Kilewo: Wabunge wa Dar acheni kulalamikia kauli ya Magufuli, chukueni hatua

Tanzania bila dikiteta kama kagame au kumzidi, hatuendi mbele. Bora huyo dicteta awe na nisa safi ya maendeleo
 
Yaani unaweza kuona uongozi wa pamoja wa wabunge wetu wa Dar es Salaa! kama siyo wabunge wote, viongozi wengi wa kuchaguliwa hapa Tanzania.

Wameungana pamoja kutetea nauli za kigamboni, kwa maslahi ya kisiasa kama alivyosema mh. Dewji na si jingine.

Nilisikia kwenye redio, wapo redio kwamba kuna zahanati / hospitali inayoitwa Tungi Kigamboni, dawa za mseto wanazo dozi kumi kwa ration ya miezi mitatu, daktari kwa sasa yupo likizo hakuna wa kumshikia nafasi yake, maabara haina mpimaji vipimo, ukiugua wanabashiri huu utakuwa ni ugonjwa fulani, halafu unaandikiwa dawa ya kununua duka la dawa.

Zahanati hiyo ipo Kigamboni, lakini mbunge wa eneo hana habari kushughulika na matatizo hayo na mengineyo.

Ukiwauliza hawa wabunge, kazi za msingi walizo ahidi kufanya, hawajafanya chochote kwa tathimini ya mwaka mmoja waliopo madarakani.

Mbunge wangu, madaraja yameharibiwa na mvua, barabara zimeharibika, lakini mbunge wetu hajafanya mkutano wowote na wapiga kura wake, lakini amepata muda wa kwenda press conference.

Tunaweza kujiuliza swali la msingi Tanzania, hivi viongozi wa kuchaguliwa, wabunge, serikali za mitaa, madiwani wanaonyesha uongozi wowote? Au uongozi hauwezi Tanzania ? Basi kwanini tunapoteza muda kuchagua viongozi ??

Mkuu nadhani hiyo hospitali ipo Tundwisongani kwa akina Angelina Lukindo wa WAPO Radio! Maabara ipo lakini haina Mpimaji!! Daktari yupo likizo hakuna wa kumshikia!!

Kweli wanasiasa wana shida yaani wakiona sehemu kuna kura basi wanaweza kufanya lolote ili wazipate hizo kura: Zungu alikataa watu wasihame jangwani na matokeo yake wamepoteza maisha! Biashara sasa hapa Dar ni kila mahala hata katikati ya barabara lakini hao wanaofanya biashara ni wapiga kura hivyo hawaguswi!! Mambo shagala baghala kwa sababu wa kuwaogopa wapiga kura. Tunashindwa kutekeleza sheria zilizopo kwa sababu ya wapiga kura! Watu wanauza mapanga barabarani hatuwasemi kwa sababu ni wapiga kura. Siku mtu akiwapoka mapanga yale akawacharanga watu sijui tutasemaje!! Nadhani tutawaachia kwa kuwa ni wapiga kura.

Sheria ina sehemu yake na wapiga kura wawe na sehemu yao, tusichanganye! Ni vema tukawaelimisha wapiga kura kufuata sheria na siyo kuwafanya wawe waasi kila mahala kwa kuwa tu wana kitambulisho cha kupiga kura!
 
Tuache unafiki, sasa kama ni katibu wa CDM hapa jijini kilichokushinda kuitisha iyo move unayotaka wabunge waitishe ni nini? CDM si ndio chama cha mapambano? Kwa nini wewe umeshindwa kuyaongoza hayo mapambano ya kupinga nauli na mengine unayoona yatalifanya jiji la Dar kuwa active wakati uko kwenye chama cha wapiganaji. Au wewe ndo kenge kwenye msurur wa mamba.? Ng'atuka bana acha kutuletea usaniii hapa. Nilitegemea kauli hii itolewe na kiongozi wa magamba lakini si CDM
 
kama wewe ni kiongozi wa chama ndani ya dar, ulishindwa nini na wewe kuwaongoza wananchi kuzidai haki zao kama hawo wabunge wameshindwa?
Kwani kulipa nauli halali ni suala la haki nalo? Mbona hao wabunge wengine wana bishara ya daladala wasishushe nauli za daladala zao au wasafirishe wananchi bure kama kweli wanawapenda wananchi wao?
Hiyo ni siasa tupu.
Maghufuli, chapa kazi kijana
 
Maisha yazid kua magum sana kwa mtanzania wa kipato cha chini, hivi madin, wanyama na kodi kubwa tunazotozwa ZnaFANYA nini? Kama hata umeme tu nao washida, SEKTA YA AFYA, WALIM na mambo mengine YAMUHIM WAYaPUUZA KWA KUTOANDAA MALIPO YAO YA KUANZA KAZI! AaaH MI KIUKWEL AWAMU HII YA NNE IMENICHOSHA NA ANANIKERA SANA HUYU, KWA UPUUZI ANAOUCHEKEA, KWANN ASIWE MKALI NA KUKEMEA UJINGA UNAOENDELEA AAAH..
 
kwani tatizo la kupanda kwa gharama za uendeshaji limeanza mwezi wa 12?je kwa siku hizi panton hunywa mafuta kiasi gani?mantainance ya panton inagharimu kiasi gani?makusanyo ni kiasi gani?je makusanyo hayo yanaendana na idadi ya watu au mizigo inayosafirishwa na kama haiendani kuna upungufu kiasi gani?je hakuna fungu jingine ya kuendesha huduma hii?naomba wadau tutakaochangia tujaribu kujibu maswali haya.
 
Mimi niseme tu kwamba wa kulaumu si tu wabunge bali hata viongozi wa kisiasa.Dar ni makao makuu ya vyama vyote vya upinzani,kwanini hawachukui hatua? Tukija hata kwenye chama pekee tegemeo cha chadema mbona harakati zao wanafanyia tu mikoani? Mbona vyama vikubwa duniani harakati zake ziko miji mikuu? Chadema hawajawahi hata kuitisha mkutano wa hadhara hapa Dar tokea uchaguzi mkuu.Sasa badala ya kufanya haya mtegemee wabunge wa CCM waongoze harakati Dar? Think twice!

Hapo kwenye red. Dar mnajifanyaga masharobaro. Likiitwa timbwili mnajifungia kwenye viyoyozi. Hamuwezi move kama machalii wa Arusha, Mwanza na Mbeya.

Pia ulitaka CDM walale Dar ili wafanane na vyama vingine vya presi conference?
 
Hivi zile Boat za Azm Dewji ziliishia wapi?...maana nakumbuka Mh POMBE alizikomalia kweli kweli

ndio naona anajipendekeza hapo! watanzania kwa unafiki we acha tu

Jamani kwa mtazamo wangu, suala la kupandisha nauli ndio hoja hapa hakuna mtu anayependa sifa kama dewji anavyosema..... suala la kivuko cha kigamboni ni sehemu ya mahuitaji ya lazima kwa wakazi wa kigamboni, sasa hitaji la lazima unapopandisha gharana maana yake kuna matipliers effect kwa huduma nyingine pia kama kukodi gari kwa mfano ilikumleta mgojwa mjini, usafirishaji wa chakula kutoka katikati ya mji nk....
 
bado sana watanzania tunatakiwa tupokee lugha kali toka kwa viongozi wetu na gharama za maisha zipande hata mara 100 ili tuzibuke maana bado tu mambumbumbu.
 
kwanza kile kivuko ilibidi tuwe tunavuka bure. sababu kile kipo badala ya daraja. je wakijenga daraja tutakua tunatoa hela? sisi tunavukia huku vijibweni nyuma ya kwa wachina high way lakini tunalipa mia tatu tena ni mtumbwi je kwanini kile kivuko cha umma kiwe mia mbili? hapana haiwezekani. Mia
 
Dah! Kweli siasa za bongo ni habari nyingine. Kwanza, kabisa nilishtuka kuwa tumefukarishwa kiasi nyongeza ya sh. 100 inaleta mjadala wa kitaifa! Lakini baadaye nimeishia kumsikitikia Dr. Magufuli kwa kukosa mikakati sahihi ya kuwasilisha mada zake. Nilifikiri harakati za ubunge zinatosha kumtengenezea kauli maridhawa. Sasa, naona (utendaji) uwaziri umemharibia. Hivyo, hana budi kupata upya darsa la mawasiliano ili ajue kauli za kuwapa wapiga kura. Hii kuwaambia wapige mbizi ilhali wametoka kuibuka kwenye gharika juzijuzi tu ni comedy mbovu! Na hao wabunge wa DSM kweli hawana soni kulishikia bango suala hilo kiasi hicho!
 
Vyovyote atakavyosifiwa Magufuri si kiongozi Bora na Bora kiongozi. Maana angeshirikisha wadau hata kidogo angeeleweka.Pia majibu ya kibabe kama haya anayoyatoa yatamtokea puani Kwani si tulishaambiwa huko nyuma ni heli tule majani lakini ndege ya Raisi lazima inunuliwe! sasa aliyesema hivyo yuko wapi? Historia kwa kawaida ina tabia ya kujirudia. Huyu nae tutakuja muona Kisutu we ngoja tu auchezee umma.
 
Dr. Masaburi alimaliza kila kitu ila watu hawakumuelewa. He made it clear kwamba wabunge wa mkoa wa Dar wanatumia makalio kufikiria. Kauli zao kuhusu Dr.John Joseph Pombe Magufuli (MB) kuongeza nauli ya kivuko kutoka Tzs. 100 hadi 200 zimethibitisha hilo.
 
GreatThinkers,

Lazy people likes someone WHO CANt WalK TheiR TalK, Magufuri Atleast Walks His Talk


Waliowaahidi Uwongo kwa nini hamuandamani leo hii bei imekuwa Tsh.200 mnanuna.
 
Nchi hii imegawanyika mno! wabunge wetu wanatakiwa watembeleee nchi zingine "kwa hela zao" (siyo zimbabwe na wala siyo somalia....you know what? achana na nchi za Africa ) waone miji ilivyoendelea kutokana na makusanyo ya kodi. mbunge ambaye hajatoka nchi ya tanzania always ataona Dar ni kama ahera. Mji wa Dar unasikitisha mno ni mchafu sana kama ilivyokuwa london miiaka ya 1500 pale kipindupindu kilikuwa kimeota mizizi mifereji ya maji machafu ilikuwa haifanyi kazi. kwa ufupi walikuwa wanakunywa maji machafu kama ilivyo dar kwa sasa, mvua kidogo mji wote unaeelea maji machafu!. Nchi hii inahitaji wachapa kazi sio wachapa midomo hao wabunge wabuni shughuli za kuwaendeleza wapiga kura wao, inasikitisha kuona vijana wanazeekea kwenye vijiwe hawajui nini wafanye. mbunge aliye na akili ndiyo angedai hayo malipo yawafikie walengwa( hasa vikundi vya vijana vya ushirika, iwe ni barber shop au vinginevyo. Tatizo tulilo nalo ni wabunge wengi wako chini ya kiwango cha chini kuongonza.
kutokana na tafakari yangu binafsi nadhani jeuri ya wabunge hawa inatokana na jeuri ya maamuzi pingamizi kama ilivyoonyeshwa na Rais Kikwete pale alipo mpinga hadharani kuhusu ile kadhia ya mabango nchini. sasa wameona huyu mnyamwezi hana nguvu pwani na si hivyo tu pinda naye alimpandilia huko jimboni kwake na kumbeza mbele ya wapiga kura wake.
Naona maoni mengi humu yamejaa fitna, hayana upembuzi kama slogan yenyewe ya jamii forums inavyosema-kuchangua kiongozi yeyote watanzania angalieni record zake za uchapa kazi .yanayotupata sasa katika nchi hii ni makosa yetu tuliyoyafanya miaka sita iliyopita...Mangufuli he is in wrong boat.
 
Woote mnaoongea mnaongelea Magufuri kuwaambia wapige mbizi, wananchi kumzomea na kumtusi ni mnaona sawa!Kuwa kiongozi haikuondelei mtu ubinadamu na mara nyingi wengi wetu tungezomewa na kutukanwa lazima tungetukana zaidi ya hapo bora yeye kawa mstaarabu. Wengi wetu tungesema kxxxxx zenu.
Ukweli usemwe serikali sasa hivi iko ICU haina pesa, ukiangalia ukweli wa mambo Vivuko vya Kigamboni serikali inatoa Huduma, na tulipokuwa tunaenda kuchota pessa Hazina kumekauka! Hivyo kivuko lazima kijiendeshe period!!!!!
Maghufuli analiita bereshi bereshi, sio mwanasiasa ni mtendaji na tunahitaji watendaji kama hawa kumi nchi iende mbele
 
Back
Top Bottom