Kila siku ni 'wasaidizi wake'... KWANINI SIYO KIKWETE mwenyewe?

Nadani suluhisho pekee ni katiba mpya.Pili natumaini wengi hatujui majukumu ya kiongozi mkuu na watendaji wake.Mimi ni baba nadhani nisipo kuwa na msimamo nzuri na ufuatiliaje si dhani kama familia yangu itakuwa bora japo kwa wasio kuwa na jicho la tatu wanaweza sema mkwe wangu hawezi kulea watoto na nk.Ila msingi mbovu na nzuri wa familia yangu ni mm mwenyewe baba.
 
MM kwa hili ulilolisema, kuna kitu kinatakiwa kufanywa ktk Serikali yote. Ikiwa kama CAG anakagua na kutuletea madudu kila mwaka ktk mahesabu ya umma, basi kuna haja ya Kufanya "HR AUDIT" Nadhani matatizo yote haya yanaanzia hapo.
 
MM, kuna siku bwana Deus Kibamba alikua anapiga sana kelele kuhusu katiba, wakati huo kulikua na vuguvugu kubwa, na jamaa alikua anasema lazima kutafanyika maandamano nch nzima, ghafla akawa bubu, kwa kama siku mbili za ukimya kwenye media, jamaa akawa anahojiwa live mlimani TV, jamaa alimwagia sifa JK na akalaumu sana watu wa chini, alimsifia sana sana!
 
Hi serikali na uongozi wake wana psychological illness BLAMING/KULAUMU kwa kila jambo. Wataalamu wanasema huu ugonjwa ni hatari na una addiction kama wabugia unga. Kwa Case Study ya serikali hii tunaweza kusema ni very infectious, Mkuu amewaambukiza watendaji wake wote.
 
Mwanakijiji
Huyu Jamaa sio kwamba yuko hands off, huyu Jamaa yuko busy, tena yuko busy kuliko marais wowote waliotangulia, na huo ambao watu wengi wanafikiria ni ukimya au kupuuzia ni matokeo ya ubusy wake.

Kikwete ni msanii toka mtoto mdogo, anaingia ndani usiku, hata kama ni kwa bahati mbaya anapiga chombo chenye maji yanamwagika alafu hasemi, kwa msaada wa giza anatoka nje taratibu kwa uangalifu mkubwa sana, ikija kujulikana maji yamemwagika wanalaumiwa wengine, na sababu za kumshuku kwamba alihusika zinakosekana sababu by that time yeye anakuwa aliishakimbilia kwa majirani anakula story (uzurulaji).

Bahati nzuri wakati wote alikuwa anakuja kubainika kwamba yeye ndio muhusika sababu kesho yake asubuhi, atakuwa ama na kidonda mguuni ambacho ni ushahidi kwamba alimwagikiwa na maji ya moto, au nguo zake kukutwa zimeanikwa wakati hazijafuliwa ikiwa ni ushahidi kwamba alimwagikiwa na maji.

Hivyo anaendeleza tabia yake, baada ya 2015 tutajua kila kitu, tujiandae kuwaomba msamaha akina Nundu na Maige.
Tutakapofanya Owner verification exercise ama kwa msaada wa Anti Money Launderig Act, au Public Officers code of ethics act au sheria nyingine yoyote ile ndio tutajua who exactly MOVED THE CHEESE.
 
mganga wa jk kiboko..yani nchi za watu wenye akili timamu keshakimbizwa ikulu,he is good for nothing

Kikwete ni muoga sana hivyo amehakikisha kuwa kote serikalini na kwenye CCM hakuna watu karibu yake wanaoweza kumkosoa bila ya kumuonea aibu; ndio maana washauri wake ni watu dhaifu na kwenye chama hakuna watu kama walivyokuwa wakina Mzee Mtandika na Rajabu Diwani ambao waliweza kumkabili Mwalimu head on!!
 
Kila siku nasema kikwete ni janga la kitaifa, ukisema mawaziri nakataa kwa kuwa kuna kikao cha baraza la mawaziri na kikwete ndiye mwenyekiti na mambo yote yanajadiliwa kwenye vikao hivyo. Iweje utekelezaji wa maagizo kwenye vikao ashindwe kuwawajibisha hadi wabunge waseme? Kikwete ni tatizo kuna rafiki yangu nimewahi kumwambia kuwa kazi anayoweza huyu jamaa ni kuwa MJUMBE WA NYUMBA KUMI BASI
 
Mzee Mwanakijiji,

Sina hakika kama nakubaliana moja kwa moja na content ya mada yako au vipi, lakini lililo wazi kwangu ni kwamba, binafsi NAKERWA, NAKASIRISHWA, NA KUCHUKIZWA sana na haya mambo kwamba eti "ameshauriwa vibaya na wasaidizi wake!" Huwa mara zote najiuliza ikiwa anashauriwa vibaya ni kwanini basi kila wakati awe anachukua huo ushauri mbaya!!

Labda ni kwanini sina hakika endapo nakubaliana moja kwa moja na content mzima wa mada yako, ni ule wasi wasi wako kwamba huenda lengo ni kumlinda na mabaya yake! Huu wala sio upuuzi wa CCM bali ni upuuzi wa Kitanzania! Hata hao wapinzani nao lugha yao ndiyo hiyo....."Rais anashauriwa vibaya na wasaidizi wake...!" Nina hakika hata wewe Mzee Mwanakijiji ningeweza kupitia post zako zote za nyuma, sina shaka yoyote nako ningekutana na madai kutoka kwako kwamba "Rais anashauriwa vibaya na wasaidizi wake...!"
 
kuna wanaosema ni waisaidizi wake kwasababu ni-wajinga
kuna wanaosema ni wasaidizi wakekwa sabab wanajua ukweli na wanapindisha, wanafaidi
kuna wanaojua ukweli kwa sababu wanampenda kikwete kwa sura yake!!
 
Naomba hii ni niifanye quote yangu for few more days:
binafsi NAKERWA, NAKASIRISHWA, NA KUCHUKIZWA sana na haya mambo kwamba eti "ameshauriwa vibaya na wasaidizi wake!" Huwa mara zote najiuliza ikiwa anashauriwa vibaya ni kwanini basi kila wakati awe anachukua huo ushauri mbaya!!
 
Raisi Kikwete anathibitisha yale ambayo professor Lipumba alisema kwamba ni Msanii

Amejijengea walinzi wa utawala wake ambao wimbo wake ni kwamba anashauriwa vibaya na watendaji na watendaji kutokana na mfumo wa uoga CCM wananyamaza na kubeba lawama

Hajali lawama kwa sababu anatumia njia za hila kwa kupitia mtoto wake Ridhiwani kukitokea malalamiko au matamko au maandamano ya wenye shida basi vikundi vya akina Tovutwa,Ulanga balazo wa Amani ya bila taasisi wanajitokeza kwenye vyombo vya habari kutetea ujinga kwa nguvu zote kwenye vyombo vya habari vyote

Hana chembe ya uongozi wakati wote wa matatizo anakimbia nchi anarudi wananchi wamekasirika mpaka wamepasuka ni mbinu ya yeye kutokuhusishwa na tatizo
Kigeugeu wale anaowatumia kwa manufaa yake kwenye ofisi alizo waweka huwaruka pindi kuna shida
Ukweli Raisi Kikwete ni Mzandiki na Mnafiki mkubwa hasaidii taifa hili mpaka 2015 tutakuwa tumepata hasara za kiuchumi kisiasa mara 10,000
 
We are almost there in knowing where the heaviest section of the burden is located. When there will not be anyone else to blame, we will have a confidence that we are there.
 


Tangu 2006 kuna mengi yametokea kuhusiana na utendaji na uongozi wa Rais Kikwete. Kuna imani ambayo imejengeka kuwa Rais "anashauriwa vibaya" na hivyo huwa anasema au anafanya vitu kwa sababu 'wasaidizi' wake wamemuelekeza vibaya n.k Kuanzia sakata la mapanki na mwitikio wake kuhusu filamu ya Darwin's Nightmare hadi hii ziara ya Marekani kuna vitu vinafanyika na mara zote watu wote hulaumiwa isipokuwa rais mwenyewe.

Tumeona kwenye CCM kama ilivyo kwenye serikali wanalaumiwa watu wengine wote isipokuwa mtu pekee ambaye anastahili kulaumiwa. Mawaziri mara nne wamelaumiwa na wananchi na mara nne ndani ya miaka sita Rais amelazimika kufanya mabadiliko. Lakini mara hizo zote wanalaumiwa ni mawaziri na watendaji isipokuwa mtu pekee mwenye uwezo wa kuwawajibisha.

Sasa itachukua muda gani kwa watu wengine kuelewa na kukubali kuwa tatizo yawezekana ni Rais mwenyewe na namna (manner) ya uongozi wake wa kukaa pembeni (hands off approach)? Yawezekana amekuwa akiachilia vitu vitokee kwa sababu hataki kubeba lawama na hivyo watu wengine kabisa walaumiwe? Kwa mfano la Lowassa analaumiwa Mwakyembe, la mawaziri wanalaumiwa watendaji wa chini, la watu kuwajibishwa wanalaumiwa wabunge n.k? Yeye mwenyewe mara zote anakuwa mtu wa kunung'unika asiyekubali kosa lolote au kuwajibika kwa lolote?

Inawezekana pia ni jitihada ya kumuonesha kuwa ame-delegate power na hivyo haitaji kujishughulisha na mambo hayo yote?

Kwani JK alichaguliwa kusudi asikilize ushauri tu? Maana taifa hili limeingia gharama kubwa kwa kigezo hicho hicho cha ushauri au washauri,.
Sasa si hakuna haja ya kufanya uchaguzi wa rais ipeke yake, na tufanye uchaguzi wa washauri kama ni muhimu namna hiyo
 

Tangu 2006 kuna mengi yametokea kuhusiana na utendaji na uongozi wa Rais Kikwete. Kuna imani ambayo imejengeka kuwa Rais "anashauriwa vibaya" na hivyo huwa anasema au anafanya vitu kwa sababu 'wasaidizi' wake wamemuelekeza vibaya n.k Kuanzia sakata la mapanki na mwitikio wake kuhusu filamu ya Darwin's Nightmare hadi hii ziara ya Marekani kuna vitu vinafanyika na mara zote watu wote hulaumiwa isipokuwa rais mwenyewe.

Tumeona kwenye CCM kama ilivyo kwenye serikali wanalaumiwa watu wengine wote isipokuwa mtu pekee ambaye anastahili kulaumiwa. Mawaziri mara nne wamelaumiwa na wananchi na mara nne ndani ya miaka sita Rais amelazimika kufanya mabadiliko. Lakini mara hizo zote wanalaumiwa ni mawaziri na watendaji isipokuwa mtu pekee mwenye uwezo wa kuwawajibisha.

Sasa itachukua muda gani kwa watu wengine kuelewa na kukubali kuwa tatizo yawezekana ni Rais mwenyewe na namna (manner) ya uongozi wake wa kukaa pembeni (hands off approach)? Yawezekana amekuwa akiachilia vitu vitokee kwa sababu hataki kubeba lawama na hivyo watu wengine kabisa walaumiwe? Kwa mfano la Lowassa analaumiwa Mwakyembe, la mawaziri wanalaumiwa watendaji wa chini, la watu kuwajibishwa wanalaumiwa wabunge n.k? Yeye mwenyewe mara zote anakuwa mtu wa kunung'unika asiyekubali kosa lolote au kuwajibika kwa lolote?

Inawezekana pia ni jitihada ya kumuonesha kuwa ame-delegate power na hivyo haitaji kujishughulisha na mambo hayo yote?

jamaa ni mjanja sana tekiniki anayotumia ndiyo inayomfanya aendelee kudumu. watu wanafanya makosa anavuta weeeeeee hadi akiona sasa haiwezekani tena kuvuta anawatosa ili kujisalimisha hivo hivo na anaendelea kudumu
 
naomba nitofautiane nawe, tatizo ni top layer yote si magamba. Si ma 'think tank'
 
Ubarikiwe sana kwa kusema ukweli mchungu.

Ni kweli mara zote hii hoja imekosa mashiko na miguu, lakini nashangaa imeendelea kutumika. Kuna mambo mawili, nionavyo:
1) JK anaogopwa sana (ni dikteta wa hisia); kiasi kwamba hakuna mwenye kudiriki kumkosoa ktk ccm na serikali.
2) Ni kweli kuna wasaaidizi wanam-sabotage kwa vile ameshindwa kusimamia mambo fulani muhimu ya kitaifa

kikwete si dikteta wala haogopwi bali walao kupitia udhaifu uliopo wanamfurahia ni kama panya wamuumapo mtu aliyelala fofofo watauma tu wala hawapulizi, hivi ndivyo nchi inavyoliwa kwa sasa. wanafiki ni tele wanaona lakini wanajifanya hawaoni watamwita Kikwete kwa nembo kubwakubwa; Dakta! mheshimiwa, haya kila siku huko USA sifa tele kwaTZ toka USA watu kimya wala hawamhoji mheshimiwa Hivi Marekani aikusifu kakupata au umempata? haya nchi ya asali na maziwa badala ya chemichemi kutobokea ngorongoro itatobokea kule carlifonia WATU WAKE KIMYA! HUKO NDIKO KUMSAIDIA RAIS? baada ya vyadarua sasa mtanyweshwa kikombe cha babu obama mbu waliongia kwenye neti zilizochakaa wakikuuma tu watakufa hapohapo
 
Back
Top Bottom