Kichankuli
JF-Expert Member
- Dec 18, 2008
- 887
- 189
Kama kumbukumbu zangu ziko vizuri, wazo la kuanzisha tuzo hii hapa Tanzani lililetwa na Mwanamziki marehemu James Dandu, sikumbuki mwaka. Kwa sasa tuzo hii imepanuka, kukomaa na kupata umaarufu mkubwa sana ndani na nje ya nchi. Masikitiko yangu ni namna ambavyo waandaaji wa tuzo hizi wameshindwa kuenzi juhudi za marehemu Dandu na badala yake wadhamini ndiyo wamehodhi tuzo hiyo.
Ushauri wangu kwa Waandaaji ni kwamba wangeweza kubadili jina la tuzo hii ili pia lijumuishe jina la Muasisi wake, mathalani, mashindano yanaweza kujulikana kama Mtoto wa Dandu Kilimanjaro Music Award.
Nawasilisha kwa maoni toka kwa wadau
Ushauri wangu kwa Waandaaji ni kwamba wangeweza kubadili jina la tuzo hii ili pia lijumuishe jina la Muasisi wake, mathalani, mashindano yanaweza kujulikana kama Mtoto wa Dandu Kilimanjaro Music Award.
Nawasilisha kwa maoni toka kwa wadau