa upya baada ya kubainika haina kiwango. Mkandarasi ambaye ni Kampuni ya Kajima kutoka Japan iliyohusika katika ujenzi huo, imeomba radhi baada ya kubainika kuwa ndiyo yenye makosa na itaijenga upya kwa gharama zake. Pamoja na kampuni hiyo kuomba radhi Kampuni Mshauri wa mradi, Ingerosec ameondolewa.

Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli na Balozi wa Japan nchini, Hiroshi Nakagawa walitoa taarifa hiyo jana kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam. Uamuzi huo unatokana na matokeo ya timu iliyoundwa kwa kushirikisha Shirika la Maendeleo la Japan (Jica), Kampuni ya Kajima, Ing’erosec, Wakala wa Barabara (Tanroads) na wataalamu baada ya kuonekana kuwa barabara haina ubora.

Timu hiyo iliyofanya kazi yake kwa takribani miezi mitatu, iliundwa baada ya kukutana na Balozi wa Japan. Serikali ya Japan ndiye mdhamini wa mradi huo wa ujenzi wa kilometa 10.1 za barabara hiyo iliyogharimu Sh bilioni 30. Wadau hao walikagua na kugundua kuwa barabara haikuwa katika kiwango. “Walikaa wakakubaliana, Balozi ameleta barua, Kajima amekubali barabara itarudiwa upya, wameomba radhi,” alisema Dk. Magufuli. Serikali imempa mkandarasi Kajima miezi miwili afanye upembuzi wa mradi na Oktoba 20, mwaka huu awasilishe taarifa ya maeneo yaliyolipuliwa kujengwa kabla ya kazi kuanza.

http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?n=20906
 
Habari njema, lakini SOURCE PLS!!!

Hatuna budi kumpongeza mhe.Magufuli kwani ameonesha tunaweza kuikataa mikataba iliyo chini ya viwango tatizo wengine wakipozwa basi kesi kwisha na wanasaini kupokea miradi iliyosub standard.
SOURCE TAARIFA YA HABARI ITV SAA 2 USIKU 30/08/2011
 
Mh. Kikwete kupongezwa kwa hili ni jambo jema na ni stahili yake, kama tu vile anavyopaswa kukosolewa na kubebeshwa lawama za kero na adha zisizopungua zitokanazo na ukosefu wa maadili ya uongozi ya watumishi mbalimbali aliowateua na ulegelege uliodhahiri katika majukumu yake mengi hapa nchini!!

Kupongezwa kwa lipi hasa? Ripoti za kiwango duni cha barabara hii zilianza kutolewa siku nyingi tangu kazi ilipofikia asilimia 20. Muda wote huo JK na serikali yake walikuwa wapi hadi kuaachia mambo shaghalabagala hadi mwisho ndiyo wanazinduka? Why? Wangemshtusha mkandarasi tangu awali, si kungoitokea yote haya -- ucheleweshaji wa barabara.
 
Yaani ujenzi wa hii barabara ulivyokuwa una sababisha kero wakati ule kama kero ile itarudi tena basi ni bora kubaki na hii ya kiwango cha chini. Niliwahi kukaa kwenye foleni masaa saba nikitokea mkuranga. Toka siku hiyo sikuwahi tena kupita barabara ile mpka ilipomalizika.

Hivi kweli hizo pesa ni msaada au mkopo?
 
Mh John Magufuli songa mbele onesha njia - Jua hamko wengi na watz wanawahitaji -your actions speak louder words
 
pamoja na kump0a pongezi tele kaka Magufuli, kuna haja ya kuwawajibisha USALAMA WA TAIFA! kwani wao walikuwa wapi hadi barabara inakamilika?

nawapa pole wakazi wa lindi na mtwara kwani wahuni wanawarudisha nyuma maenedeleo yenu kwa kuwafanya mtumie masaa mengi barabarani!
 
Kupongezwa kwa lipi hasa? Ripoti za kiwango duni cha barabara hii zilianza kutolewa siku nyingi tangu kazi ilipofikia asilimia 20. Muda wote huo JK na serikali yake walikuwa wapi hadi kuaachia mambo shaghalabagala hadi mwisho ndiyo wanazinduka? Why? Wangemshtusha mkandarasi tangu awali, si kungoitokea yote haya -- ucheleweshaji wa barabara.


Hii ni kituko kingine cha serikali ya CCM, sishangai sana swala la barabara kurudiwa kwa gharama za mkandarasi, kama sikosei miaka ya 90 kampuni ya kijapan Kajima ilirudia kipande cha barabara ya Salendar baada ya makabidhiano barabra hiyo iliharibika kuna sehemu ilitoboka(sijui kwa nini) lakini ilirudiwa kwa gharama zisizokuwa za serikali, pia kama sikosei mradi mwingine wa msaada wa Japan maeneo ya Namanga kulikuwa na lami iliumuka na ilibidi irudiwe, yote haya yalifanyika wala hatukusikia mtu akipongezwa,

katika mfumo wa serikali ya Japan misaada yao yote husimamiwa na wao (Japan) na design hufanywa na wao hata contractor huchaguliwa na wao wenyewe, kwanini inakuwa hivi, jibu ni jepesi hawana imani na sisi, na ni haki yetu kupata kilicho bora hata kama ni msaada,

Zote hizi ni hasira za wizara ya miundo mbinu na tanroads kuwa hizo fedha hazikupitia mikononi mwao laiti kama zingelipitia kwao yote haya tusingeli yajua , kuna barabara nyingi ambazo tumezijenga wenyewe kwa fedha zetu wenyewe na viwango vyake ni dhaifu mno lakini hatusikii kelele zozote, mfano mzuri ni ile barabara inayopita kwao Magufuli, ilijengwa na contractor wa kichina ilikuwa na kiwango kisicho sitahili lakini hadi leo kimya contractor aliondoka na kuacha mashimo, laikini badala yake tumeona contractor mwingine wa kichina akiitengeneza kwa gharma za serikali, mfano mwingene ni barabara ya MZA-SHYNGA border, baada ya makabidhiano barabara hiyo iliharibika na inatengenezwa kwa gharama zetu wenyewe,

nilimsikia Waziri Maghufuli kuwa hata thickness ya subase na lami ilikuwa chini ya specification, inaeleweka kuwa kwa kila malipo inatakiwa uthibisho wa kile kilicho fanyika ili iwe stahili ya malipo ( certificate), sasa yote haya ilikuwaje hayakuzingatiwa na contractor aliruhusiwa aendelee na kazi, hata wasimazi upande wa mteja ambao ni serikali walikuwa wapi, ni hatua gani zimechukuliwa dhidi yao, nafikiri hii inibua maswali mengi kuliko majibu
 
Wakuu habari hii nimeishuhudia kwenye taarifa ya habari ya saa mbili usiku ya TBC1 kwamba Waziri wa Ujenzi Mhe. Magufuli ameandaa operesheni kabambe ya kuondoa gereji zote zilizo ndani ya hifadhi ya barabara. Kwa mujibu wa Magufuli mwenyewe maandalizi ysliyofanyika ni pamoja na kuandaa askali wa FFU watakaoendesha zoezi zima. Mhe. Magufuli amesema kupitia operesheni anataka kutoa fundisho kws watanzania kuhusu umuhimu wa kuheshimu sheria.

Haya wenye gereji zilizo ndani ya hifadhi ya barabara kaeni mkao wa kula!
 
Wakuu habari hii nimeishuhudia kwenye taarifa ya habari ya saa mbili usiku ya TBC1 kwamba Waziri wa Ujenzi Mhe. Magufuli ameandaa operesheni kabambe ya kuondoa gereji zote zilizo ndani ya hifadhi ya barabara. Kwa mujibu wa Magufuli mwenyewe maandalizi ysliyofanyika ni pamoja na kuandaa askali wa FFU watakaoendesha zoezi zima. Mhe. Magufuli amesema kupitia operesheni anataka kutoa fundisho kws watanzania kuhusu umuhimu wa kuheshimu sheria.

Haya wenye gereji zilizo ndani ya hifadhi ya barabara kaeni mkao wa kula!

Sawa ni maamuzi mazuri lakini pia ninatumani hatakuwa kiongozi bora kama hata kuwa amewapa taarifa hao
wausika ili watoe mali zao kwa hiari, sio muda wote kutumia nguvu

nakubaliana naya mia kwa mia lakini wapewe muda wa kuhama hawa watu wanajijenga kiuchumi lakini pia na sisi wateja wao tunawaitaji kujua watakua wapi, tuwe tunaangalia na effect nyingine
 
subiri pinda na jekei,watakavyowakingia kifua.Jamaa wanahofia kufunikwa kwa ulegelege wao
 
Huyu ndie anafaa kuwa PM wacha Pinda anakaa analia lia tuuu iiii uiiiiii,,,albinoooooo iiiii...why usikamate muuaji afungwe unalia NATO ikishusha bomu kama Libya si utazimia?!!
 
Hatimaye kampuni ya Kijapani Kajima Construction Company iliyoboronga vibaya sana katika ujenzi wa bârabara yenye urefu wa kilomita 10 ya Kilwa jijini Dar es Salaam imeomba radhi nakukubali kuifanyia marekebisho makubwa kuanzia mwezi wa kumi. Hayo yalitokea baada ya waziri wa ujenzi kuwashikilia bango wakandrasi hao nakukataa katakata makabidhiano ya barabara hiyo.

Ripoti ya pamoja iliyotolewa na wataalamu wa maswala ya ujenzi waliokagua mradi huo kutoka Japan International Co-operation (JICA) Tanzania Roads Agency (TANROADS) na Wizara ya Ujenzi ilitanabaisha mapungufu makubwa ya kiufundi na kiuhandisi yaliyofanywa na kampuni ya Kajima.

Wanajamvi sipati picha kampuni hii ndiyo ileile iliyojenga Morogoro road ni vigumu kuamini Kajima ya sasa ilibidi ifumue nakujenga upya mizunguko (round about) yote pale misheni mpaka leo daraja kila wakijenga linabomoka ama kweli tumechezewa.
Source: Daily News
 
Huyu ndie anafaa kuwa PM wacha Pinda anakaa analia lia tuuu iiii uiiiiii,,,albinoooooo iiiii...why usikamate muuaji afungwe unalia NATO ikishusha bomu kama Libya si utazimia?!!
<br />
<br />
Acha kuzimia atafariki kabisa.
 
Wakuu habari hii nimeishuhudia kwenye taarifa ya habari ya saa mbili usiku ya TBC1 kwamba Waziri wa Ujenzi Mhe. Magufuli ameandaa operesheni kabambe ya kuondoa gereji zote zilizo ndani ya hifadhi ya barabara. Kwa mujibu wa Magufuli mwenyewe maandalizi ysliyofanyika ni pamoja na kuandaa askali wa FFU watakaoendesha zoezi zima. Mhe. Magufuli amesema kupitia operesheni anataka kutoa fundisho kws watanzania kuhusu umuhimu wa kuheshimu sheria.
Haya wenye gereji zilizo ndani ya hifadhi ya barabara kaeni mkao wa kula!

Mawaziri wengine waige! japokewa kuigaiga napo bila kuwa creative inapoteza muelekeo! wivu wa maendeleo ndio unaotakiwa! kama tungekuwa na mawaziri watono hivi wa aina hiyo yaani wenye ujasiri wa kufanya maamuzi aggressive bila kuogopa kivuli namna hiyo mambo yangebadilika!
 
Hicho ndicho kinachonifanya nimhusudu Magufuli. Mara kadhaa amejaribu kufanya maamuzi magumu kwa faida ya wananchi wengi huku akitekeleza matakwa ya sheria. Tungekuwa na angalau robo ya mawaziri wenye ujasiri huo, tusingekuwa hapa tulipo leo.
 
Wandugu,

I am just thinking loudly, hivi kwa nini isitokee jeikei akamteua Mhe. Pombe Magufuli kuwa waziri wa nishati na madini ili apunguze uzembezembe wa kipuuzi unaofanywa katika sekta hiyo? Mimi naamini kabisa kwamba Mhe. Magufuli anaweza kuleta changes kwenye sekta hii muhimu kwa ustawi wa taifa letu. Najua baadhi ya mapungufu ndani ya shirika muhimu kama la tanesco yanaweza kumalizwa na u-serious wa waziri tu.

Mnaonaje jamani.
 
Pamoja na kuwa na mishemishe zake,ila ana chembe ya huruma na uzalendo. Tatizo ni mazingira ya kazi ya sasa! Atakubaliana na kila mtu maana uteuzi nyingi zinaendana na kulipa fadhila siku hizi.
 
Magufuli is not the leader you all think he is. Anajua tu kujionyesha mbele ya media. Ila ukiangalia wizara zote alizo pitia rushwa zilikithiri na wala hakuwezi kupunguza. Generally speaking haja fanya kitu chochote kikubwa bali anajua kujionyesha kwenye yale madogo anayo yafanya.
 
Back
Top Bottom