Kilimo cha Kisasa: Jihadharini na vijana Matapeli/Makanjanja

Nkobe

JF-Expert Member
Feb 17, 2013
2,162
3,162
Wana JF naliongea hili kwa masikitiko makubwa kutokana na hii tabia ya vijana wa Kitanzania. Baadhi ya vijana wa Kitanzania wamegeuka kuwa watafuta maisha kwa njia ambazo haziwezi kuwa na matunda kwa taifa hili wala kwa wao. Vijana wamekuwa wakitaka maisha ya Short cut sana.

Hapa naongelea swala la kilimo. Kumetokea vijana ambao wanakwenda Kenya, wanapata mafunzo ya muda mfupi ya kilimo cha kisasa ikiwemo kilimo cha greenhouse, ufugaji wa samaka wa kisasa nk. Badala ya vijana kujitahidi kuanzisha kilimo cha kisasa wanageuka na kujifanya wataalam "Ukanjanja".

Wakipata mafunzo ya Muda mfupi baada ya hapo ujitangaza kuwa wao ni wataalam wa kilimo cha Greenhouse. Vijana wanageuka kuwa Madalali wa wauza Greenhouse badala ya wao kujikita katika kilimo. Nasema hii baada ya kuona watu wengi wakipata hasara kutokana na kudanganywa juu ya gharama za kujengewa Greenhouse.

Inapotokea hawa vijana wakafanikiwa kukudanganya kuwa wao ni wataalam baadhi ukimbilia Kenya kuleta wajenzi, au wao wenyewe kwa kubahatisha uhamua kukujengea, pia wanakuchaji pesa nyingi sana kupita kiasi, kuna wengine anakwambia kukujengea greenhouse ya ukubwa wa mita 8x30 inabidi uwalipe milioni 3 za ufundi, ambapo hiyo ni kazi ya siku mbili tu, na kama ukienda kwenye makampuni husika unajengewa bure, wewe utawapa chakula mafundi

Nakushauri wewe mkulima, ukitaka kufanya kilimo cha kisasa jitahidi kufanya utafiti kwa njia mbalimbali ikiwemo kwa INTERNET ili upate taarifa sahihi za hicho kilimo. Kwa upande wa greenhouse tafuta makampuni yanayoeleweka, nenda ukapate taarifa sahihi. Pia wenzetu Kenya wako mbele sana katika kilimo hicho, pia waweza kwenda huko ili upate uhalisia.

Jihadharini na vijana wapenda short cut
 
Aisee bwana kobe hujasomeka kabisa. Sikuelewi rudia kuandika kwa ufafanuzi zaidi
 
Aisee bwana kobe hujasomeka kabisa. Sikuelewi rudia kuandika kwa ufafanuzi zaidi

Sawa mkuu, ninachikisema hapa ni kwamba kumetokea vijana wengi wanaojiita wao ni wataalam wa kilimo katika greenhouse, lakini ukiwachunguza si wataalam, wataishia kukujengea greenhouse kwa bei ya juu na kukuchaji pesa mara mbili ya gharama halisi.

Pia maelekezo ya jinsi ya kulima yanakuwa ni ya uongo maana unakuta wao wenyewe hawana uzoefu zaidi ya kuhudhuria semina siku 2 huko Kenya. Mfano humu kwenye JF kuna aliejitangaza kuwa anafundisha kilimo cha greenhouse, lakini anasema ujuzi ameona kwa mjomba wake
 
W

Inapotokea hawa vijana wakafanikiwa kukudanganya kuwa wao ni wataalam baadhi ukimbilia Kenya kuleta wajenzi, au wao wenyewe kwa kubahatisha uhamua kukujengea, pia wanakuchaji pesa nyingi sana kupita kiasi, kuna wengine anakwambia kukujengea greenhouse ya ukubwa wa mita 8x30 inabidi uwalipe milioni 3 za ufundi, ambapo hiyo ni kazi ya siku mbili tu, na kama ukienda kwenye makampuni husika unajengewa bure, wewe utawapa chakula mafundi

Nakushauri wewe mkulima, ukitaka kufanya kilimo cha kisasa jitahidi kufanya utafiti kwa njia mbalimbali ikiwemo kwa INTERNET ili upate taarifa sahihi za hicho kilimo. Kwa upande wa greenhouse tafuta makampuni yanayoeleweka, nenda ukapate taarifa sahihi. Pia wenzetu Kenya wako mbele sana katika kilimo hicho, pia waweza kwenda huko ili upate uhalisia.

Jihadharini na vijana wapenda short cut

Kweli nieamini kila binaadam ana Weekend yake kwenye maisha ya sasa
Mbona Nkobe hueleweki,unajichanganya kwenye maelezo yako,unaona aibu kama vile unatongoza mzee.

Hapo kwenye red ndio umenimaliza kabisaaa.

Na inakuwaje wewe unamlipa mtu pesa ya Greenhouse wakati kuna makampuni yanafahamika kwa kazi hiyo.
Mali ya Bahili huliwa mara tatu,ndio kimechokukuta.

Sasa wewe ni mkulima Kanjanja umekutana na wataalam Makanjana=Kanjanja Farming Project
Sasa tatizo lipo wapi hapo.
 
Nahitaji kujua update za bei za drip lines, pia matumizi ya maji ktk ekari moja kwa mara moja tank lita ngapi linatosha?
 
Back
Top Bottom