Elections 2010 Kilichonishtua Juu Ya Dr Slaa Pale Mwembetogwa

huyu ni yule majid wa ccm au ? hutupati ng'o. eti hawajui ofisi za chadema. sisi tunataka mabadiliko tutamchagua dr Slaa. habari za chama chake hatuna mpango nazo. mi nakaa karibu kabis na ofisi za chadema makao makuu lakini .lakini sijawahi hata kutia mguu pale wala kuomba kadi yao ila kura yangu ni kwa Dr.slaa
 
maggid amefanya kile ambacho wengi hatutaki kukisikia ingawa ni muhimu. ni vema tukajisahihisha. dr slaa ni mwa jf atasoma na kujirekebisha, he isi a human, na kukkosolewa ndo maisha
 
zakwako zenye mvuto na zilizo ndani ya uwezo wako ziko wapi tuzisome? uchambuzi wako wa kisayansi na kisomi uko wapi ndugu nikazisome? labda mwenzetu unauwezo wa kuchanganua mambo na labda makala zako ni more analogy!!! tafadhali naomba nisome makala zako ili niweze kuzilinganisha na za Majjid kwani unaonesha wewe ni mahiri zaidi ili tunufaike na uchambuzi wako!! usiandike kwa mate na hali wino upo!!!

Ndege wenye rangi moja......
 
Asante Maggid kwa uchambuzi wako.

Uchambuzi huu umenifungua macho juu ya nini hasa kilijiri kwenye viwanja vya Mwembetogwa. Kwa mtazamo wangu uchambuzi wako ni mzuri na unaweza kumsaidia Dr. Slaa kuutafakari kwa kina ule uliouita kuwa ni udhaifu wake. Ila kuna mambo ambayo nimeshindwa kuelewa kwa nini wewe unadhani ulikuwa ni udhaifu wa Dr. Slaa.

Mojawapo ni hili la kutokumtaja Monica Mbega. Ninavyojua mimi Monica Mbega ni mgombea ubunge wa CCM na huu haukuwa mkutano wa kampeni wa CCM. Lengo kubwa la Dr. Slaa lilikuwa ni kuwapigia kampeni wagombea wa CHADEMA. Kumtaja Monica Mbega kwenye hadhara ile lingekuwa ni kosa la kimkakati kwani angempa "free publicity" mgombea wanayepambana naye. Yawezekana ni kweli kama unavyosema kuwa kulikuwa na wanachama wa CCM kwenye mkutano ule lakini ukweli ni kuwa walikuja pale kumsikiliza mgombea urais wa CHADEMA akinadi sera za chama chake na wagombea wa chama chake.

Jingine ni hili wazo kuwa huenda Dr. Slaa hapati muda mwingi wa kutafuta taarifa zenye kuwagusa watu walio mbele yake kumsikiliza. Hili limeorodheshwa kama moja ya madhaifu ya Dr. Slaa lakini sikuona sehemu yoyote katika uchambuzi wako ambapo umeelezea kwa kina matatizo ya wananchi ambayo unadhani kuwa Dr. Slaa hana taarifa nayo.

Kingine unaeleza kuwa kwa mtazamo wako unadhani kuwa kujazana kwa watu wengi pale Mwembetogwa kulichangiwa pia na namna CCM ilivyoboronga katika kumpata mgombea ubunge jimbo la Iringa Mjini. Hili nalo kwa mtazamo wangu hujalitolea ufafanuzi wa kutosha. Katika uchambuzi huu huu umeeleza kuwa watumishi wengi wa serikali walihudhuria mkutano wa Dr. Slaa tofauti na miaka ya nyuma ambapo walikuwa na hofu ya kuonekana wanaunga mkono upinzani. Je huoni kuwa kujitokeza kwa watu wengi inaweza pia kuwa ni dalili za ongezeko la uelewa wa watu juu ya haki zao linalowasukuma kuwa tayari kusikiliza sera za wagombea mbalimbali wanaotafuta kura zao?

Katika kuhitimisha umeeleza kuwa tatizo la CHADEMA na vyama vingi vingine vya upinzani linabaki pale pale; oganaizesheni. Umeeleza pia kuwa kuwa wengi katika umati ule uliokusanyika pale Mwembetogwa hawajui zilipo ofisi za CHADEMA mjini. Hawawajui makada wa Chadema. Ungeboresha sana uchambuzi wako kama ungenonesha matokeo ya watu uliowahoji, japo kwa uchache, pale kwenye mkutano na wakakiri kuwa hawajui ofisi za CHADEMA zipo wapi.

Lakini pia umeeleza kuwa Mkutano kama ule ilikuwa ni fursa kwa Chadema kuwatambulisha makada wa Chadema na wapi wapenzi wa Chadema waende kupata taarifa za chama chao. Kimsingi nakubaliana na wewe kuwa ilikuwa ni fursa nzuri kwa Dr. Slaa kufanya hayo ambayo umeyapendekeza. Lakini lazima kukumbuka kuwa lengo hasa la mkutano kama huu ni kuwaomba wananchi kura kwa kunadi zera za CHADEMA. Kama angetumia dakika kadhaa kutangaza ofisi za CHADEMA na kuwanadi makada wa chama angepunguza muda wa dakika 43 aliotumia kuhutubia wananchi. Kwa bahati mbaya CHADEMA hawana fursa ya kuendelea na mikutano kibabe mpaka saa moja usiku kama wanavyofanya washindani wao wa CCM. Hivyo kila dakika ni muhimu katika kutimiza lengo hasa la mkutano husika la kunadi sera za chama.
 
Duu nyie watu, mmedata:

Chai Na Chapati Ya Maji Nyumbani Kwa Kaka Michuzi



Leo nilipata heshima ya kukaribishwa nyumbani kwa ndugu yangu Muhidin Issa Michuzi. Hapo nikakaribishwa chai ya nguvu iliyowekwa viungo na kitafunwa cha chapati ya maji. Mchana ukaingia, ikawekwa pilau ya nyama mezani na vyote vyenye kuendana nayo. Basi, nikiwa na Michuzi huwa tuna mengi ya kuongea, kukumbushana na kucheka pia. Nikirudi Iringa nitajitahidi nipike chapati ya maji!

Wapenda chapati wewe!!! eeeh!

Haya bana! Ina maana JK anweza kuwapa shavu la U-DC watu kama hawa!!! Wapendao chai na pilau, siju nn!!!
 
Na wewe mtani wangu kwani ni lazima ujibu kila kitu?

Wewe kama mwandishi uwe unaandika tu unayoyaona yanafaa kuandika.

Sisi kama Wasomaji tutasoma na kuamua kama kweli wewe ni MWAANDISHI kweli au na wewe ni Chambio la Mafisadi.

Jisikie huru kuandika unachotaka na sisi tuache tuwe HURU kukutafutia kundi unalostahili kuwa.

Acha kuandika na baadaye kuja hapa KUTETEA maelezo yako. Hata uandike kumsifu Slaa, wengine bado watakushambulia.

Nafuatilia sana makala zako. Mwenye akili anakuelewa na asiye na akili basi kazi kwake. Kuna wengine wanataka kutafuniwa kila kitu ila ujumbe wako wa kijibwa cha Manzese, ulisema yote.

Mbona hatukaribishani kwenye Ulanzi sasa? Mie ngoja nisema, karibu basi Sikonge, maembe yataanza hivi karibuni.

Kazi ataikamilishaje??
 
Wewee,

achana na Chapati bwana. Na chapati zenyewe za Michuzi, i wish na mie ningelikuwepo.

Lazima nikiri kuwa na mie ni mpenzi sana wa Chapati ila sema sifahamu kuzitengeneza.

Nikifika Iringa basi ntamtafuta Maggid kwa udi na uvumba ili nikapate Chai na Chapati. Ntajikaribisha mwenyewe heheheee :)
Wapenda chapati wewe!!! eeeh!

Haya bana! Ina maana JK anweza kuwapa shavu la U-DC watu kama hawa!!! Wapendao chai na pilau, siju nn!!!
 
Nilidhani kuwa ni Mwandishi tu. Ila kwa sababu jamaa ni Mwalimu na kama sikosei anapenda sana mijadala, basi anavyofanya ndiyo haswaaa inatakiwa afanye. Akiandika juu ya CCM sidhani kama watu watajadili. Anaangalia mkondo wa maji na kujitahidi kuwa kama Samaki kwa kukinzana nao. Nimekubaliana naye kwa hilo kwani hii makala imeleta maelezo mengi zaidi ya kama angeliandika kumsifu Slaa.

Au wewe unaonaje? Mie nimemkubali kuwa Maggid ni Mwalimu Mzuri na atakuwa anawapa wanafunzi wake wakati mzuri sana na hata wanaporudi nyumbani wanakuwa wanafikiria au kujadili na wazazi wao juu ya mada ya ijayo au iliyopita.
Kazi ataikamilishaje??
 
Noooo, usiwe neutral, be specific, unajua unaweza ukawa na kitu kizuri lakini kikaonekana kibaya kutokana na jinsi ulivyokiwasilisha.
Wewe uko upande gani? Au lengo lako nini?
 
Kiuhalisia CCM hawana jipya na hilo halina ubishi. Ahadi hizi ni zile zile miaka nenda rudi kama wanavyofanya katika Bunge la bajeti. Lakini strategy za kuwaong'oa nazo bado ni loose. Inahitajika organisation ya kueleweka yenye kuweka wanafiki kando, wabaguzi wa kidini au kikabila pembeni, maslahi ya nchi mbele, ubabaishaji na udikteta mbele na maadili yaliyotukuka hapo ndio nchi yetu itakombolewa kwa sasa ni blah blah yu ndio zinaendelea.


Mkuu inabidi tuweke ubabaishaji na udikteta mbele! Then kazi ipo.

Halafu when i read you very itelligibly naona ni kati ya watu ambao upo ok na status quo na hupendi mabadiliko kwani yatapoteza ile comfort zone uliyopo.

Ila sisi wenzako we want to see every Tanzanian and not only a few, benefit from country spoils, we want to see manzese ikiwa na tumaini jipya, watoto wakisoma na kupata maisha mazuri. That can only be achieved when your government (CCM) is replaced with the well envisioned one,as for now we want to see what Dr. Slaa has in store for us.
 
Anachosema ni kweli kashfa za EPA, Deepgreen etc azumngumze huku mjini hasa hapa DAR. Akijita kwamba Kagoda peke yake alichota Bil.40 ambazo ni sawa na kilometa kadhaa za barabara hapa mjini tungekuwa na kero kidogo ya foleni. JK must be a worried man!!
 
Mjengwa mbona hukutuambia ulichokiona uwanja wa Sanora alipotembelea JK na pia kutoa uchambuzi wa strengths na weaknesses zake. Bado inaonekana unaogelea kwenye dimbwi la kutaka kutuaminisha CCM na JK are perfect na wengine ni wakulinganishwa.

You said it, kwanini haleti uchambuzi wa JK na Lipumba?
 
Ndugu Zangu,

Nimeona mada niliyoianzisha kwenye mjengwablog imeingizwa humu na wengi wameshiriki kuichangia, na mimi pia. Mada inasema " Nilichokiona Jana pale Mwembetogwa". Lakini ziada ya pale Mwembetogwa ni ukweli kuwa mwanzoni kabisa mwa hotuba yake, Dr Slaa alitoa kauli mbele ya umati ule. Kauli ambayo binafsi niliisikia na ilinishtua sana. Dr Slaa alisikika akitamka kuwa kuna kiongozi wa mkoa ( CHADEMA) ( Alimtaja jina) ambaye amehongwa na mgombea ubunge wa CCM jimbo lingine la Iringa ( naye alimtaja jina) ili asirudishe fomu zake. Dr Slaa akataka kiongozi huyo wa zamani wa CHADEMA apuuzwe na akitaka aende mahakamani.

Nadhani katika wakati huu kuna umuhimu wa kuwafahamu zaidi wagombea wetu. Na kumtakia mema Dr Slaa ni pamoja na kumwambia yale tunayoyaona ni mapungufu. Si kummwagia sifa tu. Maana, kwa kitendo kile, Dr Slaa kwa mtazamo wangu alimdhalilisha kiongozi yule wa CHADEMA mbele ya umati ule. Na bahati mbaya au nzuri kiongozi huyo wa CHADEMA alikuwapo. Kwa macho yangu nilimwona kiongozi huyo wa CHADEMA akishiriki kupiga makofi kuungana na umati uliokuwa ukishangilia kauli ya Dr Slaa. Masikini, kiongozi yule wa CHADEMA, bila shaka alipigwa na butwaa na hakuwa na la kufanya bali naye kupiga makofi!

Kwangu nilishtushwa na kusikitishwa sana. Bado naamini Dr Slaa hakumtendea haki kiongozi yule wa CHADEMA. Kama Dr Slaa alikuwa na ushahidi wa alichokisema, basi, hakuwa na haja ya kumtuhumu na kumtolea hukumu kiongozi yule pale hadharani. Kiongozi yule wa CHADEMA aliyehukumiwa hadharani ni mwanajamii hapa Iringa. Ameshapigwa mhuri mbaya bila hata kupewa fursa ya kujitetea. Kwa mzazi kama mimi naelewa jinsi kiongozi yule atakavyojisikia vibaya mbele ya familia yake, mke na watoto wake. Kwamba ametoka kwenye mkutano wa mgombea urais huku yeye akitajwa hadharani kuwa amehongwa asirudishe fomu.

CHADEMA wana vikao vyao, kwa kutanguliza busara wangeyamaliza ya kwao kwenye vikao vyao vya ndani, si hadharani. Na kama mgombea Urais, Dr Slaa anapaswa awe mfano wa kuheshimu utawala wa sheria. Hili ningelisema kama nilivyolisema hata kama lingefanywa na Kikwete wa CCM, Lipumba wa CUF au mgombea ye yote yule. Nisingelisikia nikalinyamazia. Kuandika ni kushauri pia. Tusingependa Dr Slaa apitishwe njia ya Mrema, ina miba na matope. Anayesoma na kuhusika na kilichoandikwa ana uhuru wa kupokea ushauri na kuufanyia kazi au kuachana nao. Nimechokoza mjadala....

Maggid,
Iringa.
 
Hatudanganyiki, Kama wataka kuwa Mwandishi wa habari wa Raisi Kikwete basi tumia njia nyingine!
 
Back
Top Bottom