Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Najua wapo waliokerwa hasa na dhana kuwa miaka "hamsini" haihusiani na "Tanzania" wala "Tanzania Bara" bali yanahusiana na "Tanganyika". Hawa walipenda maadhimisho yaitwe kwa haki kabisa kuwa ni ya uhuru wa "Tanganyika". Tukiondoa hilo ambalo ni dhahiri kwa baadhi ya watu kuna vitu vingine vimekera sana kiasi kwamba unatamani hata siku kuu nzima ingeahirishwa hadi tuweze kuipatia.
Umeona toka Januari - Rais alipotangaza maadhimisho haya makubwa - taasisi zikifanya maonesho, matangazo ya kiile kinachoitwa "mafanikio ya miaka hamsini". Lakini kilele cha yote ni maadhimisho makubwa yaliyofanyika Alhamisi usiku (sijui mikoani walifanya nini siku hiyo) na yale ya Uwanja wa Uhuru. Na kati ya hapo pote kuna mengi yamefanyika.
a. Je umefurahia kuwa maadhimisho yameenda kama ulivyotarajia?
b. Je, kuna vitu ambavyo ulidhani vitafanywa lakini havikufanyika?
c. Je vile vilivyofanyika vimefanyika kwa uzito unaoonekana.
d. Taarifa za sasa kwamba tumetumia karibu bilioni 70 kufanikisha maadhimisho haya unaamini yameendana na hela zilizotumika au ni fedha kidogo sana au nyingi sana?
Kama unaona hakuna kilichokukera bila ya shaka kipo kilichokufurahisha sana na unatamani yakifanyika ya Muungano basi yafanane na haya.
Umeona toka Januari - Rais alipotangaza maadhimisho haya makubwa - taasisi zikifanya maonesho, matangazo ya kiile kinachoitwa "mafanikio ya miaka hamsini". Lakini kilele cha yote ni maadhimisho makubwa yaliyofanyika Alhamisi usiku (sijui mikoani walifanya nini siku hiyo) na yale ya Uwanja wa Uhuru. Na kati ya hapo pote kuna mengi yamefanyika.
a. Je umefurahia kuwa maadhimisho yameenda kama ulivyotarajia?
b. Je, kuna vitu ambavyo ulidhani vitafanywa lakini havikufanyika?
c. Je vile vilivyofanyika vimefanyika kwa uzito unaoonekana.
d. Taarifa za sasa kwamba tumetumia karibu bilioni 70 kufanikisha maadhimisho haya unaamini yameendana na hela zilizotumika au ni fedha kidogo sana au nyingi sana?
Kama unaona hakuna kilichokukera bila ya shaka kipo kilichokufurahisha sana na unatamani yakifanyika ya Muungano basi yafanane na haya.