Kisima
JF-Expert Member
- Oct 8, 2010
- 4,094
- 4,396
mkuu nashukuru sana,
Tupo pamoja!
mkuu nashukuru sana,
Naomba unijibu unayo miembe na miashoki??
mitiki ndo nini wakuu na mimi nitoe ushauri!.
Mimi nimejikita kwenye mitiki, syprus(carribeae} na misila.
Mkuu, unapatikana wapi?
katika mbegu ambazo ninaweza kuziandaa ni za mitiki hadi kupanda kitaluni
Mbegu zote unaweza kuandaa kama unao muda wa kutosha.
Kuhusu mashamba inategemea na sehemu husika ila kwa Moro&Tanga(mitiki) changamoto kubwa ni wafugaji tu bei iko chini. Kwa syprus nenda Iringa au Sengerema ila changamoto ni upatikanaji wa eneo kubwa mahala pamoja na bei ipo juu sana.
Nipo Moro mkuu.
Mkuu kisima..hapo Moro uko maeneo gani?na kama hutojali naweza pata eneo la bei rahisi kwa kilimo na ufugaji...
Mkuu Kilimo mitiki inastawi ukanda wote wa pwani, kwa mikoa ya pwani, moro na tanga ndipo mahala pake haswaa kwa upandaji wa mitiki. Maeneo ya baridi kali mitiki haikui haraka na hudumaa.
15+ yrs mkuu, kama umeamua kujikita kwenye kilimo cha miti nakushauri upande na pines, cyprus, msila etc hii inavunwa mapema kuliko mitiki, japo mitiki ni habari nyingine interms of thamani.
Hizo ni ndani ya miaka kumi mkuu unalamba hela, cyprus&pine ni tsh50k kwa chupa ya ml350 zipo punje zaidi ya 2k ntakupa njia ya kuziandaa kwajl ya kuweka kitaru.
Msila debe1 la mbegu ni sh50k.
Ondoa hiyo mikorosho yote kisha lima kwa trekta hallow then tafuta miche ya mitiki upande 2.5metres apart&each. So kwenye ekari1 utakuwa na miche 640.
Ukitaka stamp za hii miche nitafute mimi kwa shehena yoyote ile bei sh 250 haipungui.
Kama upo ukanda wa pwani kipindi kizuri cha kupanda ni kuanzia 15th march.
Kisima naomba mawasiliano yako nataka miche ya mitiki
NshakuPM mkuu!