Henry Kilewo
JF-Expert Member
- Feb 9, 2010
- 899
- 1,084
Nukuu toka kwa Kilewo kwenye fb................
Ndugu zangu Watanzania: Hivi karibuni mkuu wa mkoa wa Dar es salaam bwana sadick, alinukuliwa na chombo kimoja cha habari, bwana sadick kupitia chombo hicho aliniponda kuwa najitafutia umaarufu kupitia wahanga wa mafuriko wale wapangaji, alipinga kauli yangu ya kuwa wapangaji wanastahili kupewa viwanja na huduma zote za msingi za kibinadamu kama ambavyo wanapewa wenyenyumba kwa kuwa waathirika wakubwa siyo wenye nyumba bali ni wapangaji. Bosi wake juzi amemuumbua kwa kuungana na Tamko la CHADEMA mkoa wa Dar es salaam nililolitoa kwa niaba ya chama.
Najiuliza ni kwanini mkuu wa mkoa alikuwa analazimisha wapangaji wasipatiwe viwanja na huduma mbalimbali za msingi..... jibu lake ni kuwa kila jiongozi tuliye naye anaangalia dili la kupiga badala ya kusimamia ukweli... ila sinto mpongeza Rais kwa hilo kwani ni wajibu wake wa kuwatumikia watanzania ila nampa pole kwakuwa na mkuu wa mkoa bomu........... Nitaendelea kuwapigania watu wangu...( Wananchi) mpaka haki itakapo tendeka kwa wote
Ndugu zangu Watanzania: Hivi karibuni mkuu wa mkoa wa Dar es salaam bwana sadick, alinukuliwa na chombo kimoja cha habari, bwana sadick kupitia chombo hicho aliniponda kuwa najitafutia umaarufu kupitia wahanga wa mafuriko wale wapangaji, alipinga kauli yangu ya kuwa wapangaji wanastahili kupewa viwanja na huduma zote za msingi za kibinadamu kama ambavyo wanapewa wenyenyumba kwa kuwa waathirika wakubwa siyo wenye nyumba bali ni wapangaji. Bosi wake juzi amemuumbua kwa kuungana na Tamko la CHADEMA mkoa wa Dar es salaam nililolitoa kwa niaba ya chama.
Najiuliza ni kwanini mkuu wa mkoa alikuwa analazimisha wapangaji wasipatiwe viwanja na huduma mbalimbali za msingi..... jibu lake ni kuwa kila jiongozi tuliye naye anaangalia dili la kupiga badala ya kusimamia ukweli... ila sinto mpongeza Rais kwa hilo kwani ni wajibu wake wa kuwatumikia watanzania ila nampa pole kwakuwa na mkuu wa mkoa bomu........... Nitaendelea kuwapigania watu wangu...( Wananchi) mpaka haki itakapo tendeka kwa wote