Nikupateje
JF-Expert Member
- Dec 22, 2009
- 1,334
- 988
Tumeshajadili na sitaki kurudia kauli ya John Mnyika kutolewa nje bungeni aliposema kuwa Rais Kikwete ni kiongozi dhaifu.
Mwaka jana David Kafulila ilikuwa hivihivi alitakiwa kufuta kauli yake aliposema serikali ya legelege haikusanyi kodi. Kafulila kama Mnyika alikataa katakata kufuta kauli yake. Lakini Kafulila alienda mbali kwa kusema kuwa hafuti kauli kwa sababu ame-quote hotuba ya Julius Nyerere iliyosema:...Serikali Corrupt haikusanyi kodi...Kesi ikaisha maana ni kweli wengi tunaijua hii kauli.
John Mnyika naye angeweza kusema kuwa kusema Rais wa nchi ni kiongozi dhaifu si kumdhalilisha kwani yeyote angeweza kum-quote Julius Nyerere pia.
Je, Mnyika angemnukuu Julius Nyerere wapi? Soma kitabu cha Nyerere kiitwacho UONGOZI WAKE NA HATIMA YA TANZANIA. Sentensi ya mwisho kwenye ukurasa wa 50 inasema hivi:
{..Rais Mwinyi ni mtu mwema na mpole, lakini ni kiongozi dhaifu; au upole wake na udhaifu wake unatumiwa na watu ambao wala si wema wala wapole kuhatarisha umoja na amani ya nchi yetu..}.
Hapa Mnyika angekuwa amemaliza kesi kama mwenzake Kafulila kirahisi kabisa.
Na wala tusingefikia hatua ya kulifanya neno DHAIFU kupata umaarufu ulioanza masaaa kadhaa baada ya kutimuliwa Mnyika hadi kufanya T-SHIRT zenye neno hilo (DHAIFU) kupanda gharama kama kiatu kilichomponda George Bush kilivyopanda bei baada ya yule mwandishi Muntadhar al-Zaidi kumtupia hicho kiatu.
Mwaka jana David Kafulila ilikuwa hivihivi alitakiwa kufuta kauli yake aliposema serikali ya legelege haikusanyi kodi. Kafulila kama Mnyika alikataa katakata kufuta kauli yake. Lakini Kafulila alienda mbali kwa kusema kuwa hafuti kauli kwa sababu ame-quote hotuba ya Julius Nyerere iliyosema:...Serikali Corrupt haikusanyi kodi...Kesi ikaisha maana ni kweli wengi tunaijua hii kauli.
John Mnyika naye angeweza kusema kuwa kusema Rais wa nchi ni kiongozi dhaifu si kumdhalilisha kwani yeyote angeweza kum-quote Julius Nyerere pia.
Je, Mnyika angemnukuu Julius Nyerere wapi? Soma kitabu cha Nyerere kiitwacho UONGOZI WAKE NA HATIMA YA TANZANIA. Sentensi ya mwisho kwenye ukurasa wa 50 inasema hivi:
{..Rais Mwinyi ni mtu mwema na mpole, lakini ni kiongozi dhaifu; au upole wake na udhaifu wake unatumiwa na watu ambao wala si wema wala wapole kuhatarisha umoja na amani ya nchi yetu..}.
Hapa Mnyika angekuwa amemaliza kesi kama mwenzake Kafulila kirahisi kabisa.
Na wala tusingefikia hatua ya kulifanya neno DHAIFU kupata umaarufu ulioanza masaaa kadhaa baada ya kutimuliwa Mnyika hadi kufanya T-SHIRT zenye neno hilo (DHAIFU) kupanda gharama kama kiatu kilichomponda George Bush kilivyopanda bei baada ya yule mwandishi Muntadhar al-Zaidi kumtupia hicho kiatu.