MJADALA: Maswali, majibu na ushauri kuhusu Kilimo cha Mpunga cha kitaalam pamoja na masoko yake

Asante mdau. Kwahiyo nikikomaa na kilimo cha mpunga naweza pata pesa ya ya kujikimu sio?
Zaidi ya pwani mkoa gani mwingine naweza pata kwamba la kukodi kwa being raisi.
Asante sana!

Ndugu yangu Robbinhood Kilimo cha mpunga kitakachokuinua ni kile cha kwenye maeneo yenye umwagiliaji.

Huko ukishamailiza kupandikiza mpunga wako hesabu hiyo ni hela au ni chakula tayari!

Achana na kilimo cha kutegemea mvua utalia siku zote! Mkoa wa Morogoro kuna maeneo kupanda na kuvuna ni mwaka mzima, hakuna eti umechelewa msimu, watu wanapanda tu mwaka mzima.

Wanaoongelea kuchelewa msimu ni kwa kilimo cha kutegemea mvua. Mashamba ya kukodi ni mengi na bei ni nzuri tu. Kuna maeneo si utani, bei ya kukodi na ya kununua hakuna tofauti, tembea ujionee!
 
@Robbinhood,
Robbinhood, kilimo cha mpunga wa umwagiliaji ni cha uhakika. Risk zake ni pale serikali inapozuia uuzaji mchele nchi za nje, hapo bei hudoda kabisa! Risk nyingine ni kulima eneo lenye mkondo wa mafuriko, huko watu hupata hasara!

Na risk nyingine ni ndege na panya kuna misimu hutokea mlipuko wa hao viumbe ambapo wakulima hukimbia mashamba. Ndege wakiwa wengi hata watu 3 kwa ekari moja huweza kutoka povu mdomoni kwa kukimbia huku na kule kufukuza ndege!

Ukilima kiangazi peke yako kwa umwagiliaji maeneo yenye wafugaji wa Kimasai jua unawatayarishia malisho! Watakuja kuingiza mifugo yao mchana kweupe na mwenyewe ukishuhudia kwa macho yako! Chezea masai wewe!!??

Mpunga unafaida kubwa hasa ukiangalia bei ya mchele sokoni hivi sasa, ukistawisha ipasavyo kwenye mashamba ya umwagiliaji kwa kufuata maelekezo ya wataalamu unapaswa upate kuanzia gunia 25 kwa ekari moja!

Kila gunia ukikoboa ukapata kilo 70 za mchele ukauza bei ya jumla 1500/= wakati wa uhaba, ekari moja unapata sh 2.6 Millioni!

Gharama ya kutunza shamba hadi kuingiza nyumbani Dakawa Morogoro ilikuwa sh 550,000/= mwaka 2011! Sijui msimu uliopita hali ilikuwaje! Kwa hiyo utaona faida ni kubwa tu hasa ukilima eneo kubwa!!

Wengi tunafahamu kuwa mchele umekuwa ukiuzwa sokoni rejareja kwa bei kubwa tu! Inawezekana kabisa kuvuna hata zaidi ya magunia 35 kwa ekari iwapo utaalamu utatumika na kutambua misimu yenye mavuno makubwa!

Wakulima wazoefu kutoka maeneo ya umwagiliaji watakubaliana kabisa na maelezo haya!!! Hii siyo hadithi ya machungwa 4,000 kwa mchungwa wa miaka 3 nooo!!! It is real!!
 
Mkuu japo suala la bei na risk siwezi kuongele chochote ila maeneo mazuri kwa kilimo cha mpunga ni IFAKARA ukiwa unaelekea wilaya ya MAHENGE ukishavuka tu mto kilombero kuna eneo wenyeji wanaliita mashambani...

Ni eneo zuri sana kwa mpunga na linakubali mpunga kweli kweli, pia kuna ardhi ya kutosha na maji ya kutosha pia, kwa suala la soko la bidhaa ni rahisi sana kusafirisha kuja DAR ES SALAAM....
 
Asante maji moto kwa ukarimu wako nimenyonya chapisho la kilimo cha mpunga
 
Kubota,
Aise asante sana mdau. Nashukuru kwa kunipa mwangaza. Naona hii ni idea Nzuri na sio ya kubahatisha. Ntakutafuta tuongee zaidi.
 
Ndugu yangu Robbinhood Kilimo cha mpunga kitakachokuinua ni kile cha kwenye maeneo yenye umwagiliaji. Huko ukishamailiza kupandikiza mpunga wako hesabu hiyo ni hela au ni chakula tayari! Achana na kilimo cha kutegemea mvua utalia siku zote! Mkoa wa Morogoro kuna maeneo kupanda na kuvuna ni. mwaka mzima, hakuna eti umechelewa msimu, watu wanapanda tu mwaka mzima. Wanaoongelea kuchelewa msimu ni kwa kilimo cha kutegemea mvua. Mashamba ya kukodi ni mengi na bei ni nzuri tu. Kuna maeneo si utani, bei ya kukodi na ya kununua hakuna tofauti, tembea ujionee!
.
Sawasawa kamanda. Kwahiyo unanishauri nikajikite morogorokuliko kwenda mbeya AU mkoa mwingine sio?!. Ubarikiwe sana
 
Mkuu japo suala la bei na risk siwezi kuongele chochote ila maeneo mazuri kwa kilimo cha mpunga ni IFAKARA ukiwa unaelekea wilaya ya MAHENGE ukishavuka tu mto kilombero kuna eneo wenyeji wanaliita mashambani.

Ni eneo zuri sana kwa mpunga na linakubali mpunga kweli kweli, pia kuna ardhi ya kutosha na maji ya kutosha pia, kwa suala la soko la bidhaa ni rahisi sana kusafirisha kuja DAR ES SALAAM....

Asigwa. Nashukuru sana kwa USHAURI wako. Shukrani
 
Mi nina uzoefu kwa iringa...gharama zote (kwa ekali)mpaka kufikisha mpunga store ni kama ifuatavyo:
'000'
1. Kukod shamba-100
2. Mbegu-11
3. Kuvuruga-80
4. Kurembeka-80
5. Kung'olea-60
6. Kufyeka-40
7. Kupga-40
8. Mfanyakaz-200
9. Mengneyo-150
JUMLA = 761
Ni kaz ya miez 7 (januar to july ) na hapo una uhakika wa kupata gunia ishirini mpaka ishirin na tano(20-25) zenye thaman ya 2000. Hvyo chukua hzo 2,000,000 toa 761,000 unapata 1,239,000/ekari,.. karibuni
 
NOTE:makadirio hayo hayatofautiana sana sehem na sehem yan kama tofaut ni ndogo sana hasa kwa maeneo yanayohitaji madawa na mbolea,kwa iringa hakuna mbolea wala madawa
 
Ni kaz ya miez 7 (januar to july ) na hapo una uhakika wa kupata gunia ishirini mpaka ishirin na tano(20-25) zenye thaman ya 2000. Hvyo chukua hzo 2,000,000 toa 761,000 unapata 1,239,000/ekari,.. karibuni

2,000,000 kwa gunia ishirini ni wastani wa gunia sh 100,000, hii ni bei ya shambani au ukipeleka mjini(usafiri hujaweka) au ukihifadhi na kuuza baadae(hujaweka gharama ya kuhifadhi)?
 
Alex Mponela,

Kupitia kwenye uzi huu kuna kitu ningeomba kutoka kwako, hasa hasa juu ya hili la kununua mchele badala ya kulima, vipi naweza kuelezea kimahesabu? ie Gunia moja la mchele/mpunga ni bei gani kipindi cha mavuo, ukusanyaji mzigo unaweza kuchukua siku ngapi kwa gunia kama 500, gharama za ghala ziko vipi, usafiri wa kupeleka ghalani na bei ya kuuza siku ya mwisho ni wastani gani.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom