Babylon
JF-Expert Member
- Feb 5, 2009
- 1,332
- 82
Kilango adaiwa kusambaza kadi feki za CCM Same
Saturday, 05 June 2010
Elias Msuya
MBUNGE wa Jimbo la Same Mashariki kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Anne Kilango amedaiwa kusambaza kadi feki za CCM ili kumpa ushindi katika kura za maoni zinazotarajiwa kufanyika baadaye mapema mwaka huu.
Kubainika kwa kadi hizo, kumekuja kufuatia uandikishaji wa wanachama katika daftari la wapiga kura la CCM, unaoendelea nchi nzima.
Taarifa kutoka jimboni humo zinasema kuwa, kadi feki zimebainika katika matawi ambayo inasemekana ndiyo ngome ya Mbunge huyo ambayo ni pamoja na Tarafa za Mamba, Vunta, Mpinji na Kirangare.
Taarifa hizo pia zinasema kuwa, mbunge huyo amekuwa akiwatumia viongozi wa CCM katika kata na tarafa hizo, wakiwemo wenyeviti, makatibu na madiwani wa CCM wilayani humo.
"Makadi hayo ni feki ya CCM yaliletwa jimboni na Kilango mwenyewe na kuyakabidhi kwa watendaji wa CCM, madiwani, makatibu kata na matawi. Ni mradi wa Kilango," alisema diwani wa kata moja katika wilaya hiyo ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini kwa ajili ya usalama wake.
Diwani huyo pia alisema wahakiki walipokwenda jimboni humo, viongozi wa CCM wa kata zote waliitwa wakiwa na madaftari ya wanachama wao, na ilibainika kuwa kadi nyingi za wanachama wao, siyo halisi.
"Walipoulizwa walikiri kuwa kadi hizo walipewa na madiwani ambao nao walipewa na Mbunge Anne Kilango" alisema
Hata hivyo Katibu wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro, Sophia Kilingo aliyekuwa akiongoza uhakiki huo alipoulizwa kwa njia ya simu kuhusu madai hayo, alionyesha kushtuka na kusema kuwa ni mapema kuzungumzia madai hayo kwani bado uhakiki unaendelea.
"Wewe nani kakwambia? Siyo kweli, kwanza bado tunaendelea na uhakiki," alisema.
Alipoulizwa kuwa uhakiki huo utamalizika lini alizidi kuwa mkali.
"Wewe nimeshakwambia kuwa tunaendelea na uhakiki, kwani una haraka gani? Tukimaliza nitakwambia," alisema Kilingo na kukata simu.
Naye Anne Kilango alipoulizwa aliruka na kueleza kuwa hana sababu ya kufanya hivyo.
"Mimi ndiyo nahusika? Huyo aliyekwambia ndiye akueleze yote, sina sababu ya kufanya hivyo. Kwa heri," Alisema Kilango na kukata simu yake.
Saturday, 05 June 2010
Elias Msuya
MBUNGE wa Jimbo la Same Mashariki kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Anne Kilango amedaiwa kusambaza kadi feki za CCM ili kumpa ushindi katika kura za maoni zinazotarajiwa kufanyika baadaye mapema mwaka huu.
Kubainika kwa kadi hizo, kumekuja kufuatia uandikishaji wa wanachama katika daftari la wapiga kura la CCM, unaoendelea nchi nzima.
Taarifa kutoka jimboni humo zinasema kuwa, kadi feki zimebainika katika matawi ambayo inasemekana ndiyo ngome ya Mbunge huyo ambayo ni pamoja na Tarafa za Mamba, Vunta, Mpinji na Kirangare.
Taarifa hizo pia zinasema kuwa, mbunge huyo amekuwa akiwatumia viongozi wa CCM katika kata na tarafa hizo, wakiwemo wenyeviti, makatibu na madiwani wa CCM wilayani humo.
"Makadi hayo ni feki ya CCM yaliletwa jimboni na Kilango mwenyewe na kuyakabidhi kwa watendaji wa CCM, madiwani, makatibu kata na matawi. Ni mradi wa Kilango," alisema diwani wa kata moja katika wilaya hiyo ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini kwa ajili ya usalama wake.
Diwani huyo pia alisema wahakiki walipokwenda jimboni humo, viongozi wa CCM wa kata zote waliitwa wakiwa na madaftari ya wanachama wao, na ilibainika kuwa kadi nyingi za wanachama wao, siyo halisi.
"Walipoulizwa walikiri kuwa kadi hizo walipewa na madiwani ambao nao walipewa na Mbunge Anne Kilango" alisema
Hata hivyo Katibu wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro, Sophia Kilingo aliyekuwa akiongoza uhakiki huo alipoulizwa kwa njia ya simu kuhusu madai hayo, alionyesha kushtuka na kusema kuwa ni mapema kuzungumzia madai hayo kwani bado uhakiki unaendelea.
"Wewe nani kakwambia? Siyo kweli, kwanza bado tunaendelea na uhakiki," alisema.
Alipoulizwa kuwa uhakiki huo utamalizika lini alizidi kuwa mkali.
"Wewe nimeshakwambia kuwa tunaendelea na uhakiki, kwani una haraka gani? Tukimaliza nitakwambia," alisema Kilingo na kukata simu.
Naye Anne Kilango alipoulizwa aliruka na kueleza kuwa hana sababu ya kufanya hivyo.
"Mimi ndiyo nahusika? Huyo aliyekwambia ndiye akueleze yote, sina sababu ya kufanya hivyo. Kwa heri," Alisema Kilango na kukata simu yake.